image

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Furqaan (25:64-76)

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Furqaan (25:64-76)

4.Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Furqaan (25:64-76)



Katika Suratul-Furqaan sifa za Waumini zinabainishwa tena kama ifuatavyo:


"Na waja wa Rahmaan; Ni wale wanaokwenda ulimwenguni kwa unyenyekevu; na wajinga wakisema nao (maneno mabaya) huwajibu (maneno ya) salama. (25:63)


Na wale wanaopitisha baadhi ya saa za usiku kwa ajili ya Mola wao kwa kusujudu na kusimama. na wale wanaosema:


"Mola wetu! Tuondolee adhabu ya Jahannam, bila shaka adhabu yake ni yenye kuendelea. (25:64-65)


Hakika hiyo (Jahannamu) ni kituo kibaya na mahali (pabaya kabisa) pa kukaa". Na wale ambao wanapotumia hawatumii kwa fujo wala hawafanyi ubakhili, bali wanaokuwa katikati baina ya hayo. (25:66-6 7)


Na wale wasiomuomba Mungu mwingine pamoja na Allah, wala hawaiui nafsi aliyoiharamisha Allah ila kwa haki, wala hawazini; na atakayefanya hayo atapata madhara (papa hapa ulimwenguni). (25:68).


Na atazidishiwa adhabu siku ya Kiyama na atakaa humo kwa kufedheheka milele. (25:69)


Ila yule atakayetubia na kuamini na kufanya vitendo vizuri, basi hao ndio Mwenyezi Mungu atawabadilishia maovu yao kuwa mema; na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu. (25:70)


Na aliyetubia na kufanya wema, basi kwa hakika yeye anatubu kweli kweli kwa Mwenyezi Mungu. (25:71)



Na wale ambao hawashuhudii shahada za uwongo, na wanapopita penye upuuzi, hupita kwa hishima (yao). (25:72)


Na wale ambao wanapokumbushwa aya za Mola wao hawaziangukii kwa uziwi na upofu. (25:73).


Na wale wanaosema: "Mola wetu! Tupe katika wake zetu na watoto wetu yaburudishayo macho (yetu) (nyoyo zetu), na Utujaalie kuwa waongozi kwa wamchao (Mungu). (25:74)


Hao ndio watakaolipwa ghorofa (za Peponi) kwa kuwa walisubiri, na watakuta humo hishima na amani. (25:75)


Wakae humo milele; kituo kizuri na mahali pazuri (kabisa pa kukaa). (25:76)



Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa sifa za Waumini ambao hapa wameitwa "Waja wa Rahman" ni pamoja na:
(i)Kuishi na watu kwa Wema
Waumini wa kweli huishi na watu kwa wema kwa kuwathamini na kuwaheshimu; kujizuia na kuwafanyia watu kibri, kujizuia na kujikweza na kujitukuza mbele ya wengine, kujizuia na kuwadhalilisha watu na kuwavunjia heshima. Kutembea katika ardhi kwa unyenyekevu ni pamoja na kuchungua barabara mipaka ya Allah(s.w) na mtume wake(s.a.w)


(ii)Huepukana ugomvi na Mabishano
Waumini wa kweli huepuka kabisa tabia ya ugomvi na mabishano. Waumini hufahamu fika kuwa kwenye ugomvi na mabishano shetani huwepo na huchochea faraka baina ya ndugu. Namna ya kuepukana na wagomvi kwa salama inaelekezwa katika Qur-an (41:36)



(iii)Hudumu katika Kuswali Tahajjud
Kuamka usiku na kuswali swala ya "Tahajjud" (kisimamo cha usiku - Qiyamullayl) kwa ajili ya kutafuta radhi za Allah (s.w) na Rehema zake. Swala hii huswaliwa usiku wa manane hususan katika theluthi ya mwisho ya usiku inayokaribiana na Al-fajiri. Swala hii ni lazima kwa kila Muislamu mwenye azima ya kuulingania Uislamu na kuusimamisha katika jamii. Ukirejea Historia ya kushuka Qur-an, amri ya kwanza aliyopewa Mtume (s.a.w) kwa niaba ya umma wake ni Kusoma kwa ajili ya Allah (s.w) - Qur-an (96:1-5); amri ya pili ikiwa swala ya Tahajjud (Qur-an 73:1-5) ili iwe maandalizi ya kukabili shughuli nzito ya kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii. Msisitizo wa Qiyamullayl tunaupata vizuri katika aya ifuatayo:


"Je, afanyaye ibada nyakati za usiku kwa kusujudu na kusimama na kuogopa akhera na kutarajia rehema ya Mola wake (ni sawa na asiyefanya hivyo)? Sema: "Je wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?" Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu." (39:9)



(iv)Huogopa adhabu ya Allah (s.w)
Waumini wa kweli huogopa adhabu ya Allah (s.w) aliyowaandalia watu waovu huko akhera kwa kujitahidi kutenda mema na kujiepusha na maovu na kila mara kuomba:


"Nawale wanaosema:Mola wetu! Tuondolee adhabu ya Jahannam, bila shaka adhabu yake ni yenye kuendelea. Hakika hiyo (Jahannamu) ni kituo kibaya na mahali (pabaya kabisa) pa kukaa." (25:65-66)



(v)Hutumia Neema kwa Insafu
Waumini wa kweli hutumia neema walizopewa na Allah (s.w) kwa insafu. Hawafanyi ubadhirifu au israfu wa neema kama vile kutumia vibaya mali, wakati, vipaji na ujuzi. Waumini daima huzigatia kuwa Allah (s.w) hawapendi waja wanaofuja neema walizotunukiwa na Allah (s.w). Wasiotumia neema kwa insafu, ni wafuasi wa shetani.


"Na wape jamaa wa karibu haki zao, na mayatima (vile vile) na masikini, wala usifanye ubadhirifu." (1 7:26)


Hakika wafanyao ubadhirifu ni marafiki wa shetani, na shetani ni mwenye kumkufuru Mola wake. (17:27)



(vi)Hawamshirikishi Allah (s.w)
Waumini wa kweli hawamshirikishi Allah (s.w). Hujiepusha na aina zote za shirk. Shirk katika dhati, shirk katika sifa, shirk katika hukumu na shirk katika mamlaka ya Allah (s.w). Kufanya shirk ni dhambi kubwa ya daraja la kwanza. Qur-an inaonya na kutahadharisha kuwa:



Hakika Mwenyezi Mungu hasamehi (dhambi ya) kushirikishwa na kitu na husamehe yasiyokuwa haya kwa amtakaye. Na anayemshirikisha Allah bila shaka amebuni dhambi kubwa. (4:48). Pia rejea Qur-an (4:116) na (39:65)



(vii)Hulinda na kutetea haki ya Uhai wa Nafsi
Waumini wa kweli hulinda na kutetea haki ya uhai wa kila nafsi yenye haki ya kuishi. Hivyo, hujitahidi kujiepusha na ushiriki wa kusababisha au kufanya mauwaji ya nafsi ambayo kwa mujibu wa mwongozo wa Allah (s.w) hustahiki kuishi. Ulinzi wa utetezi huu wa haki ya uhai wa nafsi unatokana na mwongozo wa Allah katika Qur-an kuwa:


Mwenye kuiuwa nafsi pasina nafsi hiyo iliyouliwa kuuwa au kufanya fisadi katika ardhi, itakuwa kana kwamba ameuwa watu wote. Na atakayelinda nafsi hiyo, atakuwa kana kwamba amelinda uhai wa watu wote. (5:32)



(viii)Hawafanyi Uzinzi
Waumini wa kweli hawaikaribii zinaa wala kufanya uzinifu. Na zaidi hawashawishi wala kushiriki kwa namna yoyote ile katika mambo yanayosababisha zinaa kufanyika.


"Wala usikaribie zinaa. Hakika hiyo ni uchafu (mkubwa) na ni njia mbaya (kabisa)." (17:32)



(ix)Husema Kweli daima
Waumini wa kweli husema kweli daima. Hawatowi ushahidi wa uongo au kutetea batili. Wanapowajibika kutoa ushahidi juu ya jambo, husema ukweli hata kama ni dhidi ya nafsi zao wenyewe au watu wao wa karibu. (Rejea Qur-an 4:135, 5:8)



(x)Hawavutiwi na mambo ya Kipuuzi
Waumini wa kweli ni wale ambao hawavutiwi na mambo ya kipuuzi ambayo wafuasi wa Ibilisi huyatumia katika kuwavutia watu kwa lengo la kuwapumbaza na kuwateka akili zao. Muumini huwa hana muda wa kupoteza au fursa ya kuikabidhi akili yake kwa twaghuti aichezee. Hivyo, kwenye mambo ya kipuuzi waumini hupita haraka kwa heshima zao, na ikibidi kuweka jambo m-badala lenye maana na manufaa kwa jamii.



(xi)Humwitikia Allah (s.w) anapowaita
Waumini wa kweli humwitikia Allah (s.w) anapowaita kwa makatazo na maamrisho yake katika Qur-an. Hivyo hutii kwa unyenyekevu maagizo ya Allah (s.w) kila wanapokumbushwa kwa kusomewa au Kusoma wenyewe aya za Kitabu cha Allah (s.w) na Allah (s.w) ananadi katika Qur-an kuwa:


Na waja wangu wanapokuuliza kuhusu mimi, basi (waambie) hakika Mimi nipo karibu najibu maombi ya mwombaji pindi anaponiomba. Basi na waniitikie na waniamini Mimi ili wapate kuongoka. (2:186)


(xii)Hujenga Familia za Kiislamu
Waumini hujitahidi kujenga familia za Kiislamu kwa kumuongoza mke na kuwalea watoto na wale wote waliochini ya mamlaka yake katika mipaka ya Ucha-Mungu kwa kuwaamrisha kutenda mema na kuwakataza maovu. Pamoja na jitihada hiyo huomba msaada wa Allah (s.w) kwa kuleta dua ifuatayo:


โ€œ Mola wetu! Tupe katika wake zetu na watoto wetu yaburudishayo macho (yetu) (nyoyo zetu), na Utujaalie kuwa waongozi kwa wamchao (Mungu). (25:74)
Kwa ujumla waumini wa kweli ni wale wanaojipamba na tabia njema kama iliyoelekezwa katika Qur-an na Sunnah na hao ndio watakao stahili kuingia peponi.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 650


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰2 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰3 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Mtazamo wa uislamu juu ya dini
Kwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini. Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Muโ€™uminuun (23:1-11)
Soma Zaidi...

Maadili kati surat Al-Hujurat (49:1-13)
Enyi mlioamini! Soma Zaidi...

Sifa na majina ya siku ya mwisho siku ya kiyama
Soma Zaidi...

Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.
Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s. Soma Zaidi...

Mitume wa uongo
Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s. Soma Zaidi...

Taqwa (Hofu ya kumuogopa Allah) ni popote ulipo
ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุฐูŽุฑูู‘ ุฌูู†ู’ุฏูŽุจู ุจู’ู†ู ุฌูู†ูŽุงุฏูŽุฉูŽุŒ ูˆูŽุฃูŽุจููŠ ุนูŽุจู’ุฏู ุงู„ุฑูŽู‘ุญู’ู…ูŽู†ู ู…ูุนูŽุงุฐู ุจู’ู†ู ุฌูŽุจูŽู„ู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ูู…ูŽุงุŒ ุนูŽู†ู’ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽ... Soma Zaidi...

Vipi Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia njia ya maandishi
Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi. Soma Zaidi...

Muumini ni yule ambaye anazungumza ukweli
Ukweli ni katika sifa za waumini. Siku zote hakuna hasara katika kusema ukweli. Kinyume chake uongo ni katika madhambi makubwa sana. Soma Zaidi...

Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu Soma Zaidi...

(b)Umbile la Mwanaadamu ni la kidini
Ukizingatia maana halisi ya dini, kuwa dini ni utaratibu wa maisha, utadhihirikiwa kuwa umbile la mwanaadamu ni la kidini. Soma Zaidi...

Lengo la maisha ya mwanadamu
Soma Zaidi...