image

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu.

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu. Kila palipo na fursa nzuri ni muhimu kuibadili misikiti iliyopo na kuifanya vituo vya harakati. Lakini ichukuliwe tahadhari kubwa ili tusije tumbukia kwenye kosa la kuvamia misikiti ya watu kabla ya kufikia kipindi cha kuikomboa – Fat-h-Makka.



Pili, hatunabudi kujenga mshikamano wa Waislamu kwa njia ya kupendana na kuhurumiana na hasa kwenye matatizo na shida. Rejea udugu baina ya Answar na Muhajiriina. Hatunabudi kujenga mazingira na tabia ya kufanya kazi za bega kwa bega (za kitamasha) katika kuendeleza shughuli mbali mbali kwa ajili ya maendeleo ya Uislamu.



Tatu, hatunabudi kukaa vizuri na wasiokuwa Waislamu hasa wale wasiotupiga vita bayana.Tuwaheshimu, tuwatendee haki na tusiwatukanie miungu yao wala kuidhihaki dini yao. Tuwalinganie kwa hekima na tuwape changamoto ya hoja na mawaidha mazuri.




Waite (waite watu) katika njia ya Mola wako kwa hikima na mauidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora (siyo kwa kuwatukana wao au kutukana Dini yao. Kwa njia hii huwezi kumvuta mtu). Hakika Mola wako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake, naye ndiye anayewajua walioongoka. (16:125)



Nne, hatunabudi kuwajua vema maadui wa Uislamu na Waislamu na kuzijua vyema hila na mbinu zao katika kuuhujumu Uislamu. Kila Muislamu anatakiwa awe msalama kwa kumjua ni nani adui wa Uislamu, yuko wapi na anafanya nini dhidi ya Uislamu.



Tano, kila Muislamu mwanamume hanabudi kuwa mkakamavu na jasiri aliyetayari kuingia vitani ili kuihami Dini ya Allah(s.w).

Basi waandalieni (wawekeeni tayari) nguvu mziwezazo (silaha), na mafarasi yaliyofungwa tayari (mipakani), ili kwazo (nguvu hizi) muogopeshe maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu, (mnaowajua) na pia (maadui zenu) wengine wasiokuwa wao, msiowajua nyinyi (lakini) Mwenyezi Mungu anawajua. Na chochote mtakachokitoa katika njia ya Mwenyezi Mungu (kama hii misaada ya vita vya Jihadi) mtarudishiwa kamili wala hamtadhulumiwa. (8:60)



Sita, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii yetu, hatuna budi kuimarisha uchumi wetu.Uchumi ndio raslimali kuu ya kusimamishia Uislamu katika jamii. Kila kitu cha kimaendeleo kinahitaji matumizi ya mali. Hatunabudi kuhuisha na kuimarisha ukusanyaji na ugawaji wa Zakat na Sadaqat kijamii.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 301


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Daud(a.s)
Kutokana historia ya Nabii Daud (a. Soma Zaidi...

Sababu za makafiri wa kiqureish kuupinga ujumbe wa uislamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME SULAIMAN(A.S)
Sulaiman(a. Soma Zaidi...

CHANZO CHA VITA VYA VITA VYA AL-FIJAR NA ATHARI ZAKE
MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU). Soma Zaidi...

Mtume alipoanza kulingania uislamu na changamoto alizokumbana nazo kutoka kwa maadua wa uislamu
7. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Zakaria(a.s) na Yahya(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Zakaria (a. Soma Zaidi...

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu
Musa(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII YUNUS
Soma Zaidi...

Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani
2. Soma Zaidi...

Upinzani Dhidi ya Dola ya Kiislamu Wakati wa Makhalifa
Soma Zaidi...

Hatua na Mambo (Taasisi za Kisiasa) za msingi alizotumia Mtume (s.a.w) katika kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah
Kuanzishwa kwa Dola ya Kiislamu Madinah. Soma Zaidi...