HISTORIA NA MAISHA YA MTUME IDRISA (A.S)
Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a.
Nabii Idris (a.s)
Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a.s) katika Mitume 25 waliotajwa katika Qur-an ni Idrisa(a.s).
Nabii Idrisa(a.s) ametajwa kwa ufupi katika Qur-an
“Na mtaje Idrisa katika Kitabu (hiki). Bila shaka yeye alikuwa mkweli sana (na) Nabii. Na tulimuinua daraja ya juu kabisa.” (19:56-57).
Na (mtaje) Ismail, na Idrisa na Dhul-kifli wote walikuwa miongoni mwa wanaosubiri.” (21:85)
Katika aya hizi Nabii Idrisa(a.s) ametajwa kuwa alikuwa Nabii wa Allah(s.w) aliyepea katika ukweli na subira na Allah akamnyanyua daraja ya juu kabisa kutokana na sifa zake hizo. Hatuna taarifa zaidi ya harakati za Nabii Idrisa(a.s) katika kuhuisha Uislamu na kuusimamisha katika jamii yake, bali itoshe tu kuwa mwanaharakati anayefanya kazi ya Mitume wa Allah ya kusimamisha Uislamu katika jamii hanabudi kujipamba na tabia ya ukweli na subira.
Inasemekana kuwa nabii Idrisa:-
1. Ndiye mtu wa kwanza kuandika
2. Ndiye mtume wa kwanza kutoa darsa
3. Ndiye mtu wa kwanza kushona nguo
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija
Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu.
Soma Zaidi...Mtume kumuoa bi khadija
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 15. Hapa utajifunza kuhusu chimbuko la ndoa ya Mtume s.a.w na bi Khadija.
Soma Zaidi...Mafunzo kutokana na vita vya badri
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu
Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a.
Soma Zaidi...Maana ya kusimamisha uislamu katika dini
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...