image

Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi

Ukombozi wa mji wa Makka (Fat-h Makka) mwaka 8 A.

Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi

Msafara wa Tabuk Dhidi ya Warumi


Ukombozi wa mji wa Makka (Fat-h Makka) mwaka 8 A.H. uliwezesha Uislamu kuenea kwa kasi kubwa Uarabuni kote. Nchi jirani za wakristo, hasa katika Himaya ya Warumi, zilishikwa na wivu mkubwa kutokana na kuimarika kwa Uislamu hasa kwa kasi kubwa kiasi kile. Pia waliona hatari iliyopo mbele yao kutokana na kuibuka nguvu kubwa ya Uislamu. Waliona hapana budi kuandaa mashambulizi ya nguvu ili kupunguza kasi ya nguvu ya Uislamu.



Hivyo, Warumi chini ya uongozi wa Heracleus, waliandaa jeshi kubwa sana dhidi ya Dola ya Kiislamu, wakishirikiana na nchi nyinginezo za wakristo.



Kama kawaida yake, Mtume(s.a.w) alipohakikisha juu ya maandalizi ya Warumi na nchi za Kikristo dhidi yake, hakusubiri mpaka wamvamie, bali aliandaa jeshi kubwa la Waislamu na kuelekea Syria kupambana na jeshi la Warumi.



Baada ya wiki mbili (siku 14) jeshi la Waislamu lilipiga kambi. Tabuk, mji ulioko kati ya Madinah (mji mkuu wa Dola ya Kiislamu) na Damascus (mji mkuu na mkongwe wa Syria), likingojea lisikie zaidi juu ya miondoko ya jeshi la maadui. Warumi walipopata habari juu ya maandalizi ya kivita ya Mtume(s.a.w), wakikumbuka matokeo ya vita vya Muttah, waliogopa na kurudi ndani ya mipaka yao.



Kwa kuwa lengo la jeshi la Mtume(s.a.w) lilikuwa kuihami Dola ya Kiislamu na wala sio kuvamia Syria, alibakia pale Tabuk, kilometa 700 kutoka Madinah, na kuendelea na kazi ya Da’awah. Makabila mengi ya Wakristo yalijisalimisha kwa dola ya Kiislamu na kuwa tayari kulipa Jizya. Huo ukawa ndio mwisho wa ‘U-super power” wa dola ya Kirumi na Uislamu ukachukua nafasi yake na kutimia neno la Allah(s.w):



Yeye ndiye aliyemtuma, (aliyemleta) Mtume wake kwa uwongofu na dini iliyo ya haki, ili ishinde juu ya dini zote. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa Shahidi. (48:28)

MafunzoYatokanayo na Mapambano Dhidi ya Maadui wa Dola ya Kiislamu.


Kwanza, kila Uislamu unavyopiga hatua ya maendeleo ndivyo maadui wake wanavyozidi kuwa wengi na kujiimarisha. Katika kipindi cha Makkah, ambapo Waislamu walikuwa katika hali ya udhaifu, adui alikuwa mmoja tu, Makafiri wa Kiquraish. Katika kipindi cha Madinah ambapo Dola ya Kiislamu ilianzishwa na kuendelea kila uchao, maadui nao waliongezeka mpaka ikabidi Waislamu waingie vitani kupambana na kuwashinda maadui watano walioainishwa.



Pili, Waislamu watakapojitahidi kupigania Uislamu kwa kadiri ya uwezo wao kwa kutoa mali zao na nafsi zao, Allah atawawezesha kupata ushindi kwa hali yoyote iwayo.



Tatu, Siri ya mafanikio ya Waislamu ya kusimamisha na kuendeleza Dola ya Kiislamu ni kule kumtii kwao Allah(s.w) na Mtume wake katika kila waliloamrishwa na kila walilokatazwa kwa shauku kubwa ya kupata radhi za Allah(s.w) na kuepukana na ghadhabu zake.





                   



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 380


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Watu waliovunja amri ya kuheshimu siku ya Jumamosi.
Katika zama za kale Mayahudi walikatazwa kufanya kazi siku ya Jumamosi. Soma Zaidi...

Historia ya maimam Wanne wa fiqh
Soma Zaidi...

Imam Malik Ibn Anas
Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AANALELEWA NA BABU YAKE MZEE ABDUL-ALMUTALIB AKIWA NA UMRI WA MIAKA SITA (6)
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana. Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 02
Soma Zaidi...

Ghasia na chokochoko za Makhawariji na kuuliwa kwa Ally
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SULEIMAN
Soma Zaidi...

Historia ya kujengwa kwa Alkabah (Maka)
Kama tulivyoona katika maisha ya Mtume Ibrahim(a. Soma Zaidi...

Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake
Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri. Soma Zaidi...

Mapambano ya waislamu dhidi ya Makabila ya kiarabu wakati wa Mtume
Soma Zaidi...

Chanzo cha Mapato katika serekali ya Kiislamu wakati wa Makhalifa
Soma Zaidi...

Kuangamizwa kwa jeshi la tembo mwaka alizaliwa Mtume Muhammad s.a. w
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w sehemu ya 4. Hapa utajifunza kuhusu historia ya kuangamiza kwa jeshi la tembo. Soma Zaidi...