image

Neema Alizotunukiwa Nabii Daudi(a.s)

Neema Alizotunukiwa Nabii Daudi(a.s)

Neema Alizotunukiwa Nabii Daudi(a.s)



(i) Kupewa Utume na Elimu.

Nabii Daudi pamoja na kupewa utume na ufalme, alifunuliwa elimu kubwa:

"Ewe Daudi! Hakika tumekujaalia kuwa khalifa katika ardhi; basi wahukumu watu kwa haki wala usifuate matamanio ya nafsi yasije yakakupoteza na njia ya Mwenyezi Mungu" (38:26).



"Na bila shaka tuliwapa Daudi na Suleiman ilimu (kubwa kabisa) wakasema: "Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu. Aliyetufadhilisha kuliko wengi katika waja wake waliomuamini". (27:15).



(ii)Kupewa Zaburi.

Katika Qur'an vinatajwa vitabu vikuu 4 vya Allah(s.w). Vitabu hivyo ni Zaburi, Taurati, Injili na Qur'an. Zaburi alipewa Mtume Daudi (a.s).

β€œβ€¦Na Daud tukampa Zaburi" (4:163).



(iii)Kipawa cha Mawasiliano na Viumbe Wengine Zaidi ya Wanaadamu.

Ilivyo kawaida wanaadamu huwasiliana wao kwa wao hasa kwa njia ya lugha. Na wanyama na viumbe wengine nao

wana namna ya kuwasiliana wenyewe kwa wenyewe. Lakini Allah(s.w), Muweza wa yote alimjaalia Nabii Daudi kuwa na mawasiliano na viumbe wengine. Aidha alitiishiwa baadhi ya viumbe akawa anashirikiana navyo katika kumdhukuru Allah(s.w).




"Subiri juu ya hayo wanayosema, na umkumbuke mja wetu Daudi Mwenye nguvu (ya kuendesha Utume na Ufalme); kwa yakini yeye alikuwa mwelekevu sana".Hakika sisi tuliitiisha milima (iwe) pamoja naye, ikimtukuza (Mwenyezi Mungu pamoja naye) jioni na asubuhi. Na pia Ndege waliokusanywa (makundi kwa makundi), wote walikuwa wanyenyekevu kwake" (38:17-19).



(iv)Ustadi Katika Matumizi ya Chuma.

Umuhimu wa matumizi ya chuma hasa katika kuihami Dini ya Allah ni jambo kongwe katika historia ya mwanaadamu. Moja ya neema aliyopewa Nabii Daudi ni ujuzi wa kukifua chuma na
kutengeneza zana mbali mbali ikiwa ni pamoja na zana za vita.




"Na kwa hakika Tulimpa Daudi fadhila kubwa kutoka kwetu. (Tuliyaamrisha majabali yawe yanaitikia Dua pamoja naye. Tukayaambia): Enyi milima! Rejezeni sauti pamoja naye. Na (nyie) ndege (pia )". Na tukamlainishia chuma" (34:10).



"(Tukamwambia): Tengeneza (nguo za chuma) pana, na upime vizuri katika kuunganisha; na fanyeni vitendo vizuri, bila shaka Nayaona (yote) msiyoyatenda" (34:11).



"Na tukamfundisha (Daudi) matengenezo ya mavazi ya vita kwa ajili yenu ili yakuhifadhini katika mapigano yenu. Je! Mtakuwa wanaoshukuru?" (21:80).


(v)Hakimu Muadilifu

Nabii Daudi alipewa ilimu na akili ya kukata hukumu:

"Na Tukautia nguvu ufalme wake na Tukampa ilimu na (akili ya)
kukata hukumu" (38:20).



Yapo matukio mawili katika historia ya maisha ya Nabii Daudi yanayotoa kielelezo cha unyenyekevu wake katika kuifuata haki. Tukio la kwanza ni lile linalobainishwa katika Qur'an Surat Sad aya ya 21 mpaka 25. Katika aya hizi zinatajwa habari za watu wawili waliokuwa wanagombana na kumwendea Nabii Daudi ili awahukumu. Nabii Daudi aliathiriwa mno na maelezo ya upande mmoja kiasi kwamba akatoa hukumu bila ya kusikiliza upande wa pili. Lakini punde akatanabahi na kugundua kosa alilolifanya akarejea kwa Mola wake na kuomba maghfira. Tukio hili linabainishwa katika Qur'an kama ifuatavyo:



"Na je imekuwasilia habari ya wagomvi walipopindukia (ukutani kuingia) chumbani kwake (Nabii Daudi?)" (38:21).


Walipomuingilia Daudi na akawaogopa. Wakasema: "Usiogope; (sisi ni) wagombanao wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe; basi tuhukumu, kwa haki wala usipendelee, na utuongoe katika njia iliyo sawa" (38:22).


Hakika huyu ni ndugu yangu, yeye ana kondoo majike tisini na tisa, na mimi nina kondoo mmoja tu jike, lakini amesema: "Nipe huyu wako nikufugie, (na mimi mwenyewe sitaki) na amenishinda katika maneno" (38:23).



Akasema: "Kweli amekudhulmu kwa kukuomba kondoo wako kuongeza katika kondoo wake, na bila shaka washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao, isipokuwa wale walioamini na kutenda mema, na hao ni wachache". Na mara Daudi akaona ya kwamba tumemtia mtihanini. Akaomba maghufira kwa Mola wake, na akaanguka kunyenyekea na akaelekea (kwa Mola wake) (38:24).



"Basi tukamghufiria (tukamsamehe) hayo. Na kwa hakika ana yeye kwetu cheo kikubwa na mahali pazuri (marejeo mazuri)" (38:25).



Katika tukio hili kosa alilolifanya Nabii Daud ni kule kukata hukumu kabla ya kusikiliza upande wa pili. Kama inavyobainishwa na aya hizi msemaji wa awali alikuwa hodari wa kuyapanga maneno kiasi kwamba alimfanya Nabii Daud amwone ana haki kabla hata hajasikiliza upande wa pili. Lakini hata hivyo kwa ule Ucha-Mungu wake alizindukana na kuomba maghufira.



Hili ni fundisho kubwa sana kwetu kuwa katika hali yoyote itakayokuwa, mtu asipitishe hukumu kwa kutegemea maelezo ya upande mmoja tu.

Katika tukio la pili Nabii Daud(a.s) na mwanawe Sulaiman(a.s) waliletewa shauri. Mbuzi wa mtu mmoja waliingia shambani na kuharibu kabisa mimea ya mtu mwingine. Uharibifu huo ulikuwa ni mkubwa kiasi cha kumkosesha kabisa mavuno muhusika kwa mwaka mzima.



Nabii Daud(a.s) alitoa hukumu kuwa mbuzi waliohusika na uharibifu ule, apewe mwenye shamba kama fidia. Lakini mtoto wake Sulaiman aliona hukumu iliyo ya haki zaidi si kumpa mwenye shamba mbuzi wale moja kwa moja. Bali awachukue akae nao anufaike na maziwa, sufi na watoto watakaozaliwa kiasi cha kufidia hasara ya mazao yake kisha mbuzi warejeshwe kwa mwenyewe. Nabii Daud kwa vile alikuwa ni mtu wa haki mwenye kusimamia uadilifu hakusita kuchukua rai hii japo imetoka kwa mtoto wake. Tunakumbushwa katika Qur'an:



"Na (wakukbushe) Daudi na Suleiman walipokata hukumu juu ya konde, walipolisha humo mbuzi wa watu usiku. Nasi kwa hukumu yao hiyo tulikuwa mashahidi, (tunaona, tunasikia") (21:78). Tukamfahamisha Suleiman (kuliko Mzee wake, Daudi). Na kila mmoja tulimpa hukumu na ilimu" (21:79).



Ikumbukwe Daud(a.s) alikuwa ni Mtume kisha Mfalme wa Wayahudi, lakini hakuwa na takaburi za kifalme. Alikuwa laini katika kusimamia uadilifu. Alikuwa mtu rahisi mbele za watu kiasi kwamba alifanya kazi za mikono ili kujitafutia riziki yake na familia yake



(vi) Mtoto Mwema, Sulaiman (a.s)

"Na tukampa Daud (Mtoto aliyeitwa) Suleiman aliyekuwa Mtu Mwema na aliyekuwa mnyanyekevu.(38:30)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 662


Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake
Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu. Soma Zaidi...

Maana ya Kuamini Mitume wa Allah (s.w) katika maisha ya kila s iku.
Waumini wa kweli wa Mitume wa Allah (s. Soma Zaidi...

NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W)
Zifuatazo ni njia nyingi za kumjua Mwenyezi Mungu (EDK form 2:dhana ya elimu katika uislamu) Soma Zaidi...

Nafasi ya Elimu katika uislamu
Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu. Soma Zaidi...

Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa
Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki. Soma Zaidi...

Neema Alizotunukiwa Nabii Daudi(a.s)
Soma Zaidi...

Vipi Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia njia ya maandishi
Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi. Soma Zaidi...

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah
Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe). Soma Zaidi...

DUA WAKATI WA KURUKUU,KUITIDALI, KUSUJUDI NA NAMNA YA KUSOMA TAHIYATU
6. Soma Zaidi...

Dhana ya ibada kwa mtazamo wa uislamu..
Mtazamo wa uislamu juu ya ibada (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kwa namna gani nabii Musa na Bi Mariam waliweza kuzungumza na Allah nyuma ya pazia
Nabii Musa na Mama yake nabii Isa bi Mariam waliweza kuwasiliana na Allah nyuma ya pazia. Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Anfal (8:2-4) na Al-Hujurat
"Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa khofu; na wanaposomewa aya zake huwazidishia imani na wanamtegemea Mola wao tu basi. Soma Zaidi...