Umuhimu wa jihad katika kusimamisha uislamu katika jamii
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
- Umuhimu wa Jihad katika kusimamisha Uislamu katika jamii.
- Kusimamisha Uislamu (Jihad) katika jamii ni amri (faradh).
Kama ilivyoamrishwa swala, funga, zakat na hijja, Neno “kutiba” (mmelazimishwa) limetumika katika jihad kama lilivyotumika katika kufunga, kulipa kisasi na faradh zingine pia za kutekeleza Uislamu.
Rejea Qur’an (2:216), (2:183), (2:178,180) na (22:78).
- Msamaha na Pepo hupatikana kwa kufanya juhudi (jihad) za maksudi katika kusimamisha Uislamu katika jamii.
Kutekeleza faradh kama swala, funga, zaka na hija na ibada zingine za sunnah za binfsi, itakuwa sio sababu ya msingi ya kupata msamaha na pepo ya Mungu, mpaka jitihada ya dhati katika kupigania Uislamu katika jamii ifanyike.
Rejea Qur’an (4:74), (9:111), (61:10-13), (2:154), (3:169-171), (3:142), (3:157), (2:214) na (9:16).
- Mwenyezi Mungu (s.w) ameteremsha chuma (silaha) kuwa nyenzo ya kusimamisha Uislamu katika jamii.
Mitume wametumwa kusimamia haki na uadilifu katika jamii kwa kutumia miongozo ya vitabu vya Allah (s.w) na pia chuma (silaha) kimeteremshwa ili mitume na waumini wakitumie katika kusimamia haki na uadilifu ndani ya jamii.
Rejea Qur’an (57:25).
- Kusimamisha Uislamu katika jamii ndio lengo kuu la maisha ya Waumini.
Mwenyezi Mungu (s.w) ametubainishia kuwa chochote tutakachokipenda au tutakachokifanya nje na lengo la kusimamisha Uislamu katika jamii hatakuwa na radhi juu yetu. Rejea Qur’an (9:23-24).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Simulizi za Hadithi Audio π2 kitabu cha Simulizi π3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π4 Kitau cha Fiqh π5 Kitabu cha Afya π6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume
Uchaguzi wa βUmar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili.
Soma Zaidi...Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina
Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s.
Soma Zaidi...