Maana ya Kuamini Mitume wa Allah (s.w) katika maisha ya kila s iku.

Waumini wa kweli wa Mitume wa Allah (s.

Maana ya Kuamini Mitume wa Allah (s.w) katika maisha ya kila s iku.

Maana ya Kuamini Mitume wa Allah (s.w) katika maisha ya kila s iku.


Waumini wa kweli wa Mitume wa Allah (s.w) ni wale wenye tabia ifuatayo:




1. Kuwatii Mitume ipasavyo kwa kufanya yale yote waliyoamrisha na kuacha yale yote waliyoyakataza kama Qur’an inavyosisitiza:“... Na anachokupeni Mtume basi pokeeni, na anachokukatazeni jiepusheni nacho...” (59:7)Sem a: “Ikiw a nyinyi mnampenda Mw enyezi Mungu, basi nifuateni;(hapo)Mw enyezi Mungu atakupendeni na atakughufirieni madhambi yenu.Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghufira, mwenye rehema.Sema: “Mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume. Na kama mkikengeuka, (Mw enyezi Mungu atakutieni adabu), kw ani Mw enyezi Mungu haw apendi Makafiri” (3 :31-32)


2.Kuwafanya Mitume vigezo vya maisha yao kibinafsi, kifamilia na kijamii kama inavyosisitizwa katika Qur-an:“Bila shaka mnao mfano mwema (wa kuiga) kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, kwa mwenye kumuogopa Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, na kumtaja Mwenyezi Mungu sana ”. (33:21)


3.Kuwapenda Mitume kuliko nafsi zao kama Qur-an inavyosistiza:“Sema “Kama baba zenu na wana wenu na ndugu zenu na wake zenu na jamaa zenu na mali m lizozichum a na biashara mnazoogopa kuharibikiw a,na majumba mnayoyapenda; (ikiwa vitu hivi) ni vipenzi zaidi kw enu kuliko Mw enyezi Mungu na Mtume wake na kupigania dini yake, basi ngojeni mpaka Mw enyezi Mungu alete am ri yake; na Mw enyezi Mungu hawaongozi watu maasi” (9:24)
Kumpenda Mwenyezi Mungu na Mtume si jambo lingine zaidi ya kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa unyenyekevu na upendo. Muumini wa kweli hatakuwa tayari kuifurahisha nafsi yake au kumfurahisha yeyote awaye kinyume na kumfurahisha Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Ni katika maana hii Mtume (s.a.w) anasema:
“Hatakuwa mmoja wenu ni Muumini wa kweli mpaka anipende zaidi kuliko chochote kile ikiwa ni pamoja na familia yake, mali yake na watu wote”.(Sahihi Muslim)
“Yeyote yule anayependa Sunnah yangu ananipenda, na yeyote yule anayenipenda atajikuta yuko ubavuni kw angu huko Peponi.” (Tirm idh)


4. Kuwafanya Mitume kuwa Mahakimu wao pale wanapohitilafiana katika jambo lolote lile kama tunavyojifunza katika Qur-an:“Naapa kwa (haki ya) Mola wako (Ewe Muhammad); wao hawawi wenye kuamini mpaka wakufanye hakimu katika yale wanayokhitalifiana, kisha wasione uzito nyoyoni mwao juu ya hukumu uliyopitisha, na wanyenyekee kabisa.” (4:65)“Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiyari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake hakika amepotea upotofu (upotevu) ulio wazi. ” (33:3 6)


5.Kuwa na yakini kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) ndiye Mtume wa mwisho kama Qur-an inavyosisitiza:“Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na mwisho wa Mitume, na Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.” (33:40)


6.Kumswalia Mtume(s.a.w) mara kwa mara katika swala na kila anapotajwa. Kumswalia Mtume(s.a.w) ni amri ya Allah(s.w) kama inavyotuelekeza ifuatavyo:Hakika Mwenyezi Mungu anamteremshia Rehema Mtume;na Malaika wake. Basi; Enyi mlioamini, msalieni Mtume na muombeeni amani.(33:56)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2928

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad

Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.

Soma Zaidi...
Nini chanzo cha elimu zote na ujuzi wote

Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
Mitume wa uongo

Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s.

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa Elimu kwa mtazamo wa kikafiri

Kwa mtazamo wa kikafiri elimu imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Elimu ya dunia na Elimu ya akhera.

Soma Zaidi...
Kwa nini Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa

Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.

Soma Zaidi...
Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamh juu ya ibada

Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada

Soma Zaidi...
Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah

Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio.

Soma Zaidi...