Navigation Menu



Muhutasari wa sifa za wanafiki

Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.

Muhutasari wa sifa za wanafiki

Muhutasari wa sifa za wanafiki


Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:-
(1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.


(2)Hujaribu kumdanganya Mwenyezi Mungu pamoja na waumini wakidhani kuwa yaliyo nyoyoni mwao hayajulikani.


(3)Hufanya maovu katika ardhi huku wakidai kuwa wanatenda mema.


(4)Huwaona waumini wa kweli kuwa ni wajinga kwa kufuata kwao Uislamu inavyotakikana.


(5)Huwacheza shere Waislamu.


(6)Hujiiona kuwa wao ni bora kuliko waumini


(7)Hujikomba kwa viongozi wa kitwaaghuti.


(8)Huwafanya makafiri na Washirikina kuwa marafiki zao wa ndani badala ya Allah(s.w) Mtume wake na waumini.


(9)Huyapenda zadi maslahi ya dunia kuliko ya akhera.


(10)Hukataa kuhukumiwa na sheria za Allah (s.w).


(11)Hutumia viapo kama kifuniko cha maovu yao.


(12)Huchanganya haki na batili, kufuru na Uislamu.


(13)Huendea swala kwa uvivu.


(14)Hawamtaji Allah ila kidogo sana.


(15)Huwafitinisha Waislamu.


(16)Huchukia Waislamu wanapofikwa na kheri na kufurahia wanapofikwa na msiba.


(17)Hawako tayari kutoa mali zao katika njia ya Allah (s.w) na wakitoa chochote hutoa kwa ria


(18)Huwazuia watu kutoka katika njia ya Allah.


(19)Huzifanyia stihizai (shere) aya za Qur-an.


(20)Huamrisha maovu na kukataza mema.


(21)Husema uongo na kuvunja ahadi.


(22)Huwa vunja moyo na kuwakatisha tamaa Waislamu wa kweli ili wabakie katika ukafiri sawa na wao.


(23)Hufanya hiyana katika mambo ya kheri na kuchagua mambo mepesi mepesi.


(24)Wanawaogopa na kuwachelea watu zaidi kuliko Allah (s.w).


(25)Hush irikiana na maadui kuupiga vita Uislamu na Waislamu.



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 633


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)
(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s. Soma Zaidi...

Je, Nabii Isa(a.s) ni Mtoto wa Mungu?
Mwenyezi Mungu si kiumbe. Soma Zaidi...

Kuanzishwa kwa vitenge vya ulinza na Usalama, na usalama wa taifa
Soma Zaidi...

HISTORIA YA MAISHA YA MTUME S.A.W KABLA YA UTUME
MAISHA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Historia ya bi Khadija na familia yake na chanzo cha utajiri wake.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 17. Historia ya Bi Khadija na familia yake. Soma Zaidi...

Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad
7. Soma Zaidi...

Hijra ya Mtume(s.a.w) Kwenda Madinah
Njama za Kumuua Mtume(s. Soma Zaidi...

tarekh
MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU). Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME DAUD(A.S).
Nabii Daudi(a. Soma Zaidi...

UTARATIBU WA KULEA MIMBA
Soma Zaidi...