Kutokana historia ya Nabii Daud (a.s) tunajifunza yafuatayo
(i) Katika kuchagua kiongozi wa kuendeleza harakati za kusimimisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuzingatia sifa nne za msingi zifuatazo:
(a) Elimu ya mwongozo na mazingira – (58:11)
(b) Ucha-Mungu-mwenye kujitahidi kufuata kwa unyenyekevu maamrisho ya Allah(s.w) na Mtume wake na kujitahidi hivyo hivyo kujiepusha na makatazo yao – Qur’an (49:13)
(c) Siha au Afya nzuri na ushupavu. Mtume(s.a.w)
amesema:
“Muumini mwenye afya nzuri (kawiyyu) ni bora zaidi kuliko muumini nyoronyoro (legelege).”
(d) Mwenye tabia njema – Pia Mtume (s..a.w) kasema;
“Aliye kipenzi changu kuliko wote katika nyinyi (Waislamu) ni yule aliyewazidi kwa tabia njema” (Al-Bukhari).
(ii) Utii kwa kiongozi muumini (mcha-mungu) ni msingi wa mafanikio kwa waislamu
(iii) Waumini wachache wenye msimamo na wenye kumtegemea Allah(s.w) wana uwezo wa kusimamisha haki (Uislamu) katika jamii.(2:249)
(iv)Tusitoe hukumu juu ya shutuma kabla hatujapata maelezo na kuyapima kutoka kwa yule anayeshutumu na anayeshutumiwa.
(v) Tushukuru neema na vipaji vya ziada alivyotutunukia Allah(s.w) na kuwa mstari wa mbele katika kusimamisha uadilifu katika jamii – Nabii Daud (a.s) alikuwa mfalme juu ya watu, milima, upepo na ndege, lakini hakutakabari.
(vi) Hatunabudi kuwaandalia maadui wa Uislamu silaha zinazolingana na wakati huu wa sayansi na teknologia – Nabii Daud(a.s)alitumia chuma kuandaa silaha na mavazi ya kivita – Pia rejea agizo la Allah(s.w) (8:60)
(vii) Hatunabudi kuwa na mazoezi ya kivita yatakayo tuwezesha kuwa jasiri na wavumilivu katika vita dhidi ya maadui wa Haki (Uislamu)
- Mfalme Twalut alilipa jeshi lake zoezi la kutokunywa maji ya mto ule ili kupima utii wao na uvumilivu wao.