picha

Kuzaliwa kwa Mtume S.A.W

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w, sehemu ya 5. Hapa utajifunza kuhusu kuzaliwa kwa Mtume.

KUZALIWA KWA MTUME (S.A.W) NA MAISHA YAKE KABLA YA UTUME.
Mtume (s.a.w) alizaliwa siku ya juma tatu katika mweze rabil-awali (mfunguo sita) mwezi tisa (9) kwa mujibu wa wanahistoria katika mwaka wa tembo 571 B.K.

 

Baada ya kuzaliwa mama yake alituma mtu aende akatoe habari kwa mzee Abdul al-Muttalib juu ya kuzaliwa kwa mtoto. Kwa furaha kabisa alikuja mzee na akamchukuwa mtoto akambeba na kuelekea nae mbele za al-ka’aba (nymba tukufu ya Allah) kwa kutoa shukrani zake za dhati kwa Mwenyezi Mungu. Kisha akampa jina la Muhammad, jina ambalo halikuwa likijulikana na waarabu.



Kama ilivyo kawaida ya waarabu na jamii zingine wakati ule, Muhammad alinyonya kwa mama yake na kwa baadhi ya wanawake. Mtu wa kwanza kumnyonyesha Mtume baada ya mama yake ni Thuwaibah huyu alikuwa na mtumwa wa baba yake mdogo Abuu Lahab.

 

Alivyonya Mtume Kwa Thuwaibah pamoja na mtoto wake Thuwaybah aitwaye Masrouh. Pia Thuwaybah aliwahi kumvyonyesha Hamzah bin ‘Abdul-Muttalib na baadaye alimnyonyesha Abu Salamah bin ‘Abd Al-Asad Al-Makhzumi

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 2314

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)

(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid – kumjua Allah(s.

Soma Zaidi...
Historia ya bi Khadija na familia yake na chanzo cha utajiri wake.

Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 17. Historia ya Bi Khadija na familia yake.

Soma Zaidi...
Kuangamizwa kwa jeshi la tembo mwaka alizaliwa Mtume Muhammad s.a. w

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w sehemu ya 4. Hapa utajifunza kuhusu historia ya kuangamiza kwa jeshi la tembo.

Soma Zaidi...
Ukasha bin Mihsan ni Sahaba aliyechangamkia Fursa

Katika somo hili utakwnda kujifunz anamna nambavyo Sahaba Ukasha alivyochangamkia fursa katika mambo ya heri

Soma Zaidi...