Navigation Menu



Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ibrahiim(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ibrahiim(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ibrahiim(a.s)

Tukimchukua Nabii Ibrahimu kama kiongozi wa kuigwa katika harakati za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii tunajifunza yafuatayo:



(i) Mwanaharakati hanabudi kujitakasa yenye binafsi na kuwa mnyenyekevu na mtii kamili kwa Allah(s.w) kabla ya kuiendea jamii.



(ii) Hatunabudi kuanza kulingania familia zetu kabla ya kuiendea jamii-Nabii Ibrahim alianza kumlingania baba yake Azara.



(iii) Tulinganie Uislamu kwa kutumia hoja madhubuti na mbinu mbali – Qur-an (16:125).



(iv) Tulinganie Uislamu kwa watu wa kada zote – kwa raia wa kawaida wa mijini na vijijini, wasomi na maofisa katika sekta mbalimbali na viongozi wa jamii katika ngazi mbalimbali kwa kupanga na kutumia fursa zinazojitokeza – Nabii Ibrahim (a.s) alihojiana na mfalme Namrudh.



(v) Tusimchelee yeyote katika kulingania Uislamu.



(vi) Tuwe tayari kukabiliana na machungu ya kutengwa na familia na jamii kwa ujumla kwa ajili ya kusimamisha Uislamu.



(vii) (a)Tuwe – tayari kutoa nafsi zetu, nafsi za wapenzi na wandani wetu kwa ajili ya Allah(s.w) – Qur-an (9:111).



(b) Tumpende Allah(s.w) na Mtume wake na kupigania dini yake kuliko tunavyopenda nafsi zetu na jamaa zetu wa karibu. Qur-an (9:23:24), (58:22).



(viii) Tuwe na vituo vya harakati vya kistratejia na tuwe na viongozi madhubuti katika vituo hivyo.



(ix) Tufanye harakati za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii kistratejia.



(x) Tuwe tayari kuhama makazi yetu tuliyoyazoea, kuhamia maeneo ya kistratejia kwa ajili ya kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii.



(xi) Tuandae vizazi vitakavyoturithi katika harakati – Nabii Ibrahim(a.s)aliomba watoto wema watakaomrithi katika harakati.



(xii) Tuzihusishe familia zetu katika harakati – Bi Hajarah aliridhia kubaki mwenyewe Makka na kitoto chake kichanga kwa ajili ya kutii amri ya Allah(s.w).



(xiiii)Tuwahusishe jamaa zetu wa karibu katika harakati – Nabii Ibrahim(a.s) alihama kutoka Iraq na mpwa wake Lut (a.s) na kumfanya kuwa kiongozi wa kituo cha harakati cha Transjordan.



(xiv) Tuwe wepesi wa kumuelekea Allah(s.w) kwa maombi mbalimbali ya kuomba msaada wa Allah(s.w) na kumshukuru kama alivyokuwa akifanya NabiiIbrahiim(a.s) Qur-an.(37:100-101) (14:39)



(xv) Tumuombe Allah(s.w) aturehemu na kutubariki kama alivyomrehemu na kumbariki Nabii Ibrahim (a.s) kwa kumswalia Mtume(s.a.w) mara kwa mara kama tukavyo mswalia katika swala.



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1166


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

HISTORIA YA KUUMBWA KWA NABII ADAMU (A.S)NA HADHI YAKE NA HADHI YA WANAADAMU DUNIANI
Adam(a. Soma Zaidi...

Adam na Hawah Kushushwa Ardhini
Soma Zaidi...

Mji wa Makkah na kabila la kiqureish
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kupotoshwa Mafundisho ya Nabii Isa(a.s)
Pamoja na Isa(a. Soma Zaidi...

Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Katika Mji wa Taif
Baada tu ya Mtume(s. Soma Zaidi...

Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)
Kwa tabia zake njema Yusufu(a. Soma Zaidi...

vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata
Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu. Soma Zaidi...

Nabii Yunus(a.s) Amuomba Allah(s.w) Msamaha
Ndani ya tumbo la samaki, Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Sulaiman(a.s)
Kutokana na histoira ya Nabii Sulaiman (a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISHAQA NA YAQUB
Soma Zaidi...