Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ibrahiim(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ibrahiim(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ibrahiim(a.s)

Tukimchukua Nabii Ibrahimu kama kiongozi wa kuigwa katika harakati za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii tunajifunza yafuatayo:



(i) Mwanaharakati hanabudi kujitakasa yenye binafsi na kuwa mnyenyekevu na mtii kamili kwa Allah(s.w) kabla ya kuiendea jamii.



(ii) Hatunabudi kuanza kulingania familia zetu kabla ya kuiendea jamii-Nabii Ibrahim alianza kumlingania baba yake Azara.



(iii) Tulinganie Uislamu kwa kutumia hoja madhubuti na mbinu mbali – Qur-an (16:125).



(iv) Tulinganie Uislamu kwa watu wa kada zote – kwa raia wa kawaida wa mijini na vijijini, wasomi na maofisa katika sekta mbalimbali na viongozi wa jamii katika ngazi mbalimbali kwa kupanga na kutumia fursa zinazojitokeza – Nabii Ibrahim (a.s) alihojiana na mfalme Namrudh.



(v) Tusimchelee yeyote katika kulingania Uislamu.



(vi) Tuwe tayari kukabiliana na machungu ya kutengwa na familia na jamii kwa ujumla kwa ajili ya kusimamisha Uislamu.



(vii) (a)Tuwe – tayari kutoa nafsi zetu, nafsi za wapenzi na wandani wetu kwa ajili ya Allah(s.w) – Qur-an (9:111).



(b) Tumpende Allah(s.w) na Mtume wake na kupigania dini yake kuliko tunavyopenda nafsi zetu na jamaa zetu wa karibu. Qur-an (9:23:24), (58:22).



(viii) Tuwe na vituo vya harakati vya kistratejia na tuwe na viongozi madhubuti katika vituo hivyo.



(ix) Tufanye harakati za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii kistratejia.



(x) Tuwe tayari kuhama makazi yetu tuliyoyazoea, kuhamia maeneo ya kistratejia kwa ajili ya kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii.



(xi) Tuandae vizazi vitakavyoturithi katika harakati – Nabii Ibrahim(a.s)aliomba watoto wema watakaomrithi katika harakati.



(xii) Tuzihusishe familia zetu katika harakati – Bi Hajarah aliridhia kubaki mwenyewe Makka na kitoto chake kichanga kwa ajili ya kutii amri ya Allah(s.w).



(xiiii)Tuwahusishe jamaa zetu wa karibu katika harakati – Nabii Ibrahim(a.s) alihama kutoka Iraq na mpwa wake Lut (a.s) na kumfanya kuwa kiongozi wa kituo cha harakati cha Transjordan.



(xiv) Tuwe wepesi wa kumuelekea Allah(s.w) kwa maombi mbalimbali ya kuomba msaada wa Allah(s.w) na kumshukuru kama alivyokuwa akifanya NabiiIbrahiim(a.s) Qur-an.(37:100-101) (14:39)



(xv) Tumuombe Allah(s.w) aturehemu na kutubariki kama alivyomrehemu na kumbariki Nabii Ibrahim (a.s) kwa kumswalia Mtume(s.a.w) mara kwa mara kama tukavyo mswalia katika swala.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2242

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Tukio la kupasuliwa kifua Mtume Muhammad S.A.W

Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7

Soma Zaidi...
Ni jitihada gan alizo zifanya sayyidna othman katika kuihifadh qur an ?

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Jitihada alizozifanya Khalifa wa Tatu katika kuilinda Quran

Soma Zaidi...
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam

β€œNa wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): β€œNitakuua”.

Soma Zaidi...
Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija

Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu.

Soma Zaidi...