picha

Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa watoto, sio akina Mama peke yao wanaofaidika na uzazi wa mpango vile vile na watoto wanafaidika na uzazi wa mpango kama ifuatavyo.

Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.

1.kwanza kabisa tunajua lengo kuu la uzazi wa mpango ni kupata namba ya watoto wanaohitajika na kuwapa nafasi ya kutosha kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine, kwa hiyo na watoto wanapata faida ya uzazi wa mpango kama ifuatavyo.

 

2.uzazi wa mpango ukitumiwa ipasavyo unawapa watoto nafasi ya kupendwa na wazazi wao kwa mfano watoto wakizidiana miaka minne kwa vyovyote yule mtoto atainja mapenzi ya wazazi wake kuliko wale watoto wanaozidiana mwaka mmoja mmoja kwa hiyo tuwape watoto nafasi kati ya mtoto mmoja kwenda mwingine ili waweze kuonja mapenzi ya kweli kutoka kwa wazazi wao.

 

3.Pia uzazi wa mpango unawapa watoto nafasi ya kunyonya kwa mda mrefu , tunajua wazi kubwa mtoto alinyonya kwa mda unaofaa anakuwa na afya nzuri pia anaweza kukingwa dhidi ya magonjwa kuna  wataalamu wanasema mtoto alkinyonya kwa mda wa kutosha anakuwa na akili za kufikiria kwa hiyo tuwape watoto mda waweze kunyonya kwa mda wa kutosha.

 

4.Uzazi wa mpango inawasaidia watoto wapate elimu ya kutosha kwa sababu mtoto akikaa na Wazazi kwa mda anajifunza mambo mengi kuliko wakiwa wengi na pia wazazi wataweza kupata Ela na kumpeleka mtoto wao shule nzuri kuliko kama wangekuwa wengi.

 

5.Pia uzazi wa mpango unasaidia kupunguza vifo vya watoto wakiwa wadogo , kwa sababu ya kukosa mahitaji muhimu au kuzaliwa wakiwa hawajafikishwa umri au na uzito mdogo kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa hata watoto wenyewe ikiwa wazazi wakitumia njia ya uzazi wa mpango nao wanapata faida kwa hiyo wazazi na jamii kwa ujumla mnaalikwa kutumia njia za uzazi wa mpango ili kuyafanya maisha ya watoto yapendeze

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 1649

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Dalili za tezi dume na sababu za kutokea kwa tezi dume.

dalili za ugonjwa wa tezi dume, na sababu za kutokea kwa tezi dume, maana ya tezi dume na athari zake

Soma Zaidi...
Mambo ambayo mama anapaswa kujua akiwa mjamzito

Posti hii inahusu zaidi mambo anyopaswa kujua akiwa mjamzito. Ni mambo muhimu ya kuzingatia kwa mama akiwa mjamzito.

Soma Zaidi...
Madhara ya kutumia madawa ya shida ya upumuaji

Post hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya shida ya upumuaji, ni madhara madogo madogo ambayo utokea kwa watumiaji wa matatizo ya kupumua.

Soma Zaidi...
Ongezeko la homoni ya estrogen

Posti hii inahusu zaidi ongezeko la homoni ya estrogen, kwa kawaida homoni hii ya estrogen inapaswa kulingana ikitokea ikaongezeka uleta madhara mbalimbali kwenye mwili na Kuna dalili ambazo zzz inaweza kujionesha wazi mpaka tukafahamu kuwa ni tatizo la o

Soma Zaidi...
Wanaopasawa kutumia PEP

PEP Ni dawa ambazo utumiwa na watu wanaojamiiana na watu wenye virus vya ukimwi ila wenyewe hawawezi kupata kwa sababu ya kutumia dawa hizo.

Soma Zaidi...
Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.

Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h

Soma Zaidi...