Somo Hili linaeleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form2: dhana ya elimu ya uislamu)
Udhaifu wa Mtazamo wa Makafiri juu ya Dini dhidi ya Mtazamo wa Uislamu.
Katika Uislamu dini maana yake ni mfumo, utaratibu, mila kamili wa maisha unaofuatwa na wanaadamu.
Rejea Quran (3:83), (3:85), (18:20), (9:33) na (16:9).
Tofauti na Makafiri, Uislamu unatazama dini kama ifuatavyo:
Maana ya Dini.
Chimbuko, Chanzo au Asili ya Dini.
Kazi ya Dini katika jamii.
Maana ya Dini.
- Dini ni mfumo, utaratibu kamili wa maisha unaofuatwa na wanaadamu. Kinyume na mtazamo wa makafiri kuwa dini ni imani juu ya kuwepo Mungu Muumba.
- Hivyo, dini ni utaratibu wowote ule wa maisha wanaofuata watu (mtu) katika kuendesha maisha yake, sio lazima kuamini kuwepo wa Mungu Muumba.
Rejea Quran (109:1-6), (9:31), (25:43), (61:8-9) na (17:81).
Chimbuko, Asili au Chanzo cha Dini.
Dai la makafiri kuwa chimbuko la dini limetokana na fikra finyu na uduni wa maendeleo ya sayansi na teknolojia wakati wa ujima, sio sahihi kwa sababu;
Hakuna kipindi chochote cha maisha, mwanaadamu aliishi katika ujima na fikra finyu, kwani tangu mwanaadamu wa mwanzo alipewa elimu na fani juu ya kuyamudu mazingira yake.
Pia mwanaadamu kila zama aliletewa mwongozo sahihi wa maisha kupitia mafundisho ya mitume unaotoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w).
Rejea Quran (2:31) na (2:38-39).
- Hivyo katika Uislamu, chanzo na asili ya dini ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kwa ushahidi wa aya na hadith mbali mbali.
Kazi ya Dini katika jamii.
Mtazamo wa Makafiri, dini ni chombo cha unyonyaji, dhuluma na kujenga matabaka katika jamii, dai hili ni la kweli au sio la kweli kama ifuatavyo;
Ukweli wa dai hili ni sahihi kwa dini zote za wanaadamu kama Ushirikina, Utawa na Ukafiri.
Udhaifu wa dai hili, ni kuwa dini sahihi ilikuwa na kazi ya kuikomboa jamii kutokana na aina zote za ukandamizaji, utabaka, dhuluma, n.k.
- Hivyo katika Uislamu, dini ina kazi ya kuiongoza jamii katika maisha ya haki, uadilifu na usawa na kupigana na aina zote za dhuluma na ukandamizaji.
Rejea Quran (57:25), (28:4) na (7:103-105).
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.
Soma Zaidi...Uislamu unaitazama dini katika nyanja zote za maisha ya mwanadamu. Hii ni tofauti na mtazamo wa kikafiri juu ya dini.
Soma Zaidi...Nguzo za Imani (EDK form 2:. Dhana ya elimu ya uislamu
Soma Zaidi...Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.
Soma Zaidi...Hili ni swali kutoka katika maarifa ya elimu ya dini ya kiislamu kidato cha kwanza (EDK FORM 1)
Soma Zaidi...Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu Ni upi? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu)
Soma Zaidi...