Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni

'Na (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza.

Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni

Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni


'Na (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza. Akamwambia: 'Hakika mimi nitakufanya kiongozi wa watu (wote) (Ibrahim akasema): 'Je, na katika kizazi changu pia?' Akasema: '(Ndio lakini) ahadi yangu haitawafikia madhalimu.' (2:124)



Katika aya hii tunajifunza kuwa NabiiIbrahiim(a.s) alipewa uongozi na kuwa mfano wa kuigwa na walimwengu wote baada ya kufaulu mitihani mingi na mizito iliyomthibitisha kwa ulimwengu kuwa alikuwa mnyenyekevu na mtii kamili kwa Allah(s.w).



'Hakika Ibrahiim alikuwa Imamu (mfano mzuri wa wema wa kuigwa), mnyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu, mtii kamili, wala hakuwa miongoni mwa washirikina.' (16:120)



Kutokana na dua yake, Mitume wote waliomfuatia wametokana na kizazi chake. Kupitia kwa Is-haqa(a.s) kuna Mitume wote wa bani Israil, kuanzia kwa Israil (Yaquub(a.s)) mwenyewe hadi kwa Nabii Issa(a.s) na kupitia kwa Ismail(a.s) tunaye Mtume Muhammad(s.a.w), ambaye ni Mtume wa mwisho na Mtume wa walimwengu wote kama alivyokuwa babu yake, Ibrahiim(a.s).Katika Qur-an tunahimizwa kufuata mila ya Nabii Ibrahiim:




Na nani atajitenga na mila ya Ibrahimu (akaichukia Dini hii ya Kiislamu) isipokuwa anayeitia nafsi yake katika upumbavu? Na kwa yakini sisi tulimchagua (Ibrahimu) katika dunia; na kwa hakika yeye katika Akhera atakuwa miongoni mwa watu wema (kabisa). (Kumbukeni habari hii) Mola wake alipomwambia: 'Nyenyekea:' Akanena 'Nimenyenyekea kwa Mola wa walimwengu (wote)'. (2:130-131)



Na nani aliye bora kwa Dini kuliko yule ambaye ameuelekeza uso wake kwa Mwenyezi Mungu, naye ni mwema, na anafuata mila ya Ibrahimu (kuwa Muislamu kweli kweli). Na Mwenyezi Mungu amemfanya Ibrahimu kuwa ni kipenzi chake. (4:125)



Mila yaIbrahiim(a.s) inayosisitizwa hapa si nyingine ila ni kuwa 'Mnyenyekevu na mtii kamili' kwa Allah(s.w), kiasi cha mtu kuwa tayari na kwa moyo mkunjufu kumchinja mwanawe aliye mwema na anayempenda na kumtarajia sana. Pia kufuata mila ya Ibrahim ni kuwa tayari kufanya juhudi za kusimamisha Uislamu katika jamii na kutokomeza ushirikina bila ya kujali lolote litakalotokea hata kama ikibidi kugombana na kutengana na jamii nzima.



Hakika nyinyi muna mfano mzuri (wa kuiga) kwa Ibrahimu na wale waliokuwa pamoja naye, walipowambia jamaa zao (makafiri). 'kwa yakini sisi tu mbali nanyi, na mbali na hayo mnayoyaabudu kinyume cha Mwenyezi Mungu; tunakukataaeni, umekwisha dhihiri uadui na bughudha ya daima baina yetu na nyinyi mpaka mtakapomuamini Mwenyezi Mungu peke yake....' (60:4)

Ili kujikurubisha na mila ya Ibrahimu, Allah(s.w) ametuamrisha na kutufundisha kupitia kwa Mtume(s.a.w) kuwa tumuombee (tumswalie) Mtume na kujiombea sisi wenyewe kwa kusema:



'Ee Allah! Mrehemu Muhammad na wafuasi wa Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na wafuasi wa Ibrahim. Hakika wewe u mtukufu na msifiwa wa haki. Ee Allah! Mbariki Muhammad na wafuasi wa Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na wafuasi wa Ibrahiim. Hakika wewe u mtukufu na msifiwa wa Haki'.



                   

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 168

Post zifazofanana:-

kitabu cha matunda
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za Mwanamke katika jamii mbalimbali hapo zamani
Utangulizi:Uislamu unamuelekeza mwanaadamu namna nzuri ya kuendesha maisha yake katika kila kipengele cha maisha akiwa binafsi, katika familia na katika jamii. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Bamia
Soma Zaidi...

STANDARD FOUR ENGLISH TEST 00
Soma Zaidi...

Chanzo cha vita vya Ngamia Vita Kati ya Bibi Aisha na Khalifa Ali
Soma Zaidi...

Fahamu vitamini C na kazi zake, vyakula vya vitamini C na athari za upungufu wake.
kuhusu vitamini C, kuanzia chanzo chake, maana yake, upungufu wake na kazi zake kwenye miili yetu. Soma Zaidi...

Fast
Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta.. Soma Zaidi...

STANDARD FOUR ENGLISH TEST 001
Soma Zaidi...

AINA ZA MINYOO: tapeworm, livefluke, roundworm, hookworm, flatworm
AINA ZA MINYOO Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa. Soma Zaidi...

MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA
MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA. Soma Zaidi...

MARADHI MAKUU HATARI MATANO (5) YANAYOENEZWA KWA KUNG'ATWA NA MBU (malaria ndio inachukua nafasi ya kwanza)
1. Soma Zaidi...

Hoja juu ya hitajio la kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango
Soma Zaidi...