picha

Muhutasari wa sifa za wanafiki

Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.

Muhutasari wa sifa za wanafiki

Muhutasari wa sifa za wanafiki


Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:-
(1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.


(2)Hujaribu kumdanganya Mwenyezi Mungu pamoja na waumini wakidhani kuwa yaliyo nyoyoni mwao hayajulikani.


(3)Hufanya maovu katika ardhi huku wakidai kuwa wanatenda mema.


(4)Huwaona waumini wa kweli kuwa ni wajinga kwa kufuata kwao Uislamu inavyotakikana.


(5)Huwacheza shere Waislamu.


(6)Hujiiona kuwa wao ni bora kuliko waumini


(7)Hujikomba kwa viongozi wa kitwaaghuti.


(8)Huwafanya makafiri na Washirikina kuwa marafiki zao wa ndani badala ya Allah(s.w) Mtume wake na waumini.


(9)Huyapenda zadi maslahi ya dunia kuliko ya akhera.


(10)Hukataa kuhukumiwa na sheria za Allah (s.w).


(11)Hutumia viapo kama kifuniko cha maovu yao.


(12)Huchanganya haki na batili, kufuru na Uislamu.


(13)Huendea swala kwa uvivu.


(14)Hawamtaji Allah ila kidogo sana.


(15)Huwafitinisha Waislamu.


(16)Huchukia Waislamu wanapofikwa na kheri na kufurahia wanapofikwa na msiba.


(17)Hawako tayari kutoa mali zao katika njia ya Allah (s.w) na wakitoa chochote hutoa kwa ria


(18)Huwazuia watu kutoka katika njia ya Allah.


(19)Huzifanyia stihizai (shere) aya za Qur-an.


(20)Huamrisha maovu na kukataza mema.


(21)Husema uongo na kuvunja ahadi.


(22)Huwa vunja moyo na kuwakatisha tamaa Waislamu wa kweli ili wabakie katika ukafiri sawa na wao.


(23)Hufanya hiyana katika mambo ya kheri na kuchagua mambo mepesi mepesi.


(24)Wanawaogopa na kuwachelea watu zaidi kuliko Allah (s.w).


(25)Hush irikiana na maadui kuupiga vita Uislamu na Waislamu.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 1269

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 ai web app     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

tarekh 09

KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu hali ya bara arabu zama za jahiliyyah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na kuanzishwa kwa dola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)

KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.

Soma Zaidi...