HISTORIA YA NABII SALIH(A.S

Nabii Salih(a.

HISTORIA YA NABII SALIH(A.S

HISTORIA YA NABII SALIH(A.S)


Nabii Salih(a.s) alifuatia baada ya Hud(a.s) na alitumwa kwa watu wa kabila (Taifa) la Thamud. Makazi yao yalikuwa kaskazini mwa Arabia sehemu iliyojulikana kama al-Hijr Mada’in Salih.

Thamud waliongoza katika teknolojia ya kuchonga majabali na kuyafanya majumba ya fahari kama tunavyofahamishwa katika Qur-an:



......

“Na kumbukeni (Allah) alivyokufanyeni makhalifa baada ya ‘Ad na kukuwekeni vizuri katika ardhi; mnajenga majumba makubwa ya kifalme katika nyanda zake, na mnachonga majumba katika majabali (yake).........” (7:74)

Baada ya muda kupita Thamud nao waliacha mafundisho ya Mtume Hud(a.s) kama walivyofanya akina ‘Ad hapo zamani, wakawa wanaabudia masanamu na kufisidi katika ardhi. Ndipo Allah(s.w) akamtuma Nabii Salih(a.s) kulingania Uislamu kwa wakazi wa Hijr.



Ujumbe wa Nabii Salih(a.s) kwa Watu Wake


Nabii Salih(a.s) aliwalingania watu wa kaumu yake, wamwamini Allah(s.w) na kumuabudu ipasavyo, watubie na waombe msamaha kwa dhambi zao:




“Na kwa Thamud tukampelekea ndugu yao, Salih, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Allah; nyinyi hamna Mungu ila yeye. Yeye ndiye aliyekuumbeni katika ardhi, na akakukalisheni humo. Basi muombeni msamaha, kisha mrejee kwake. Hakika Mola wangu ni karibu (na waja wake) anapokea (maombi yao).” (11:61)

Nabii Salih aliendelea kuwalingania



“Mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini.” “Wala msitii amri za wale maasi, (wenye kupindukia mipaka ya Mungu).” “Ambao wanafanya uharibifu tu katika ardhi wala hawaitengenezi.” (26:150-152)



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1554

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana: