Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)

Mwenyezi Mungu pekee ndiye aliyewawezesha Mitume na Manabii kufanya miujiza.

Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)

Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)


Mwenyezi Mungu pekee ndiye aliyewawezesha Mitume na Manabii kufanya miujiza. Allah(s.w) aliwapa mitume miujiza ili kuwa dalili ya kuwathibitishia watu kuwa yeye ndiye aliyewatuma. Hakuna Mtume au Nabii aliyedai kufanya miujiza kwa uwezo wake mwenyewe. Na hivi ndivyo Nabii Isa alivyowaambia wana wa Israili.



.........Nimekujieni na hoja kutoka kwa Mola wenu, ya kwamba nakuumbieni, katika udongo, kama sura ya ndege, kisha nampuliza, mara anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na ninawaponesha vipofu na wenye mabalanga, na ninawafufua waliokufa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na nitakuambieni mtakavyo vila na mtakavyo weka akiba katika nyumba zenu. Bila shaka katika haya imo hoja (ya kuonesha kuwepo Mwenyezi Mungu) kwenu ikiwa ni watu wa kuamini(3:49)

Ni dhahiri kuwa miujiza yote aliyoifanya Nabii Isa(a.s), aliifanya kwa lengo la kuwathibitishia watu kuwa yeye ametumwa na Mwenyezi Mungu. Katika Biblia, Yesu alibainisha hili wazi kabla hajafanya muujiza wa kumfufua Lazaro:



Yesu akainua macho yake juu, akasema: Baba nakushukuru kwa kuwa umenisikia. Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia siku zote; lakini ni kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kuwa ndiwe uliyenituma. Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake umefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake (Yohana 11:41-44)

Kwa kuzingatia maandiko haya, utabaini kuwa hawasemi kweli wale wanaodai kuwa Yesu ni Mungu eti kwasababu alifanya miujiza ya kufufua wafu.



Wito wa Nabii Isa(a.s) kwa Wanafunzi Wake


Nabii Isa(a.s) alipoona ukaidi wao umeshitadi, akatoa wito maalum kwa wanafunzi wake ili wajitokeze wale watakaokuwa tayari kuwa naye bega kwa bega kupambana na madhalimu na kuufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu kwa wengine. Hivyo, akawauliza:



Lakini Isa alipoona ukaidi wao, alisema: Nani watakuwa wasaidizi wangu katika kumtangaza Mwenyezi Mungu (mmoja)? Wanafunzi wakasema: 'Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu. Tumemwamini Mwenyezi Mungu na ushuhudie kwamba sisi tumejisalimisha. Mola wetu! Tumeyaamini uliyoyateremsha na tumemfuata Mtume, basi tuandike pamoja na washuhudiao (3:52-53)



Baada ya hapo, wanafunzi wa Nabii Isa (a.s) wakamtaka awaombee chakula maalumu kutoka kwa Allah(s.w), wakasema:

Ewe Isa Mwana wa Maryam! Je Mola wako anaweza kututeremshia chakula kutoka mbinguni? Akasema(Nabii Isa), 'Mcheni Mwenyezi Mungu kama kweli ninyi ni wenye kuamini kweli(5:112) Wakasema: 'Tunataka kula katika hicho, na ili nyoyo zetu zitulie na tuwe miongoni mwa wanaoshuhudia(muujiza huo)(5:113) Akasema Isa bin Maryamu: 'Ewe Mwenyezi Mungu, Mola wetu! Tuteremshie chakula kutoka mbinguni ili kiwe Sikukuu kwa ajili ya wa mwanzo wetu, na wa mwisho wetu, na kiwe Ishara itokayo kwako, basi turuzuku, kwani wewe ndiye mmbora wa wanaoruzuku(5:114)



Mwenyezi Mungu akasema: 'Bila shaka Mimi nitakiteremsha juu yenu, lakini miongoni mwenu atakayekataa baada ya haya, basi Mimi nitamuadhibu adhabu ambayo sijamwadhibu yoyote katika walimwengu(5:115)



                   

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 531

Post zifazofanana:-

KUAMINI MALAIKA
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...

Namna ya kulipa swaumu ya ramadhani na ni nani anatakiwa alipe
Soma Zaidi...

Haki za kiuchumi za mwanamke katika uislamu
Haki za UchumiKuwa imara kiuchumi ni sababu mojawapo kubwa ya kumpa mtu hadhi katika jamii. Soma Zaidi...

Zoezi - 4
Soma Zaidi...

Mbinu za Da'wah Alizotumia Nuhu(a.s)
Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a. Soma Zaidi...

Maandalizi ya Kimafunzo aliyoandaliwa Mtume Muhammad
(i) Suratul- 'Alaq (96:1-5)'Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba Aliyemuumba mwanaadamu kwa 'alaq. Soma Zaidi...

FORM ONE BIOLOGY
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

DARASA LA AFYA NA AFYA YA UZAZI
Jifunze mengi kuhusu Afya, kuwa nasi kwenye makala hii hadi mwisho. Soma Zaidi...

Kuanzishwa kwa Polisi na magereza kati uislamu wakati wa Makhalifa
Kuanzishwa kwa Polisi. Soma Zaidi...

Home
Soma Zaidi...

NI ZIPI NGUZO NA SHARTI KUU ZA SWALA ILI IKUBALIWE
Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali. Soma Zaidi...

Hadithi Ya 32: Kusiwe Na Kudhuriana Wala Kulipiza Dhara
' ' ' "' ' ' '" ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' '?... Soma Zaidi...