Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Daud(a.s)
Kutokana historia ya Nabii Daud (a.
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Daud(a.s)
Kutokana historia ya Nabii Daud (a.s) tunajifunza yafuatayo
(i) Katika kuchagua kiongozi wa kuendeleza harakati za kusimimisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuzingatia sifa nne za msingi zifuatazo:
(a) Elimu ya mwongozo na mazingira – (58:11)
(b) Ucha-Mungu-mwenye kujitahidi kufuata kwa unyenyekevu maamrisho ya Allah(s.w) na Mtume wake na kujitahidi hivyo hivyo kujiepusha na makatazo yao – Qur’an (49:13)
(c) Siha au Afya nzuri na ushupavu. Mtume(s.a.w)
amesema:
“Muumini mwenye afya nzuri (kawiyyu) ni bora zaidi kuliko muumini nyoronyoro (legelege).”
(d) Mwenye tabia njema – Pia Mtume (s..a.w) kasema;
“Aliye kipenzi changu kuliko wote katika nyinyi (Waislamu) ni yule aliyewazidi kwa tabia njema” (Al-Bukhari).
(ii) Utii kwa kiongozi muumini (mcha-mungu) ni msingi wa mafanikio kwa waislamu
(iii) Waumini wachache wenye msimamo na wenye kumtegemea Allah(s.w) wana uwezo wa kusimamisha haki (Uislamu) katika jamii.(2:249)
(iv)Tusitoe hukumu juu ya shutuma kabla hatujapata maelezo na kuyapima kutoka kwa yule anayeshutumu na anayeshutumiwa.
(v) Tushukuru neema na vipaji vya ziada alivyotutunukia Allah(s.w) na kuwa mstari wa mbele katika kusimamisha uadilifu katika jamii – Nabii Daud (a.s) alikuwa mfalme juu ya watu, milima, upepo na ndege, lakini hakutakabari.
(vi) Hatunabudi kuwaandalia maadui wa Uislamu silaha zinazolingana na wakati huu wa sayansi na teknologia – Nabii Daud(a.s)alitumia chuma kuandaa silaha na mavazi ya kivita – Pia rejea agizo la Allah(s.w) (8:60)
(vii) Hatunabudi kuwa na mazoezi ya kivita yatakayo tuwezesha kuwa jasiri na wavumilivu katika vita dhidi ya maadui wa Haki (Uislamu)
- Mfalme Twalut alilipa jeshi lake zoezi la kutokunywa maji ya mto ule ili kupima utii wao na uvumilivu wao.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 web hosting 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
HISTORIA YA MTUME DHUL-KIFL(A.S)
Mtume Dhul-kifl ananasibishwa na Ezekiel anayetajwa ndani ya Biblia.
Soma Zaidi...HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani.
Soma Zaidi...Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Hud(a.s)
(i) Tuanze kulingania kwa kuonesha upweke wa Allah(s.
Soma Zaidi...Mji wa Makkah na kabila la kiqureish
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...