Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.
Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:-
(1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.
(2)Hujaribu kumdanganya Mwenyezi Mungu pamoja na waumini wakidhani kuwa yaliyo nyoyoni mwao hayajulikani.
(3)Hufanya maovu katika ardhi huku wakidai kuwa wanatenda mema.
(4)Huwaona waumini wa kweli kuwa ni wajinga kwa kufuata kwao Uislamu inavyotakikana.
(5)Huwacheza shere Waislamu.
(6)Hujiiona kuwa wao ni bora kuliko waumini
(7)Hujikomba kwa viongozi wa kitwaaghuti.
(8)Huwafanya makafiri na Washirikina kuwa marafiki zao wa ndani badala ya Allah(s.w) Mtume wake na waumini.
(9)Huyapenda zadi maslahi ya dunia kuliko ya akhera.
(10)Hukataa kuhukumiwa na sheria za Allah (s.w).
(11)Hutumia viapo kama kifuniko cha maovu yao.
(12)Huchanganya haki na batili, kufuru na Uislamu.
(13)Huendea swala kwa uvivu.
(14)Hawamtaji Allah ila kidogo sana.
(15)Huwafitinisha Waislamu.
(16)Huchukia Waislamu wanapofikwa na kheri na kufurahia wanapofikwa na msiba.
(17)Hawako tayari kutoa mali zao katika njia ya Allah (s.w) na wakitoa chochote hutoa kwa ria
(18)Huwazuia watu kutoka katika njia ya Allah.
(19)Huzifanyia stihizai (shere) aya za Qur-an.
(20)Huamrisha maovu na kukataza mema.
(21)Husema uongo na kuvunja ahadi.
(22)Huwa vunja moyo na kuwakatisha tamaa Waislamu wa kweli ili wabakie katika ukafiri sawa na wao.
(23)Hufanya hiyana katika mambo ya kheri na kuchagua mambo mepesi mepesi.
(24)Wanawaogopa na kuwachelea watu zaidi kuliko Allah (s.w).
(25)Hush irikiana na maadui kuupiga vita Uislamu na Waislamu.
Umeionaje Makala hii.. ?
KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji.
Soma Zaidi...Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.
Soma Zaidi...Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwnda kujifunz anamna nambavyo Sahaba Ukasha alivyochangamkia fursa katika mambo ya heri
Soma Zaidi...