image

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo

Adam(a.

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo


Adam(a.s) aliumbiwa mkewe kutokana na asili ile ile kama tunavyojifunza katika Qur-an:



Enyi watu! Mcheni Mola wenu ambaye amekuumbeni katika nafsi (asili) moja. Na akamuumba mkewe katika nafsi ile ile. Na akaeneza wanaume wengi na wanawake kutoka wawili hao...........” (4:1).

Adam(a.s) na mkewe waliwekwa katika Bustani (Pepo) na wakapewa uhuru wa kufurahia wapendavyo ndani ya bustani hiyo na kula matunda yote wapendavyo lakini

wasikurubie matunda ya mti moja tu waliobainishiwa. Iblis (shetani), alimlaghai Adam(a.s) na mkewe wakala matunda ya mti ule waliokatazwa.



(kisha Allah akasema): “Na wewe Adamu! Kaa Peponi pamoja na mkeo, na kuleni mnapopenda, lakini msiukaribie mti huu msije kuwa miongoni mwa waliodhulumu (nafsi zao).” (7:19)



Basi Shetani; (naye ni yule Iblisi), aliwatia wasiwasi ili kuwadhihirishia aibu zao walizofichiwa, na akasema: “Mola wenu hakukukatazeni mti huu ila (kwa sababu hii) msije kuwa Malaika au kuwa miongoni mwa wakao milele (wasife).(7:20)




Naye akawaapia (kuwaambia): “kwa yakini mimi ni mmoja wa watowao shauri njema kwenu.” Basi akawateka (wote wawili) kwa khadaa (yake). Na walipouonja mti ule, aibu zao ziliwadhihirikia na wakaingia kujibandika majani ya (miti ya huko) Peponi. Na Mola wao akawaita (akawaambia) “Je, sikukukatazeni mti huu na kukwambieni ya kwamba Shetani ni adui yenu aliye dhahiri?” (7:21-22)
Tofauti na Iblis ambaye baada ya kumuasi Mola wake hakujuta

hata baada ya kukumbushwa, Adam(a.s) na mkewe walijuta sana kwa kumuasi Mola wao kisha wakalalama kwake kuleta toba:



“Mola wetu! Tumedhulumu nafsi zetu; na kama hutatusamehe na kuturehemu, bila shaka tutakuwa miongoni mwa wenye khasara (kubwa kabisa)”. (7:23).

Kisa cha kulaghaiwa Adam na Hawwah na adui yao Ibilis mpaka wakamuasi Mola wao kwa kula matunda waliyokatazwa, kinatufunza kuwa kuna maadui wasiopenda kuona Allah(s.w) anatiiwa ipasavyo katika kuendea kila kipengele cha maisha ya kila siku. Na adui mkubwa kwa waumini ni shetani ambaye huingia katika nyoyo za watu na kuwahadaa kwa kuwapambia mambo maovu na kuyafanya mazuri kama Ibilis (mkuu wa mashetani) alivyo wahadaa wazazi wetu kwa kuwaambia



“Ewe Adamu, Je! Nikujulishe mti wa umilele na wa Ufalme usiokoma?(20:120),aidha aliwaambia:“Mola wenu hakukukatazeni mti huu ila msije kuwa Malaika au kuwa miongoni mwa wakaao milele (wasife)” (7:20).

Shetani hakuishia hapo, bali aliwaapia kwa kuwaambia:


“..................Kwa yakini mimi ni mmoja wa watowao shauri njema kwenu.” (7:21).

Hivyo waumini pamoja na jitihada zao za kuhuisha Uislamu na kuusimamisha katika jamii, hawana budi kuwa makini sana na adui

shetani ambaye daima huwajia watu kwa hadaa, tashwishi na ahadi za uongo. Mashetani ambao ni miongoni mwa majini na watu, huwapotosha watu na njia ya Allah(s.w) kupitia udhaifu wa matashi waliyo nayo; kwa mfano kama mtu anatamani kupata vitu vizuri kwa urahisi bila ya kuvifanyia juhudi stahiki,shetani atampambia aviendee vitu hivyo kwa njia ya kumuasi Mola wake japo anaweza pia asivipate kama si katika makadirio ya Allah(s.w). Tamaa ya kuwa Malaika au kuishi milele ndiyo iliyowaponza wazazi wetu, Adam na Hawwah. Tujue kuwa shetani hanauwezo wa kumlazimisha mtu kumuasi Mola wake kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:



“Akasema (Iblis): Mola wangu! Kwa Sababu umenihukumu kupotea, basi nitawapambia (wanaadamu upotevu) katika ardhi na nitawapoteza wote. (15:39)




Isipokuwa waja wako waliosafika kweli kweli. Akasema (Mwenyezi Mungu) Hii njia yao ya (kuja) kwangu imenyooka. Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao; isipokuwa wale wenye kukufuata (kwa khiari zao) katika hao wapotofu.” (15:40-42)

Wanaharakati wa kuhuisha Uislamu katika jamii wataepukana na hadaa za sheitwani kwa kufanya harakati kwa Ikhlas na kufuata vilivyo Qur-an na sunnah pamoja na kuomba msaada wa Allah(s.w) na kujikinga kwake na sheitwani kama Qur-an inavyotuongoza:




“Sema: Najikinga na Bwana Mlezi wa watu, Mfalme wa watu, Mola wa watu, na shari ya mwenye kutia wasiwasi, mwenye kurejea nyuma, atiaye wasiwasi nyoyoni mwa watu ambaye ni katika majini na watu.” (114:1-6).


au kuleta dua ifuatayo:




“.........Mola wangu! Najikinga kwako uniepushe na wasiwasi wa mashetani. Najikinga kwako Mola wangu, ili wasinihudhurie”(23:97-98)

Pamoja na kujikinga na sheitwani, hatunabudi kujiepusha na tabia za kishetani kama kuwa na kibri, majivuno na chuki binafsi dhidi ya watu pasina sababu ya msingi.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 611


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam
“Na wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): “Nitakuua”. Soma Zaidi...

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Soma Zaidi...

Khalifa na Utungaji Sheria, na utiifu juu ya sheria na usimamiaji wa haki
Soma Zaidi...

Mafunzo ya sura zilizochaguliwa
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

NI IPI FAMILIA YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) NA NI IPI NASABA YAKE, UKOO WAKE NA KABILA LAKE
FAMILIA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Hitimisho juu ya Historia ya maimam wanne
Soma Zaidi...

Juhudi za Waislamu Katika Kuhuisha Harakati za Kiislamu Zama za Nyerere hadi leo
i. Soma Zaidi...

Harun(a.s), Achaguliwa Kuwa Msaidizi Musa(a.s) na kumkabili (kumlingania) firauni
Nabii Musa(a. Soma Zaidi...

Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)
Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s. Soma Zaidi...

Chanzo cha vita vya Ngamia Vita Kati ya Bibi Aisha na Khalifa Ali
Soma Zaidi...

Imam Malik Ibn Anas
Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KULELEWA NA BABA YAKE MDOGO MTUME (ABU TALIB)
KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake. Soma Zaidi...