picha

Ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango.

Posti hii inahusu zaidi ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango, sio kwa imani potofu ambazo Watu utumia kuelezea uzazi wa mpango.

Ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango.

1.Uzazi wa mpango ni kwa ajili ya Watu wote ambao ni wanawake na wanaume kwa sababu kuna na njia za uzazi wa mpango ambazo wanaume wanapaswa kushirikiana kwa hiyo siyo kweli kwamba njia za uzazi wa mpango ni kwa ajili ya wanawake tu.

 

2. Matumizi ya njia za uzazi wa mpango hayawezi kupunguza hamu ya tendo la ndoa bali usababisha tendo la ndoa kwa tamu zaidi kwa sababu hakuna anayefikilia kama kuna uwezekano wa kupata mimba kwa hiyo njia za uzazi wa mpango uondoa hofu ya mimba.

 

3.Njia za uzazi wa mpango hazisababishi ugumba hata kidogo kwa sababu zenyewe kazi yake ni kuzuia mimba kwa hiyo haziingilian na mambo ya ugumba.

 

4. Kondomu haiwezi kusafili katika via vya uzazi yaani kutoka sehemu moja kwenda nyingine kadri ya mpangilio wa via vya uzazi vilivyo labda kondomu inaweza kutoboka sio kusafiri kutoka kwenye uke, kwenda kwenye mfuko wa uzazi na kwenye ovari hii haiwezekani kabisa.

 

5. Njia za uzazi wa mpango zinaweza kusababisha maudhi madogo madogo sio maudhi makubwa kufikia kiasi cha kutoa uhai wa Mama kwa hiyo maudhi madogo madogo ni kama vile kutokwa na damu na hiyo ni kwa mda mfupi tu 

 

6. Njia za uzazi wa mpango haziwezi kusababisha kuzaliwa kwa mtoto mfu bali kuzaliwa kwa mtoto mfu usababishwa na vitu vingine kabisa sio uzazi wa mpango, kwa hiyo Watu waache imani potofu ambazo zinaweza kusababisha kuzaa watoto wengi na wasio na mp as mpangilio kk wa sababu ya imani potofu za Watu wengine.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2123

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 ai web app     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Dalili za kuziba kwa mirija ya uzazi

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea kwa sababu ya kuziba kwa mishipa ya uzazi, ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo la kuziba kwa mishipa ya uzazi.

Soma Zaidi...
Mtoto anaanz kucheza kwa mda gan

Kuna watoto wengine huanza kucheza mapema kuliko watoto wengine. Tunapozungumzia kucheza kwa mtoto aliye tumboni yaani mimba hapa inatubidi tuangalie kwa undani zaidi, je ni muda gani mtoto ataanza kucheza?

Soma Zaidi...
Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.

Post huu inahusu zaidi utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito, ni chakula anachopaswa kutumia na ambavyo hapaswi kutumia kwa Mama mjamzito mzito, kwa sababu Mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika matumizi ya chakula ili kuweza kuongeza vitu muhimu mwil

Soma Zaidi...
Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama mtoto wa kike

Posti hii inakwenda kukueleza jinsi ya kuwjuwa kama mtoto ni wa kike ama wa kiume.

Soma Zaidi...
Mimi naumwa na tumbo chini ya kitovu upande wa kulia, ninapotok kushiriki tendo la ndoa ndonapata maumivu zaid pia nawashwa sehemu za siri itakuwa shida ni nin?

Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa yanaweza kuwa ni dalili ya maradhi fulani, ama shida kwenye mfumo w uzazi. PID na UTI hutuhumiwa kuwa ni katika sababu hizo. Ila zipo nyingine nyingi tu. Kama ina hali hii vyema ukafika kituo cha afya

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.

Soma Zaidi...