image

Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar

Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar

Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar



Zipo tofauti za kimawazo kuhusiana na uchaguzi wa Khalifa wa kwanza, Abubakar(r.a.) mara baada ya kutawafu Mtume (s.a.w.).


Wapo wasemao uchaguzi ule ulifanyika katika mazingira ya kuchanganyikiwa, kwani mkutano haukuwa rasmi. Maelezo ya kundi hili yameegemea kauli zisemazo kuwa Abubakar(r.a.) na Umar(r.a.) walistushwa na taarifa kuwa Ansar walikuwa wamekutana kwenye ukumbi wa mikutano wa Thaqifa Bani Saidah, kumchagua kiongozi anayetokana na wao ambaye


angeshika uongozi wa dola ya Kiislamu baada ya Mtume(s.a.w.). Kwa mujibu wa kauli hizo, Abubakar(r.a.) na Umar(r.a.) walilazimika kwenda kwenye mkutano huo wakiwa na dhamira ya kuzuia usiendelee, hasa ikizingatiwa kuwa Mtume alikuwa bado hajazikwa na hilo ni suala zito lilohitajia muafaka wa Waislamu wote.


Kundi jingine lina mawazo kuwa, pamoja na kuwa mkutano wa Ansar haukuwa rasmi, lakini kuchaguliwa Abubakar(r.a.) kuliwafiki, kwa kuzingatia dokezo za Mtume(s.a.w), ishara zitokanazo na Qur’an na aliyokuja kuyafanya Abubakar(r.a.) wakati wa uongozi wake, ambayo yalidhihirisha usahihi wa chaguo la mkutano wa Thaqifa Bani Saidah.


Wapo wanaosema kuwa kutokuwepo kwa watu wa nyumba ya Mtume (Ahlul-Bayt) katika mkutano ule, kunabatilisha zoezi zima la uchaguzi wa Khalifa wa kwanza. Maelezo ya kundi hili yanatiwa tashdid na usia, unaodaiwa kuachwa na Mtume(s.a.w.) kwa “Ahlul- Bayt” muda mfupi kabla ya kutawafu kwake; unaosema kwamba haki ya uongozi wa ummah huu baada yake ni ya “Ahlul-Bayt”. Kwa hivyo Ali(r.a.) ndiye aliyestahiki nafasi hiyo, na warithi baada yake ni wanawe Hassan na Hussein kwa kuwa ni wajukuu wa Mtume(s.a.w.). Kundi hili linadai Ukhalifa wa Abubakar(r.a.), Umar(r.a.) na Uthman(r.a.) ni batili kwa kuwa hao si katika watu wa nyumba ya Mtume(s.a.w.) na walipewa uongozi katika mikutano isiyo rasmi. Aidha hatua ya kuwafanya Makhalifa ni kudhulumu haki ya Ali(r.a.) akiwa ndugu wa Mtume.


Na kuna wasemao kwamba, kwa kuwa Uislamu ni dini ya Mwenyezi Mungu si ya ukoo, kabila au Taifa fulani, na kwa kuwa hakuna aya katika Qur’an inayomwamrisha Mtume(s.a.w.) kurithisha dhima ya uongozi baada yake kwa watu wa nyumbani kwake (Ahlul-Bayt), basi jukumu la uongozi wa ummah limeachwa mikononi mwa waumini wenyewe. Kiongozi atachaguliwa kwa kuzingatia sifa mbali mbali zikiwemo uoni, ucha Mungu, siha n.k.


Sifa zote hizo zimpelekee kuongoza kwa haki na uadilifu. Kwa hiyo
Ukhalifa wa Abubakar, Umar na Uthman si suala la kubishaniwa.





                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 384


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Mafunzo yatokanayo na upinzani wa maquraish dhidi ya uislamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu
Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu. Soma Zaidi...

Kusilimu kwa Wachawi wa Firaun
Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as). Soma Zaidi...

Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar
Soma Zaidi...

Maandalizi ya Kimafunzo aliyoandaliwa Mtume Muhammad
(i) Suratul- ‘Alaq (96:1-5)“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba Aliyemuumba mwanaadamu kwa ‘alaq. Soma Zaidi...

tarekh
Soma Zaidi...

Historia ya Al-Khidhri
Jina Al-Khidhri halikutajwa mahali popote katika Qur’an. Soma Zaidi...

Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake
Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Bani Israil
Soma Zaidi...

Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni
“Na (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza. Soma Zaidi...

Imam Bukhari na Sahihul Bukhari
Soma Zaidi...

Kuanzishwa kwa mahakama na mahakama ya Kadhi wakati wa makhalifa
Soma Zaidi...