Nabii Isa(a.s) Alitumwa kwa Wana wa Israil

Mtume Isa(a.

Nabii Isa(a.s) Alitumwa kwa Wana wa Israil

Nabii Isa(a.s) Alitumwa kwa Wana wa Israil.


Mtume Isa(a.s.)alipewa Utume na kuamrishwa kufikisha ujumbe wa Allah(s.w) kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israil. Akibainisha juu ya jambo hili, Nabii Isa(a.s) alisema: '............Enyi wana wa Israili; Mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu, nisadikishaye yaliyokuwa kabla yangu katika Taurati na kutoa habari njema ya Mtume atakayekuja nyuma yangu ambaye jina lake litakuwa Ahmad. (61:6).



Na katika Biblia tunafahamishwa kuwa Nabii Isa(a.s)alisema kauli hiyo kwamba yeye ni Mtume kwa wana wa Israili tu. Ukweli huu unajitokeza pale Yesu alipojibu, akisema: Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israili(Mathayo 15:21-24)


Ujumbe wa Nabii Isa(a.s) kwa Wana wa Israil

(i) Mungu ni mmoja,wapekee,si watatu,na yeye si Mungu
Kwanza kabisa, Nabii Isa(a.s) aliwataka watu wamjue na kumuamini Mwenyezi Mungu mmoja aliye wa pekee, na kuwataka wakubali kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akawaambia:



Hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na ni Mola wenu. Basi mwabuduni. Hii ndiyo njia iliyonyooka (3:51)

Ujumbe huu wa Nabii Isa, unapatikana pia katika Biblia. Nabii Isa amenukuliwa katika Bibilia akifundisha Wana wa Israili kuwa yeye si Mungu, ila ni Mtume, na kwamba Mwenyezi Mungu ni mmoja, wapekee na ndiye Mungu wa kweli.

Na uzima wa milele ndiyo huu, wakujue wewe Mungu wa pekee wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (Yohana 17:3)



Maneno haya ya Nabii Isa(a.s) yanatuonesha ukweli kuwa yeye si mungu, na wale wanaong'ang'ania kumwita, Yesu ni mungu, hawayafuati mafundisho yake, bali wanafuata uzushi wa mafundisho na maagizo ya wanadamu. Hili analithibitisha Yesu katika Biblia:

Enyi wanafiki, ni vyema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema,Watu hawa wananiheshimu kwa midomo; ila mioyo yao iko mbali nami. Nao wananiabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.(Mathayo 15:7-9)



(ii) Hakuna dhambi ya asili

Yesu amefundisha kuwa kila mwanadamu huzaliwa akiwa huru pasina tone lolote la dhambi, na kwamba watoto ndio wakuu katika Ufalme wa mbinguni na Ufalme wa mbinguni ni wao.Na hakuna yeyote atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni(peponi) ila atakayejitahidi kutotenda maovu, na kujitahidi kufanya mema akawa safi kama mtoto.



Saa ile wanafunzi wake wakamwendea Yesu wakisema, Ni nani basi aliye mkuu katika Ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao, akasema, Amini, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika Ufalme wa mbinguni. Basi yeyote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika Ufalme wa mbinguni(Mathayo 18:1-4)

Na katika maandiko mengine ya Biblia, tunasoma: Yesu akasema: Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, Ufalme wa mbinguni ni wao(Mathayo19:14)

Kutokana na mafundisho haya ya Yesu, hakuna mtu yeyote muovu atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni (Peponi), kwa kuamini kwamba Yesu kafa msalabani kwa ajili ya dhambi zake.



(iii)Waumini wanatakiwa kufuata sheria za Mwenyezi Mungu kwa kuweka Ufalme wake hapa duniani

Nabii Isa(a.s) aliwafundisha watu wamuabudu Mwenyezi Mungu peke yake katika kila kipengele cha maisha yao. Na kwamba njia ya maisha yenye kuleta amani ya kweli na maisha ya furaha ni kufuata sheria za Mwenyezi Mungu na kuacha mafundisho ambayo ni maagizo ya wanadamu. Katika Qur,an tunafahamishwa kuwa aliwaambia Waisraili. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na ni Mola wenu. Basi mwabuduni. Hii ndiyo njia iliyonyooka. (3:51)



Na katika Biblia, amenukuliwa akiwataka watu wamuombe Mwenyezi Mungu awezeshe Ufalme wake ustawi duniani kama ulivyo stawi mbinguni ili dunia isitawaliwe na kuongozwa kwa sheria zistawishazo ufuska na ufisadi katika jamii. Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni; Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, hapa duniani kama mbinguni (Mathayo 6:9-10)



                   

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 185

Post zifazofanana:-

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani
(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu. Soma Zaidi...

Milki ya raslimali katika uislamu
Milki ya RasilimaliIli kujipatia maendeleo ya kiuchumi katika zama zote mwanaadamu anahitaji rasilimali za kumwezesha kufikia azma hiyo. Soma Zaidi...

Quran haikunukuliwa kutoka kwa mayahisdi na wakristo
(vi)Madai Kuwa Mtume (s. Soma Zaidi...

Twahara
FIQH 1. Soma Zaidi...

DUA 85 - 93
SWALA YA MTUME 85. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Embe
Soma Zaidi...

Fahamu vitamini A na kazi zake, vyakula vya vitamini A na athari za upungufu wake
Vitamini A ni katika vitamini fat soluble vitamin akama vile retinol, retinal, retinoic acid na beta-carotene. Soma Zaidi...

Kwa nini lengo la Hija halifikiwi?
Soma Zaidi...

DUA ZA SWALA
DUA ZA SWALA 1. Soma Zaidi...

Dawa ya kutibu maumivu ya jino
Utaijuwa Dawa ya maumivu ya jino, sababu za maumivu ya jino na njia za kujikinga na maumivu ya jino Soma Zaidi...

Vyakula na vinywaji hatari na vilivyo salama kwa mgonjwa wa kisukari
Hapa utajifunza vyakula hatari kwa mgonjwa wa kisukari, pia utajifunza vyakula salama anavyotakiwa ale mgonjwa wa kisukari, Pia ujajifunza njia za kujikinga na kisukari Soma Zaidi...

KITABU CHA MATUNDA
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...