picha

Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa watoto, sio akina Mama peke yao wanaofaidika na uzazi wa mpango vile vile na watoto wanafaidika na uzazi wa mpango kama ifuatavyo.

Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.

1.kwanza kabisa tunajua lengo kuu la uzazi wa mpango ni kupata namba ya watoto wanaohitajika na kuwapa nafasi ya kutosha kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine, kwa hiyo na watoto wanapata faida ya uzazi wa mpango kama ifuatavyo.

 

2.uzazi wa mpango ukitumiwa ipasavyo unawapa watoto nafasi ya kupendwa na wazazi wao kwa mfano watoto wakizidiana miaka minne kwa vyovyote yule mtoto atainja mapenzi ya wazazi wake kuliko wale watoto wanaozidiana mwaka mmoja mmoja kwa hiyo tuwape watoto nafasi kati ya mtoto mmoja kwenda mwingine ili waweze kuonja mapenzi ya kweli kutoka kwa wazazi wao.

 

3.Pia uzazi wa mpango unawapa watoto nafasi ya kunyonya kwa mda mrefu , tunajua wazi kubwa mtoto alinyonya kwa mda unaofaa anakuwa na afya nzuri pia anaweza kukingwa dhidi ya magonjwa kuna  wataalamu wanasema mtoto alkinyonya kwa mda wa kutosha anakuwa na akili za kufikiria kwa hiyo tuwape watoto mda waweze kunyonya kwa mda wa kutosha.

 

4.Uzazi wa mpango inawasaidia watoto wapate elimu ya kutosha kwa sababu mtoto akikaa na Wazazi kwa mda anajifunza mambo mengi kuliko wakiwa wengi na pia wazazi wataweza kupata Ela na kumpeleka mtoto wao shule nzuri kuliko kama wangekuwa wengi.

 

5.Pia uzazi wa mpango unasaidia kupunguza vifo vya watoto wakiwa wadogo , kwa sababu ya kukosa mahitaji muhimu au kuzaliwa wakiwa hawajafikishwa umri au na uzito mdogo kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa hata watoto wenyewe ikiwa wazazi wakitumia njia ya uzazi wa mpango nao wanapata faida kwa hiyo wazazi na jamii kwa ujumla mnaalikwa kutumia njia za uzazi wa mpango ili kuyafanya maisha ya watoto yapendeze

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 1623

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 ai web app     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Sababu za maumivu wakati wa tendo la ndoa

Kama unapata maumivu wakati wa tendo la ndoa, suluhisho lako lipo kwenye makala hii

Soma Zaidi...
Kujaa gesi tumboni

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kujaa tmgesi tumbon

Soma Zaidi...
Mimi kwenye korodani yai moja limezungukwa na majimaji ,na haya maji yamekuwepo toka utotoni mwangu lakin bado sijayaona matatizo yake , je kitaaramu hii inaweza kua na athari gani? ,Naombeni ushauri

Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
Ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango.

Posti hii inahusu zaidi ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango, sio kwa imani potofu ambazo Watu utumia kuelezea uzazi wa mpango.

Soma Zaidi...
Mabadiliko kwenye uke wa Mama pale anapobeba mimba.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye uke wa Mama pale anapobeba tu mimba, Mama anapobeba mimba Kuna mabadiliko Katika uke wa Mama kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...