UMBILE LA MBINGU NA ARDHI

UMBILE LA MBINGU NA ARDHI

“Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s.

Download Post hii hapa

UMBILE LA MBINGU NA ARDHI

UMBILE LA MBINGU NA ARDHI


“Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s.w) kwa wenye akili.” (3:190).


Mungu, Muumba wa kila kitu ndiye mmiliki pekee wa viumbe vyote. Ni Yeye anayebadili mielekeo ya upepo,anayekusanya mawingu, anayewasha jua na kuiangazia dunia na kudhibiti sayari zizunguuke katika mihimili yao.



Kudai maisha haya ya dunia na ulimwengu mzima yanatokana na bahati nasibu ni kutokitumia kipawa cha busara alichotunukiwa kila mwanaadamu mwenye akili timamu. Mpango bora wa dunia na ulimwengu kwa ujumla unapinga uwezekano wa kutokea kwa bahati nasibu tu, na kinyume chake ni ishara ya wazi ya uwezo wa Allah(s.w)usio na kikomo unaodhihirisha kuwepo kwake.



Wakati ambapo ni muhali hata kwa kitu chepesi kufanya mzunguko wa moja kwa moja katika njia yake bila kwenda kombo, dunia pamoja na ukubwa wake yenye mkusanyiko wa vitu visivyo na idadi hufanya hivyo.


Na imekuwa ikifanya hivyo kwa miaka dahari, na dahari, tangu dunia kuumbwa na kuanza mzunguko wake. Allah anasema Yeye ndiye mfanyaji wa mahesabu ya mzunguko huo.
Hakika Mw enyezi Mungu am ekw is ha kiw ekea kila kitu kipimo chake. (65:3)Utaratibu huo bora wa ulimwengu unaendeshwa kwa mfumo wa ajabu unaokwenda kwa kutegemea mihimili isiyo na mashiko.Wengine hudhani kuwa baada ya kuumba, Allah(s.w)amekiacha kila kitu kijiendeshe chenyewe tu. La hasha kila tukio litokealo mahala popote pale ulimwenguni hutokea kwa idhini ya Allah(s.w) na chini ya udhibiti wake. Qur’an inatufahamisha:


Je! Hujui ya kwamba Mwenyezi Mungu anajua yaliyoko mbinguni na ardhini? Bila shaka yote yamo kitabuni mwake. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni sahali. (22:70)


Kwa ujumla, umbile la mbingu na ardhi pamoja na vyote vilivyomo - jua, mwezi, nyota, sayari mbali mbali, milima na mabonde, maji ya mvua, bahari, mito na maziwa, mimea ya kila namna, wanyama wa kila namna na kadhalika ni hoja kubwa ya kuthibitisha kuwepo Allah (s.w) na utukufu wake kwa kila mwenye kutumia akili yake vizuri. Kila mtu atakavyobobea katika taaluma zinazohusiana na maumbile ya mbingu na ardhi kama vile Jeografia, Elimu ya anga (Astronomy), Elimu ya mimea (Botany), Elimu ya wanyama (Zoology), n.k. ndivyo Imani yake ya kuwepo Allah (s.w) itakavyopea.Kwa hakika wanaomuogopa Allah (s.w) miongoni mwa waja wake ni wale wataalam...” (35:28)




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1519

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab
Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa

Soma Zaidi...
Kuamini siku ya mwisho
Kuamini siku ya mwisho

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Athari za vita vya Uhud
Athari za vita vya Uhud

Vita vya uhudi viliweza kuleta athari nyingi. Post hii itakuletea athari baadhi za vita hivyo.

Soma Zaidi...
Kwa nini Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa
Kwa nini Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa

Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.

Soma Zaidi...
 Taqwa (Hofu ya kumuogopa Allah) ni popote ulipo
Taqwa (Hofu ya kumuogopa Allah) ni popote ulipo

عَنْ أَبِي ذَرٍّ جُنْدَبِ بْنِ جُنَادَةَ، وَأَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ رَسُولِ اللَ...

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa
Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Anfal (8:2-4) na Al-Hujurat
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Anfal (8:2-4) na Al-Hujurat

"Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa khofu; na wanaposomewa aya zake huwazidishia imani na wanamtegemea Mola wao tu basi.

Soma Zaidi...
 zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama
zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama

عَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَيْضًا قَالَ: " بَيْنَمَا نَحْنُ جُلُوسٌ عِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ذَاتَ يَوْمٍ، إذْ ?...

Soma Zaidi...