Ni ipi hasa siku ambayo nitafute ujauzito

Ni ipi hasa siku ambayo nitafute ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kutafuta ujauzito

Download Post hii hapa

NI IPI HASA SIKU AMBAYO NITAFUTE UJAUZITO?

Kama ulipojifunza hapo juu kuwa zipo siku maalaumu ambazo yai hukomaa. Katika siku hizo mojawapo yai huletwa kwenye mirija ya falopia. Baada ya kukokotoa siku zako hapo juu sasa itakubidi kuongeza siku moja ama mbili nyuma. Hii ni kwa sababu makadirio ya siku hutofautiana. Na si lazima kkutafuta toto katika siku zote hizi. Unaweza kuruka kwa siku moja moja.

 

Jitahidi kufanya tendo la ndoa hasa katika siku hizo nne ulizozipata baada ya kukokotoa. Katika siku hizo jitahidi kufanya tendo siku ambayo itakuwa na sifa zifuatazo:-

 

1.Majimaji ya mwanamke ukeni yatakuwa ni mengi kuliko siku zilizopita. Mwanamke mwenyewe anaweza kujichunguza hali hii na kuigundua ila taabu. Anaweza kutumia kidole ama kitambaa safi kuchunguza uwepo wa majimaji haya katika ukeni kwake. Kumbuka hali hii isiambatane na shida nyingine za afya kama PID. Wakati mwingine inaweza kuwa ngumu kuchunguza hasa kwa wale wanaotumia uzazi wa mpango hasa hasa kwa kutumia vidonge vya homoni.

 

2.Joto la mwanamke litakuwa ni kubwa kuliko siku nyingine. Joto hili sio homa, na lisiambatane na sababu nyingine kama maumivu ya kichwa, ama kutokana na kulala sana, ama misongo ya mawazo. Kikawaida siku ambayo yai hutolewa joto la mwanamke linakuwa kubwa hivyo akishiriki siku hii ujauzito ni rahisi kuingia.

 

3.Siku ambayo mwanamke atakuwa na hamu sana ya kushiriki tendo. Wakato ambapo yai hutolewa kuna homoni huzalishwa kwa wingi. Homoni hizi zinaweza kusababisha mwanamke kutamani sana kushiriki tendo zaidi ya siku nyingine.

 

Pindi mwanamke atakapojigundua kuwa siku hii ameipata basi ni vyema kushiriki tendo ndani ya siku hii ama siku itakayofata haraka iwezekanavyo, maana yai la mwanamke linaweza kufa ndani ya muda mchach masaa 12 mpaka 24.

 

Kuna baadhi ya wanawake wanapata changamoto kutokana na kuwa na shida ya homoni katika mfumo wao wa uzazi. Hawa ni wale ambao siku zao hawazipati katika mpangilio sawa. Ni vyema wakafika kituo cha afya kupata matibabu ya tatizo hilo.

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1553

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

DALILI ZA TEZI DUME
DALILI ZA TEZI DUME

Tezi dume hii ni tezi inayopatikana katika katika mfumo wa uzazi wa mwanaume Ila hujulikana kama PROSTATE GLAND. pia hukua karibu na kibofu Cha mkojo na mirija ya mkojo hutumika kuzalisha majimaji (simen) yanayobeba mbegu hivyo bas mk

Soma Zaidi...
Mambo yanayopunguza nguvu za kiume
Mambo yanayopunguza nguvu za kiume

Posti hii inaelezea kuhusiana na nguvu za kiume zinavyopungua na Ni Mambo gani yanayofanya zipungue

Soma Zaidi...
Dalili za mimba katika mwezi wa kwanza
Dalili za mimba katika mwezi wa kwanza

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba katika mwezi was kwanza

Soma Zaidi...
Umuhimu wa uzazi wa mpango kwa Mama
Umuhimu wa uzazi wa mpango kwa Mama

Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.

Soma Zaidi...
kunauwezekano wa darri ya kchefuchefu ictokee kabsa kwa mjauzito
kunauwezekano wa darri ya kchefuchefu ictokee kabsa kwa mjauzito

Kichefuchefu ni moja katika dalili za mimba za mapema, Lucinda je upo uwezekano kwa mwanamke kuwa na ujauzito bila hata ya kuwa na kichefuchefu?

Soma Zaidi...
Namna ya kutunza uke
Namna ya kutunza uke

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza uke, tunajua wazi kuna magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo uke hautaweza kutunzwa vizuri na pia uke ukitunzwa vizuri kuna faida ya kuepuka maradhi ya wanawake kwa njia ya kutunza uke.

Soma Zaidi...
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa kondo la nyuma
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa kondo la nyuma

Kondo la nyuma ni sehemu ya mwili wa mama anapokuwa mjamziti,kondo la nyuma husaidia katika kazi mbalimbali katika ukuaji wa mtoto.

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya via vya uzazi kwa Mama mjamzito.
Mabadiliko ya via vya uzazi kwa Mama mjamzito.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye via vya uzazi kwa wajawazito, tunajua kuwa Mama akibeba mimba tu kuna mabadiliko utokea katika sehemu mbalimbali za mwili.

Soma Zaidi...
Ijue kazi ya homoni ya HCG wakati wa kupima mimba.
Ijue kazi ya homoni ya HCG wakati wa kupima mimba.

Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya HCG katika kupima mimba, HCG maana yake ni human chorionic gonadotropin ni homoni ambayo uonekanekana kwenye mkojo na damu kama mtu ana mimba.

Soma Zaidi...
Mimba huonekana katka mkojo baada ya muda gan tangu itungwe
Mimba huonekana katka mkojo baada ya muda gan tangu itungwe

Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.

Soma Zaidi...