Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu.

Download Post hii hapa

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu. Kila palipo na fursa nzuri ni muhimu kuibadili misikiti iliyopo na kuifanya vituo vya harakati. Lakini ichukuliwe tahadhari kubwa ili tusije tumbukia kwenye kosa la kuvamia misikiti ya watu kabla ya kufikia kipindi cha kuikomboa – Fat-h-Makka.



Pili, hatunabudi kujenga mshikamano wa Waislamu kwa njia ya kupendana na kuhurumiana na hasa kwenye matatizo na shida. Rejea udugu baina ya Answar na Muhajiriina. Hatunabudi kujenga mazingira na tabia ya kufanya kazi za bega kwa bega (za kitamasha) katika kuendeleza shughuli mbali mbali kwa ajili ya maendeleo ya Uislamu.



Tatu, hatunabudi kukaa vizuri na wasiokuwa Waislamu hasa wale wasiotupiga vita bayana.Tuwaheshimu, tuwatendee haki na tusiwatukanie miungu yao wala kuidhihaki dini yao. Tuwalinganie kwa hekima na tuwape changamoto ya hoja na mawaidha mazuri.




Waite (waite watu) katika njia ya Mola wako kwa hikima na mauidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora (siyo kwa kuwatukana wao au kutukana Dini yao. Kwa njia hii huwezi kumvuta mtu). Hakika Mola wako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake, naye ndiye anayewajua walioongoka. (16:125)



Nne, hatunabudi kuwajua vema maadui wa Uislamu na Waislamu na kuzijua vyema hila na mbinu zao katika kuuhujumu Uislamu. Kila Muislamu anatakiwa awe msalama kwa kumjua ni nani adui wa Uislamu, yuko wapi na anafanya nini dhidi ya Uislamu.



Tano, kila Muislamu mwanamume hanabudi kuwa mkakamavu na jasiri aliyetayari kuingia vitani ili kuihami Dini ya Allah(s.w).

Basi waandalieni (wawekeeni tayari) nguvu mziwezazo (silaha), na mafarasi yaliyofungwa tayari (mipakani), ili kwazo (nguvu hizi) muogopeshe maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu, (mnaowajua) na pia (maadui zenu) wengine wasiokuwa wao, msiowajua nyinyi (lakini) Mwenyezi Mungu anawajua. Na chochote mtakachokitoa katika njia ya Mwenyezi Mungu (kama hii misaada ya vita vya Jihadi) mtarudishiwa kamili wala hamtadhulumiwa. (8:60)



Sita, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii yetu, hatuna budi kuimarisha uchumi wetu.Uchumi ndio raslimali kuu ya kusimamishia Uislamu katika jamii. Kila kitu cha kimaendeleo kinahitaji matumizi ya mali. Hatunabudi kuhuisha na kuimarisha ukusanyaji na ugawaji wa Zakat na Sadaqat kijamii.



                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1054

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah
Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Vita vya Al Fijar na sababu zake
Vita vya Al Fijar na sababu zake

Historia na shida ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 12. Hapa utajifunza kuhusu kutokea kwa vita vya al fijar.

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya mtume ki-wahay
Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya mtume ki-wahay

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Historia ya Luqman mtu aliyesifika kuwa na Hikma
Historia ya Luqman mtu aliyesifika kuwa na Hikma

Luqman ni katika watu wema kabisa waliopita zama za nyuma.

Soma Zaidi...
tarekh 3
tarekh 3

KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba.

Soma Zaidi...