Nabii Salih(a.
Nabii Salih(a.s) alifuatia baada ya Hud(a.s) na alitumwa kwa watu wa kabila (Taifa) la Thamud. Makazi yao yalikuwa kaskazini mwa Arabia sehemu iliyojulikana kama al-Hijr Madaโin Salih.
Thamud waliongoza katika teknolojia ya kuchonga majabali na kuyafanya majumba ya fahari kama tunavyofahamishwa katika Qur-an:
......
โNa kumbukeni (Allah) alivyokufanyeni makhalifa baada ya โAd na kukuwekeni vizuri katika ardhi; mnajenga majumba makubwa ya kifalme katika nyanda zake, na mnachonga majumba katika majabali (yake).........โ (7:74)
Baada ya muda kupita Thamud nao waliacha mafundisho ya Mtume Hud(a.s) kama walivyofanya akina โAd hapo zamani, wakawa wanaabudia masanamu na kufisidi katika ardhi. Ndipo Allah(s.w) akamtuma Nabii Salih(a.s) kulingania Uislamu kwa wakazi wa Hijr.
Nabii Salih(a.s) aliwalingania watu wa kaumu yake, wamwamini Allah(s.w) na kumuabudu ipasavyo, watubie na waombe msamaha kwa dhambi zao:
โNa kwa Thamud tukampelekea ndugu yao, Salih, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Allah; nyinyi hamna Mungu ila yeye. Yeye ndiye aliyekuumbeni katika ardhi, na akakukalisheni humo. Basi muombeni msamaha, kisha mrejee kwake. Hakika Mola wangu ni karibu (na waja wake) anapokea (maombi yao).โ (11:61)
Nabii Salih aliendelea kuwalingania
โMcheni Mwenyezi Mungu na nitiini.โ โWala msitii amri za wale maasi, (wenye kupindukia mipaka ya Mungu).โ โAmbao wanafanya uharibifu tu katika ardhi wala hawaitengenezi.โ (26:150-152)
Umeionaje Makala hii.. ?
(i) Tujitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu kuondoa maovu katika jamii kwa mikono yetu na ikiwa hatuwezi tuyakemee kama alivyofanya Nabii Lut(a.
Soma Zaidi...