Udhaifu wa mtazamo wa makafiri juu ya dini dhidi ya mtazamo wa uislamu

Somo Hili linaeleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form2: dhana ya elimu ya uislamu)

 

Udhaifu wa Mtazamo wa Makafiri juu ya Dini dhidi ya Mtazamo wa Uislamu.

Katika Uislamu dini maana yake ni mfumo, utaratibu, mila kamili wa maisha unaofuatwa na wanaadamu.

Rejea Quran (3:83), (3:85), (18:20), (9:33) na (16:9).

           

            Tofauti na Makafiri, Uislamu unatazama dini kama ifuatavyo:

Maana ya Dini.

Chimbuko, Chanzo au Asili ya Dini.

Kazi ya Dini katika jamii.

 

Maana ya Dini.

- Dini ni mfumo, utaratibu kamili wa maisha unaofuatwa na wanaadamu. Kinyume na mtazamo wa makafiri kuwa dini ni imani juu ya kuwepo Mungu Muumba.

 

- Hivyo, dini ni utaratibu wowote ule wa maisha wanaofuata watu (mtu) katika kuendesha maisha yake, sio lazima kuamini kuwepo wa Mungu Muumba.

Rejea Quran (109:1-6), (9:31), (25:43), (61:8-9) na (17:81).

 

Chimbuko, Asili au Chanzo cha Dini.

Dai la makafiri kuwa chimbuko la dini limetokana na fikra finyu na uduni wa maendeleo ya sayansi na teknolojia wakati wa ujima, sio sahihi kwa sababu;

 

Hakuna kipindi chochote cha maisha, mwanaadamu aliishi katika ujima na fikra finyu, kwani tangu mwanaadamu wa mwanzo alipewa elimu na fani juu ya kuyamudu mazingira yake.

 

Pia mwanaadamu kila zama aliletewa mwongozo sahihi wa maisha kupitia mafundisho ya mitume unaotoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w).

Rejea Quran (2:31) na (2:38-39).

 

- Hivyo katika Uislamu, chanzo na asili ya dini ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kwa ushahidi wa aya na hadith mbali mbali.

 

Kazi ya Dini katika jamii.

Mtazamo wa Makafiri, dini ni chombo cha unyonyaji, dhuluma na kujenga matabaka katika jamii, dai hili ni la kweli au sio la kweli kama ifuatavyo;

 

Ukweli wa dai hili ni sahihi kwa dini zote za wanaadamu kama Ushirikina, Utawa na Ukafiri.

 

Udhaifu wa dai hili, ni kuwa dini sahihi ilikuwa na kazi ya kuikomboa jamii kutokana na aina zote za ukandamizaji, utabaka, dhuluma, n.k. 

 

- Hivyo katika Uislamu, dini ina kazi ya kuiongoza jamii katika maisha ya haki, uadilifu na usawa na kupigana na aina zote za dhuluma na ukandamizaji.

Rejea Quran (57:25), (28:4) na (7:103-105).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2580

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰3 Dua za Mitume na Manabii    ๐Ÿ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰5 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu

Ni mgawanyo upi wa elimu haukubaliki. Ni ipi elimul akhera na elimu dunia? (Edk form 1 Dhana ya elimu)

Soma Zaidi...
ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ู‡ูุฑูŽูŠู’ุฑูŽุฉูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฃูŽู†ูŽู‘ ุฑูŽุณููˆู„ูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ู‚ูŽุงู„ูŽ: "ู…ูŽู†ู’ ูƒูŽุงู†ูŽ ูŠูุคู’ู…ูู†ู ุจูุงูŽู„ู„ูŽู‘ู‡ู ูˆูŽุงู„ู’ูŠูŽูˆู’ู…ู...

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.

Soma Zaidi...
Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?

Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.

Soma Zaidi...
Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zanaย aliyotunukiwaย mwanadamuย ili aitumieย kutekelezaย majukumuย yake kama Khalifa wa Allah (s.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamh juu ya ibada

Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada

Soma Zaidi...