Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.w)unaolandana na Elimu sahihi.

(ii) Tujiepushe na tabia ya kiiblis ya kumtukuza au kumdharau mtu kutokana na nasaba, rangi, sura, hali yake kiuchumi, n.k.

(iii) Tujiepushe na tabia ya Kiiblis ya kuwa na chuki binafsi dhidi ya watu wasio na hatia yeyote.

(iv) Tujiepushe na tabia ya Kiiblis ya kibri na majivuno.

(v) Tuwe na msimamo katika kutekeleza amri za Allah(s.w) na Mtume wake na tusiwe tayari kuyumbishwa na hadaa za shaitwani.

(vi) Tunapofikwa na tashwishi za kishetani tujikinge kwa Allah(s.w).



“Na kama shetani akikushawishi kwa tashwishi (zake), wewe jikinge kwa Mwenyezi Mungu (kwa kusema: A’uudhubillah Minash-shaytwanir-Rajiim). Yeye ni mwenye kusikia mwenye kujua.” (41:36)

Au ujikinge kwa kusema:




Sema: najikinga kwa Bwana mlezi wa watu. Mfalme wa watu. Muabudiwa wa watu. Na shari ya mwenye kutia wasiwasi mwenye kurejea nyuma. Atiaye wasiwasi nyoyoni mwa watu. Ambaye ni katika majini na watu. (114:1-6)

Au kuleta Dua ifuatayo:




“...... Mola wangu! Najikinga kwako uniepushe na wasiwasi wa mashetani. Na najikinga kwako, Mola wangu, ili wasinihudhurie”. (23:97-98)


(vii) Muda wote Waislamu hawana budi kuchukua tahadhari kwani kiasili (tangu mwanzo wake) Uislamu ni dini yenye maadui miongoni mwa mashetani wa kijini na watu.



................

“Na namna hii tumemfanyia kila Nabii maadui, (nao ni) mashetani katika watu na majini. Baadhi yao wanawafunulia wenziwao maneno ya kupamba pamba ili kuwadanganya…..........” (6:112)


(viii)Mwanaadamu tangu mwanzo wa kuumbwa kwake amekusudiwa kuwa Khalifa katika ardhi na nyenzo kuu ya kumuwezesha kuwa Khalifa ni elimu ya mazingira na ya mwongozo.

(ix) Tujiepushe na kuwahusudu watu juu ya meema walizotunukiwa na Allah(s.w) bali tumuelekeeAllah(s.w) kwa unyenyekevu na
k umuomba atuneemeshe kama wale aliowaneemesha.

Wala msitamani vile ambvyo MwenyeziMungu amewafadhilisha badhi yenu (kwa vitu hivyo) kuliko wengine. wanaume wanayo sehemu (kamili) ya vile walivyovichuma; na wanawake nao wanayo sehemu(kamili) ya vile walivyovichuma na mwombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake. Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.(4:32)

(x) Allah(s.w) huwaongoza na kupokea maombi ya wale wajitakasao:
........

“...... Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanaotubu na kuwapenda wanaojitakasa” (2:222)

(xi) Muislamu muumini anatakiwa ajihidi kuondosha ubaya au alipize ubaya aliofanyiwa kwa wema,yaani kumsamehe aliyemkosea kumpa aliyemnyima na kumchangamkia aliye mkasirikia. Tunahimizwa katika Qur’an:



“Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa. Ondosha (ubaya uliofanyiwa kwa wema), tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui atakuwa kama ni jamaa (yako) mwenye kukufia uchungu. Lakini (jambo hili) hawatapewa ila wale wanaosubiri wala hawatapewa ila wenye hadhi kubwa (mbele ya Mwenyezi Mungu)”(41:34-35)

(xii) Tunapoteleza na kumkosea Allah(s.w),tumuelekee kwa unyenyekevu kwa kuleta toba ya kweli kama alivyofanya Adam(a.s) na mkewe.

(xiii) Kumkosea Allah(s.w) kwa kibri kama alivyofanya Iblis ni jambo baya mno la hatari kwani humpelekea mtu kupigwa muhuri moyoni mwake kiasi cha kumfanya asione haja yoyote ya kuleta toba. Tunakumbushwa hili katika Qur’an.



“Hakika wale waliokufuru (kwa ukaidi tu na inadi) ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye hawataamini. Kama kwamba Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya ya nyoyo zao na juu ya masikio yao; na juu ya macho yao pana kifuniko; basi watakuwa na adhabu kubwa.”(2:6-7)



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1847

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam

“Na wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): “Nitakuua”.

Soma Zaidi...