image

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo

Adam(a.

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo


Adam(a.s) aliumbiwa mkewe kutokana na asili ile ile kama tunavyojifunza katika Qur-an:



Enyi watu! Mcheni Mola wenu ambaye amekuumbeni katika nafsi (asili) moja. Na akamuumba mkewe katika nafsi ile ile. Na akaeneza wanaume wengi na wanawake kutoka wawili hao...........” (4:1).

Adam(a.s) na mkewe waliwekwa katika Bustani (Pepo) na wakapewa uhuru wa kufurahia wapendavyo ndani ya bustani hiyo na kula matunda yote wapendavyo lakini

wasikurubie matunda ya mti moja tu waliobainishiwa. Iblis (shetani), alimlaghai Adam(a.s) na mkewe wakala matunda ya mti ule waliokatazwa.



(kisha Allah akasema): “Na wewe Adamu! Kaa Peponi pamoja na mkeo, na kuleni mnapopenda, lakini msiukaribie mti huu msije kuwa miongoni mwa waliodhulumu (nafsi zao).” (7:19)



Basi Shetani; (naye ni yule Iblisi), aliwatia wasiwasi ili kuwadhihirishia aibu zao walizofichiwa, na akasema: “Mola wenu hakukukatazeni mti huu ila (kwa sababu hii) msije kuwa Malaika au kuwa miongoni mwa wakao milele (wasife).(7:20)




Naye akawaapia (kuwaambia): “kwa yakini mimi ni mmoja wa watowao shauri njema kwenu.” Basi akawateka (wote wawili) kwa khadaa (yake). Na walipouonja mti ule, aibu zao ziliwadhihirikia na wakaingia kujibandika majani ya (miti ya huko) Peponi. Na Mola wao akawaita (akawaambia) “Je, sikukukatazeni mti huu na kukwambieni ya kwamba Shetani ni adui yenu aliye dhahiri?” (7:21-22)
Tofauti na Iblis ambaye baada ya kumuasi Mola wake hakujuta

hata baada ya kukumbushwa, Adam(a.s) na mkewe walijuta sana kwa kumuasi Mola wao kisha wakalalama kwake kuleta toba:



“Mola wetu! Tumedhulumu nafsi zetu; na kama hutatusamehe na kuturehemu, bila shaka tutakuwa miongoni mwa wenye khasara (kubwa kabisa)”. (7:23).

Kisa cha kulaghaiwa Adam na Hawwah na adui yao Ibilis mpaka wakamuasi Mola wao kwa kula matunda waliyokatazwa, kinatufunza kuwa kuna maadui wasiopenda kuona Allah(s.w) anatiiwa ipasavyo katika kuendea kila kipengele cha maisha ya kila siku. Na adui mkubwa kwa waumini ni shetani ambaye huingia katika nyoyo za watu na kuwahadaa kwa kuwapambia mambo maovu na kuyafanya mazuri kama Ibilis (mkuu wa mashetani) alivyo wahadaa wazazi wetu kwa kuwaambia



“Ewe Adamu, Je! Nikujulishe mti wa umilele na wa Ufalme usiokoma?(20:120),aidha aliwaambia:“Mola wenu hakukukatazeni mti huu ila msije kuwa Malaika au kuwa miongoni mwa wakaao milele (wasife)” (7:20).

Shetani hakuishia hapo, bali aliwaapia kwa kuwaambia:


“..................Kwa yakini mimi ni mmoja wa watowao shauri njema kwenu.” (7:21).

Hivyo waumini pamoja na jitihada zao za kuhuisha Uislamu na kuusimamisha katika jamii, hawana budi kuwa makini sana na adui

shetani ambaye daima huwajia watu kwa hadaa, tashwishi na ahadi za uongo. Mashetani ambao ni miongoni mwa majini na watu, huwapotosha watu na njia ya Allah(s.w) kupitia udhaifu wa matashi waliyo nayo; kwa mfano kama mtu anatamani kupata vitu vizuri kwa urahisi bila ya kuvifanyia juhudi stahiki,shetani atampambia aviendee vitu hivyo kwa njia ya kumuasi Mola wake japo anaweza pia asivipate kama si katika makadirio ya Allah(s.w). Tamaa ya kuwa Malaika au kuishi milele ndiyo iliyowaponza wazazi wetu, Adam na Hawwah. Tujue kuwa shetani hanauwezo wa kumlazimisha mtu kumuasi Mola wake kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:



“Akasema (Iblis): Mola wangu! Kwa Sababu umenihukumu kupotea, basi nitawapambia (wanaadamu upotevu) katika ardhi na nitawapoteza wote. (15:39)




Isipokuwa waja wako waliosafika kweli kweli. Akasema (Mwenyezi Mungu) Hii njia yao ya (kuja) kwangu imenyooka. Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao; isipokuwa wale wenye kukufuata (kwa khiari zao) katika hao wapotofu.” (15:40-42)

Wanaharakati wa kuhuisha Uislamu katika jamii wataepukana na hadaa za sheitwani kwa kufanya harakati kwa Ikhlas na kufuata vilivyo Qur-an na sunnah pamoja na kuomba msaada wa Allah(s.w) na kujikinga kwake na sheitwani kama Qur-an inavyotuongoza:




“Sema: Najikinga na Bwana Mlezi wa watu, Mfalme wa watu, Mola wa watu, na shari ya mwenye kutia wasiwasi, mwenye kurejea nyuma, atiaye wasiwasi nyoyoni mwa watu ambaye ni katika majini na watu.” (114:1-6).


au kuleta dua ifuatayo:




“.........Mola wangu! Najikinga kwako uniepushe na wasiwasi wa mashetani. Najikinga kwako Mola wangu, ili wasinihudhurie”(23:97-98)

Pamoja na kujikinga na sheitwani, hatunabudi kujiepusha na tabia za kishetani kama kuwa na kibri, majivuno na chuki binafsi dhidi ya watu pasina sababu ya msingi.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 541


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Kuangamizwa kwa jeshi la tembo mwaka alizaliwa Mtume Muhammad s.a. w
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w sehemu ya 4. Hapa utajifunza kuhusu historia ya kuangamiza kwa jeshi la tembo. Soma Zaidi...

Historia ya maimam Wanne wa fiqh
Soma Zaidi...

Maana ya kusimamisha uislamu katika dini
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kulingania Uislamu kwa Jamii Nzima
Baada ya miaka mitatu ya Utume, Muhammad(s. Soma Zaidi...

Historia ya Nabii Shu'aib
atika makala hii utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Shu'aib katika Quran Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SALEHE
Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 03
Soma Zaidi...

Mtume amezaliwa mwaka gani?
Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Soma Zaidi...

Imam Malik Ibn Anas
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Shu’ayb(a.s).
Kutokana na kisa cha Nabii Shu’ayb(a. Soma Zaidi...

Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)
“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”. Soma Zaidi...