picha

Mpango wa kumuuwa Khalifa ally na Gavana Muawiya

Mpango wa kumuuwa Khalifa ally na Gavana Muawiya

Kutekwa kwa Makka, Madina na Yemen



Katika mwaka wa 40 A.H. Amir Muawiya alimtuma Busr Ibn Abi Artat na watu elfu tatu kwenda Hijazi ambako aliiteka Madina, Makka na mji wa Sanaa, Yemen na kuwataka wamtii Muawiyah. Huko Yemen aliua watoto wadogo wawili wa Gavana wa jimbo hilo Ubaidullah ambaye alikimbilia Kufa. Vile vile aliwaua wafuasi wengi wa Ali. Jariah Ibn Qudamah akiwa na askari elfu mbili alitumwa kurudisha maeneo yaliyotekwa.


Alifanikiwa kuirejesha Sanaa mikononi mwa Khalifa kwani wakati huu Busr alikwisharudi Syria. Lakini alipofika Makka alipata taarifa ya kuuwawa kwa Ali na huu ukawa ndio mwisho wa Ali. Kuuwawa kwa Ali Baada ya vita vya Nahrwan, Khawarij waliendesha mambo yao chini chini. Inadaiwa waliendelea kuisakama Serikali.


Hawakumpenda Ali wala Muawiyah kwa sababu wao ndiyo chanzo cha kugawanyika kwa Waislamu, katika kundi la Muawiyah na kundi la Ali. Amr bin al As naye walimuona ana makosa kwa vile ndiye mshauri na afisa mipango wa Muawiya. Hivyo walipanga kuwaua wote watatu alfajiri ya mwezi 17 Ramadhan 40 A.H. wakati wa swala ya Alfajiri. Ilipangwa Ali auliwe na Abdur-Rahman Muljam. Muawiya auliwe na Bark Ibn Abdullah na Amr bin al As auliwe na Amr ibn Bark.


Wauwaji hawa walitia sumu kali katika majambia yao na wote wakafanya kazi yao kama walivyopanga Misri, Syria na Kufa. Lakini matokeo hayakuwa mia kwa mia. Ali alijeruhiwa vibaya na jeraha lilisababisha kifo chake kilichotokea jioni ya mwezi 20 Ramadhan 40 A.H. Muljam alikamatwa na kuhojiwa. Kabla hajafa Khalifa Ali aliwaita watoto wake na kuwausia kumcha Mungu. Lakini alipoulizwa kama Hassan atawazwe Ukhalifa alisema, “Nawaachia Waislamu waamue”. Khalifa Ali alitawala kwa miaka mine na miezi tisa. Alikufa akiwa na miaka 63.



Baada ya Khalifa Ali kuuliwa, mtoto wake, Hassan, alichaguliwa kuchukua nafasi ya Ukhalifa lakini Muawiyah aliasi na kuandaa jeshi dhidi yake. Baada ya mapigano kidogo, Hassan alizidiwa nguvu na akaona amwachie Muawiyah Ukhaifa kwa makubaliano kuwa baada yake uongozi uchukuliwe na ndugu yake, Hussein bin Ali. Kinyume na makubaliano hayo, ambayo pia hayakuwa ya Kiislamu, Muawiyah kabla hajafa, alimteua mtoto wake, Yazid bin Muawiyah kushika uongozi wa Dola baada yake.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1035

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 web hosting    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Jinsi tukio la Karatasi lilivyotokea wakati wa Mtume siku chache kabla ya kifo chake

Tukio la kartasiTukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s.

Soma Zaidi...
NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU

Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua.

Soma Zaidi...
tarekh11

KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.

Soma Zaidi...
tarekh 07

KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO.

Soma Zaidi...
Makubaliano ya Mkataba wa Al Fudhul

Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 13. Hapa utajifunza historia ya Mkataba wa al fudhul na makubaliano yake.

Soma Zaidi...
MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AANALELEWA NA BABU YAKE MZEE ABDUL-ALMUTALIB AKIWA NA UMRI WA MIAKA SITA (6)

KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.

Soma Zaidi...