image

Njama za Mayahudi Kutaka Kumuua Nabii Isa(a.s)

Njama za kutaka kumuua Nabii Isa(a.

Njama za Mayahudi Kutaka Kumuua Nabii Isa(a.s)

Njama za Mayahudi Kutaka Kumuua Nabii Isa(a.s)


Njama za kutaka kumuua Nabii Isa(a.s) zilianza kwa kumuuliza maswali ya kumtega na kumfitinisha kwa Serikali ili imuone kuwa anachochea watu wasilipe kodi na kuhatarisha maslahi ya wakubwa Serikalini. Fitina hizi zilifanywa na Mafarisayo na Makuhani, wakamwendea Yesu wakisema:



Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yeyote, kwa maana hutazami sura za watu. basi utuambie waonaje? Ni halali kumpa kaisari kodi, ama sivyo? (Mathayo 22:16-17)



Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema:

Mbona mnanijaribu enyi wanafiki? Nionyesheni fedha ya kodi. Nao wakamletea dinari. Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii, na anwani hii? Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu (Mathayo 22:18-21)



Baada ya hila hizi kushindwa, zikapangwa njama za kutaka kumuua.

Basi wakuu wa Makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu anafanya ishara nyingi.Tunamwachia hivi, watu wamwamini. Yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie Taifa zima(Mathayo11:47-48,50)


Ahadi ya Allah(s.w) Kumuokoa Nabii Isa(a.s)


Nabii Isa(a.s) alimuomba Allah(s.w) amlinde na shari za watu wabaya waliopanga njama dhidi yake. Yesu alikwenda bustani ya Gestmane kuomba. Alipofika, akawaambia wanafunzi wake:



Roho yangu ina huzuni kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami. Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifudifudi akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.(Mathayo 26:38 39)

Mwenyezi Mungu alikubali dua ya Nabii Isa (a.s) kwa kumuhakikishia kuwa atamlinda dhidi ya njama za watu madhalimu.




“Mwenyezi Mungu aliposema: “Ewe Isa! Mimi nitakukamilishia muda wako wa kuishi na nitakuleta kwangu, na nitakutakasa na wale waliokufuru, na nitawaweka wale waliokufuata, juu ya wale waliokufuru mpaka siku ya kiama. Kisha marejeo yenu yatakuwa kwangu,Nitakuhukumuni katika yale mliyokuwa mkihitilafiana”(3:55)

Katika mahubiri yake huko nyuma, Nabii Isa (a.s) aliwasisitiza sana watu kumtegemea Mwenyezi Mungu kwa kumuomba msaada. Aliwaambia:



Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona, naye abishaye hufunguliwa. Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe? Au akiomba samaki, atampa nyoka? Basi ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, Je! si zaidi Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao? (Mathayo 7:7-11)



Kwa mujibu wa Yesu mwenyewe, Mwenyezi Mungu humsikiliza maombi yake na kumkubalia daima. Hebu na tuyarejee maneno yake aliyoyasema pale alipoomba jambo kubwa la kumfufua Lazaro:



Yesu akainua macho yake juu, akasema: Baba nakushukuru kwa kuwa umenisikia. Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia siku zote; lakini ni kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kuwa ndiwe uliyenituma. Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake umefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.
(Yohana 11:41-44)



Ndiyo kusema kuwa ikiwa Yesu ametangaza kuwa,”Ombeni, nanyi mtapewa”, Na kwakuwa Mungu, huwapa “mema wao wamwombao”, na Yesu mwenyewe anakiri kuwa Mungu anamsikia siku zote, haiwezekani kabisa asulubiwe hali ya kuwa Mungu yupo na alishamuomba!



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 410


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 03
Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na vita vya uhudi
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII IBRAHIM
Soma Zaidi...

Wapinzani wa Ujumbe wa Hud(a.s)
Waliomuamini Mtume Hud(a. Soma Zaidi...

HISTORIA NA SIRA YA UISLAMU NA MTUME MUHAMMAD KUTOKA KUZALIWA MPAKA KUFARIKI NA HARAKATI ZAKE
Soma Zaidi...

KUCHIMBWA UPYA KWA KISIMA CHA ZAMZAMA NA KUNYWA MAJI YA ZAMZAMA KISIMA KILICHO BARIKIWA
KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba. Soma Zaidi...

Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni
“Na (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza. Soma Zaidi...

Bara arabu enzi za jahiliyyah, jiografia ya bara arabu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Fat-h Makkah (Kukombolewa Makkah) baada ya mkataba wa hudaibiya
Fat-h Makkah (Kukombolewa Makkah). Soma Zaidi...

Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri
Pamoja na kudhihirikiwa na ukweli wa udhaifu wa miungu wa kisanamu, watu wa NabiiIbrahiim(a. Soma Zaidi...

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana
Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a. Soma Zaidi...

Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...