Kutekwa kwa Makka, Madina na Yemen
Katika mwaka wa 40 A.H. Amir Muawiya alimtuma Busr Ibn Abi Artat na watu elfu tatu kwenda Hijazi ambako aliiteka Madina, Makka na mji wa Sanaa, Yemen na kuwataka wamtii Muawiyah. Huko Yemen aliua watoto wadogo wawili wa Gavana wa jimbo hilo Ubaidullah ambaye alikimbilia Kufa. Vile vile aliwaua wafuasi wengi wa Ali. Jariah Ibn Qudamah akiwa na askari elfu mbili alitumwa kurudisha maeneo yaliyotekwa.
Alifanikiwa kuirejesha Sanaa mikononi mwa Khalifa kwani wakati huu Busr alikwisharudi Syria. Lakini alipofika Makka alipata taarifa ya kuuwawa kwa Ali na huu ukawa ndio mwisho wa Ali. Kuuwawa kwa Ali Baada ya vita vya Nahrwan, Khawarij waliendesha mambo yao chini chini. Inadaiwa waliendelea kuisakama Serikali.
Hawakumpenda Ali wala Muawiyah kwa sababu wao ndiyo chanzo cha kugawanyika kwa Waislamu, katika kundi la Muawiyah na kundi la Ali. Amr bin al As naye walimuona ana makosa kwa vile ndiye mshauri na afisa mipango wa Muawiya. Hivyo walipanga kuwaua wote watatu alfajiri ya mwezi 17 Ramadhan 40 A.H. wakati wa swala ya Alfajiri. Ilipangwa Ali auliwe na Abdur-Rahman Muljam. Muawiya auliwe na Bark Ibn Abdullah na Amr bin al As auliwe na Amr ibn Bark.
Wauwaji hawa walitia sumu kali katika majambia yao na wote wakafanya kazi yao kama walivyopanga Misri, Syria na Kufa. Lakini matokeo hayakuwa mia kwa mia. Ali alijeruhiwa vibaya na jeraha lilisababisha kifo chake kilichotokea jioni ya mwezi 20 Ramadhan 40 A.H. Muljam alikamatwa na kuhojiwa. Kabla hajafa Khalifa Ali aliwaita watoto wake na kuwausia kumcha Mungu. Lakini alipoulizwa kama Hassan atawazwe Ukhalifa alisema, “Nawaachia Waislamu waamue”. Khalifa Ali alitawala kwa miaka mine na miezi tisa. Alikufa akiwa na miaka 63.
Baada ya Khalifa Ali kuuliwa, mtoto wake, Hassan, alichaguliwa kuchukua nafasi ya Ukhalifa lakini Muawiyah aliasi na kuandaa jeshi dhidi yake. Baada ya mapigano kidogo, Hassan alizidiwa nguvu na akaona amwachie Muawiyah Ukhaifa kwa makubaliano kuwa baada yake uongozi uchukuliwe na ndugu yake, Hussein bin Ali. Kinyume na makubaliano hayo, ambayo pia hayakuwa ya Kiislamu, Muawiyah kabla hajafa, alimteua mtoto wake, Yazid bin Muawiyah kushika uongozi wa Dola baada yake.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 389
Sponsored links
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Kitabu cha Afya
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Kitau cha Fiqh
👉5
Simulizi za Hadithi Audio
👉6
Madrasa kiganjani
MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AANALELEWA NA BABU YAKE MZEE ABDUL-ALMUTALIB AKIWA NA UMRI WA MIAKA SITA (6)
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana. Soma Zaidi...
Maadui wa uislamu na mbinu zao: wanafiki, makafiri, mayahudi, wakristo,
Upinzani dhidi ya Dola ya Kiislamu Madinah. Soma Zaidi...
Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah
Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s. Soma Zaidi...
Uchaguzi wa Abubakari kuwa Khalifa wa kwanza baada ya kufariki Mtume Muhammad (s.a.w)
Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)
Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil. Soma Zaidi...
Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani
2. Soma Zaidi...
HISTORIA NA VISA VYA MITUME, MANABII NA WATU WEMA WALIOTAJWA KWENYE QURAN
Soma Zaidi...
Hijra ya Mtume(s.a.w) Kwenda Madinah
Njama za Kumuua Mtume(s. Soma Zaidi...
historia na maisha ya Mtume IS-HAQ(A.S.) NA YA‘AQUUB(A.S.)
Is-haq(a. Soma Zaidi...
HISTORIA YA NABII MUSA(A.S) NA HARUN(A.S)
Nabii Musa(a. Soma Zaidi...