Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Bani Israil
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Bani Israil
Kutokana na historia ya Bani Israil (Mayahudi) tunapata mafunzo ya msingi yafuatayo:
(i) Baada ya Mayahudi kufanya makosa hayo yaliyoainishwa walighadhibikiwa na Allah(s.w) na kunyang'anywa hadhi yao
ya kuwa Taifa teule na kupewa Waumini wa Ummat Muhammad(s.a.w) kama inavyoainishwa katika Qur'an:
Nyinyi ndio Umma bora kuliko umma zote zilizodhihirishiwa watu (ulimwenguni) - mnaamrisha yaliyo mema na mnakataza yaliyo maovu, na mnamwamini Mwenyezi Mungu. Na kama wale waliopewa Kitabu wangaliamini (kama walivyoamrishwa) ingalikuwa bora kwao. (Lakini) miongoni mwao wako wanaoamini; na wengi wao wanatoka katika taa ya Mwenyezi Mungu' (3:110).
(ii) Cheo cha kuwa bora walichopewa Waumini kina masharti yale yale ya kusimamisha ufalme wa Allah(s.w) hapa ulimwenguni na kuwa kiigizo chema.
"Na vivyo hivyo Tumekufanyeni Ummah bora (kama Qibla chenu Tulivyokifanya bora) ili muwe mashahidi juu ya watu na Mtume awe shahidi juu yenu.........β (2:143).
(iii) Waislamu wa Ummah huu na wao hawatasalimika na ghadhabu pamoja na laana ya Allah(s.w) endapo wataiga mwenendo wa Mayahudi na kurudia makosa yao yaliyoorodheshwa hapo juu na mengineyo yaliyoainishwa katika Qur'an.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitabu cha Afya π2 ai web app π3 Dua za Mitume na Manabii π4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π5 Simulizi za Hadithi Audio π6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Historia ya Dhulqarnain
Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: βMwenye Pembe Mbiliβ.
Soma Zaidi...Mbinu na njia walizotumia maadui wa uislamu dhidi ya waislamu na dola ya kiislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni
βNa (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza.
Soma Zaidi...