image

UTAMBUE UGNJWA WA UTI DALILI ZAKE, CHANZO NA TAHADHARI DHIDI YAKE

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

UTAMBUE UGNJWA WA UTI DALILI ZAKE, CHANZO NA TAHADHARI DHIDI YAKE

4.UGONJWA WA UTI
UTI ni kifupisho cha Urinary Track Infection. Ni ugonjwa unaoshambulia katika mfumo wa mkojo, hususan kibofu, figo na mirija ya urethra. Ugonjwa huu umekiwa ukiwapata sana wanawake kwa kiasi kikubwa kuliko wanaume. Baadhi ya takwimu zinaonyesha kuwa kati ya watu 5 mmoja ana UTI.

Maambukizi ya ugonjwa huu yanapatikana hasa chooni. Pia huenda ugonjwa huu ukaenezwa kupitia kuingiliana kimwili na utaratibu mbovu wa kujisafisha baada ya kukidhi haya. Ugonjwa huu umekuwa ukiwapata zaidi watu ambao wanatumia vyoo vya shirika yaani vyoo vinavyotumiwa na watu wengi.

Ugonjwa wa UTI umekuwa ukisababishwa na bakteria kwa kiasi kikubwa. Bakteria aina ya E.coil ambao wanapatikana kwenye utumbo mkubwa wamekuwa wakisababisha UTI kwa kiasi kikubwa kuliko bakteria wengine. Pia fangasi (fungi) na virusi huweza kusababisha UTI japo kwa kiwango kidogo.

Mtu anaweza kuchukuwa tahadhari dhidi ya ugonjwa huu kwa,;-
1.Jisafishe kutokea mbele kuelekea nyuma baada ya kukidhi haja kubwa (kwa wanawake). Hii husaidia kuzuia bakteria wanaotoka kwenye utumbo mkubwa wasipate nafasi ya kuingia kwenye njia ya haja ndogo.
2.mwaga maji kila uingiapo chooni kwaajili ya nkujisaidia. Kitendo hiki kitaondosha vijidudu vilivyopo pale chini.
3.Jisafishe sehemu za siri kabla ya kuingiliana na baada.
4.Hakikisha unakwenda kutoa haja ndogo (kukojoa) baada ya tendo la ndoa. Kitendo hiki kitasaidia kuondosha vijidudu vilivyoingia wakati wa tendo.
5.Nenda katoe haja ndogo haraka sana baada ya kuhisi.
6.Kunywa maji mengi zaidi. Husaidia kuondowa vijidudu kwa njia ya mkojo.
7.Vaa nguo za ndani za pamba, kavu na zisizobana.nguo za mpira na zinazobana husababisha jasho (majimaji) sehemu za siri. Majimaji haya husaidia bakteria kukuwa na kuishi hivyo wanaweza kuathiri njia ya mkojo.

Ugonjwa wa UTI una dalili nyingi na huenda nyingine zikafanana na dalili za malaria. Miongoni mwa dalili hizi ni;-
1.Maumivu wakati wa haja ndogo
2.Kutowa mkojo mchafu. Mkojo unawea kuwa na rangi sana, ua kama wa mawingu na kadhalika.
3.Harufu kali sana ya mkojo.
4.Mkojo kuwa na damu
5.Kukojoa marakwa mara hata kama mkojo utakuwa ni mchache sana.
6.Maumivu ya mgongo na tumbo kwa chini.(lower abdomen)
7.Maumivu ya kichwa.
8.Kuhisi uchovu sana
9.Miwasho sehemu za siri.

Itambulike kuwa ugonjwa wa UTI unatibika bila ya matatizo. Jambo la msingi ni kuwa wagonjwa wengi wamekuwa hawamalizi dozi. Kwakuwa ugonjwa huu umeenea sana na ni rahisi kuupata imetokea hali za kujirudia rudia. Hivyo mgonjwa ni muhimu kuchukuwa tahadhari tulizotzja hapo juu wakati akiwa anatumia dozi. Pia watu wawe makini na tiba za kiasili ambazo husemekana zinatibu UTI.


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 130


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

AFYA YA UZAZI (UJAUZITO, KULEA WATOTO, AFYA YA MIMBA NA MTOTO, MAGONJWA YA KINAMAMA NA WANAUME)
Soma Zaidi...

Habari za uzima,nimesoma makala yako tumbo linaniuma upande wa kulia Ila sisikii Sana yenyewe Ila nikibonyeza na mkono ndio inauma yaani ni Kama nimegongwa sehem flani alafu Kuna maumivu lakini ni mpaka upaguse ndio una experience maumivu Kama Kuna namna
Kama unasumbuliwana tumbo upande wa kulia, kushoto, kitomvuni ama kuoande wa kuliavkwachini, basi muulizaji huyu atakupa uelewa. Soma Zaidi...

Dua Sehemu ya 02
Zijuwe nyakati ambazo dua inakubaliwa kwa haraka zaidi. Zijuwe nyakati ambazo ukiomba dua hitakubaliwa. Soma Zaidi...

KWA NINI MBU HAWEZI KUAMBUKIZA HIV (UKIMWI)
Tumekusha kuona na kujua kuwa mbu anaweza kuambukiza maradhi mengi na ya virusi kama zika. Soma Zaidi...

MAAJABU YA MBU
7. Soma Zaidi...

YANAYOATHIRI AFYA KUTOKANA NA VIZAZI, FAMILIA NA KURITHI
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Kitabu Cha Darsa za Afya
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa
Kujiepusha na Vishawishi vya ZinaaKatika macho ya sheria kitendo cha zinaa kinahesabiwa pale wanapokutana kimwili mwanamume na mwanamke nje ya ndoa. Soma Zaidi...

YANAYOATHIRI AFYA KATIKA SHUGHULI ZA KILA SIKU
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Jinsi ya kuepuka magonjwa ya figo
Figo ni moja katika orgn zenye umuhimu sana mwilini na endapo itaatirika kwa namna yeyote ile, madhara makubwa kwenye mwili yanaweza kutokea na hata kifo. Katika post hii utajifunza jinsi ya kulinda mwili wako dhidi ya matatizo ya figo Soma Zaidi...

TAHADHARI KWENYE VYAKULA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

UTAMBUE UGNJWA WA UTI DALILI ZAKE, CHANZO NA TAHADHARI DHIDI YAKE
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...