Tukimchukua Nabii Ibrahimu kama kiongozi wa kuigwa katika harakati za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii tunajifunza yafuatayo:
(i) Mwanaharakati hanabudi kujitakasa yenye binafsi na kuwa mnyenyekevu na mtii kamili kwa Allah(s.w) kabla ya kuiendea jamii.
(ii) Hatunabudi kuanza kulingania familia zetu kabla ya kuiendea jamii-Nabii Ibrahim alianza kumlingania baba yake Azara.
(iii) Tulinganie Uislamu kwa kutumia hoja madhubuti na mbinu mbali – Qur-an (16:125).
(iv) Tulinganie Uislamu kwa watu wa kada zote – kwa raia wa kawaida wa mijini na vijijini, wasomi na maofisa katika sekta mbalimbali na viongozi wa jamii katika ngazi mbalimbali kwa kupanga na kutumia fursa zinazojitokeza – Nabii Ibrahim (a.s) alihojiana na mfalme Namrudh.
(v) Tusimchelee yeyote katika kulingania Uislamu.
(vi) Tuwe tayari kukabiliana na machungu ya kutengwa na familia na jamii kwa ujumla kwa ajili ya kusimamisha Uislamu.
(vii) (a)Tuwe – tayari kutoa nafsi zetu, nafsi za wapenzi na wandani wetu kwa ajili ya Allah(s.w) – Qur-an (9:111).
(b) Tumpende Allah(s.w) na Mtume wake na kupigania dini yake kuliko tunavyopenda nafsi zetu na jamaa zetu wa karibu. Qur-an (9:23:24), (58:22).
(viii) Tuwe na vituo vya harakati vya kistratejia na tuwe na viongozi madhubuti katika vituo hivyo.
(ix) Tufanye harakati za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii kistratejia.
(x) Tuwe tayari kuhama makazi yetu tuliyoyazoea, kuhamia maeneo ya kistratejia kwa ajili ya kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii.
(xi) Tuandae vizazi vitakavyoturithi katika harakati – Nabii Ibrahim(a.s)aliomba watoto wema watakaomrithi katika harakati.
(xii) Tuzihusishe familia zetu katika harakati – Bi Hajarah aliridhia kubaki mwenyewe Makka na kitoto chake kichanga kwa ajili ya kutii amri ya Allah(s.w).
(xiiii)Tuwahusishe jamaa zetu wa karibu katika harakati – Nabii Ibrahim(a.s) alihama kutoka Iraq na mpwa wake Lut (a.s) na kumfanya kuwa kiongozi wa kituo cha harakati cha Transjordan.
(xiv) Tuwe wepesi wa kumuelekea Allah(s.w) kwa maombi mbalimbali ya kuomba msaada wa Allah(s.w) na kumshukuru kama alivyokuwa akifanya NabiiIbrahiim(a.s) Qur-an.(37:100-101) (14:39)
(xv) Tumuombe Allah(s.w) aturehemu na kutubariki kama alivyomrehemu na kumbariki Nabii Ibrahim (a.s) kwa kumswalia Mtume(s.a.w) mara kwa mara kama tukavyo mswalia katika swala.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Tumeona katika historia yake kuwa Nabii Ibrahiim(a.
Soma Zaidi...Mtume aliyemfuatia Nabii Idrisa(a.
Soma Zaidi...Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”.
Soma Zaidi...Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.
Soma Zaidi...