Menu



Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar

Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar

Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar



Zipo tofauti za kimawazo kuhusiana na uchaguzi wa Khalifa wa kwanza, Abubakar(r.a.) mara baada ya kutawafu Mtume (s.a.w.).


Wapo wasemao uchaguzi ule ulifanyika katika mazingira ya kuchanganyikiwa, kwani mkutano haukuwa rasmi. Maelezo ya kundi hili yameegemea kauli zisemazo kuwa Abubakar(r.a.) na Umar(r.a.) walistushwa na taarifa kuwa Ansar walikuwa wamekutana kwenye ukumbi wa mikutano wa Thaqifa Bani Saidah, kumchagua kiongozi anayetokana na wao ambaye


angeshika uongozi wa dola ya Kiislamu baada ya Mtume(s.a.w.). Kwa mujibu wa kauli hizo, Abubakar(r.a.) na Umar(r.a.) walilazimika kwenda kwenye mkutano huo wakiwa na dhamira ya kuzuia usiendelee, hasa ikizingatiwa kuwa Mtume alikuwa bado hajazikwa na hilo ni suala zito lilohitajia muafaka wa Waislamu wote.


Kundi jingine lina mawazo kuwa, pamoja na kuwa mkutano wa Ansar haukuwa rasmi, lakini kuchaguliwa Abubakar(r.a.) kuliwafiki, kwa kuzingatia dokezo za Mtume(s.a.w), ishara zitokanazo na Qur’an na aliyokuja kuyafanya Abubakar(r.a.) wakati wa uongozi wake, ambayo yalidhihirisha usahihi wa chaguo la mkutano wa Thaqifa Bani Saidah.


Wapo wanaosema kuwa kutokuwepo kwa watu wa nyumba ya Mtume (Ahlul-Bayt) katika mkutano ule, kunabatilisha zoezi zima la uchaguzi wa Khalifa wa kwanza. Maelezo ya kundi hili yanatiwa tashdid na usia, unaodaiwa kuachwa na Mtume(s.a.w.) kwa “Ahlul- Bayt” muda mfupi kabla ya kutawafu kwake; unaosema kwamba haki ya uongozi wa ummah huu baada yake ni ya “Ahlul-Bayt”. Kwa hivyo Ali(r.a.) ndiye aliyestahiki nafasi hiyo, na warithi baada yake ni wanawe Hassan na Hussein kwa kuwa ni wajukuu wa Mtume(s.a.w.). Kundi hili linadai Ukhalifa wa Abubakar(r.a.), Umar(r.a.) na Uthman(r.a.) ni batili kwa kuwa hao si katika watu wa nyumba ya Mtume(s.a.w.) na walipewa uongozi katika mikutano isiyo rasmi. Aidha hatua ya kuwafanya Makhalifa ni kudhulumu haki ya Ali(r.a.) akiwa ndugu wa Mtume.


Na kuna wasemao kwamba, kwa kuwa Uislamu ni dini ya Mwenyezi Mungu si ya ukoo, kabila au Taifa fulani, na kwa kuwa hakuna aya katika Qur’an inayomwamrisha Mtume(s.a.w.) kurithisha dhima ya uongozi baada yake kwa watu wa nyumbani kwake (Ahlul-Bayt), basi jukumu la uongozi wa ummah limeachwa mikononi mwa waumini wenyewe. Kiongozi atachaguliwa kwa kuzingatia sifa mbali mbali zikiwemo uoni, ucha Mungu, siha n.k.


Sifa zote hizo zimpelekee kuongoza kwa haki na uadilifu. Kwa hiyo
Ukhalifa wa Abubakar, Umar na Uthman si suala la kubishaniwa.





                   


Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 771


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

HISTORIA YA NABII SHUAIB
Soma Zaidi...

Vita vya Uhud na sababu ya kutokea kwake, Mafunzo ya Vita Vya Uhud
Vita vya Uhudi. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo ya sura zilizochaguliwa
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Jinsi tukio la Karatasi lilivyotokea wakati wa Mtume siku chache kabla ya kifo chake
Tukio la kartasiTukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s. Soma Zaidi...

Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋 Soma Zaidi...

Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)
Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a. Soma Zaidi...

Tamko la suluhu baada ya vita vya Siffin
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Shu’ayb(a.s).
Kutokana na kisa cha Nabii Shu’ayb(a. Soma Zaidi...

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah
Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s. Soma Zaidi...