Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.

Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

  1. Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni. Mara tu baada ya Nabii Adam (a.s) kuumbwa na kabla hajaruzukiwa chochote na hata kabla ya kukaribishwa kwenye neema za bustanini (Peponi) alifunzwa mambo yote ya msingi yatakayomuwezesha kuwa Khalifa hapa Ulimwenguni:



“Na (Allah (s.w)) akamfundisha Adam m ajina ya vitu vyote...” (2:31).



Naye Mtume Muhammad (s.a.w) Wahyi na amri ya kwanza aliyoipokea kutoka kwa Mola wake ni kusoma kwa ajili ya Allah (s.w). Hivyo kila Muislamu analazimika kuitekeleza kwa hima amri hii ya kwanza ili aweze kumuabudu Mola wake inavyostahiki na aweze kuwa Khalifa wake hapa ulimwenguni.Aidha kila Muislamu analazimika kujielimisha mambo ya msingi yatakayomuwezesha kuwa Muumini wa kweli na kumuwezesha kuendesha maisha yake yote ya kibinafsi na kijamii kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah.



Ni wazi kuwa Muislamu mwenye kujipamba na tabia ya kujielimisha katika mambo muhimu ya maisha kwa lengo la kupata ufanisi katika kumuabudu Allah (s.w) na kusimamisha Ukhalifa katika jamii; atakuwa tofauti kiutendaji na kiuchaji na yule aliye mvivu wa kujielimisha kama tunavyojifunza katika Qur-an:



“Je, wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?” Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu.” (39:9).



“Allah atawainua daraja wale walioamini miongoni mwenu;na waliopewa elimu watapata daraja zaidi...” (58:11)



Ukizingatia kuwa kutafuta elimu ni faradh kwa kila Muislamu mwanamume na mwanamke, mkubwa na mdogo, aya hizi zatosha kuwa



kichocheo kwa kila Muumini kujibidiisha kwa kujielimisha kwa ajili ya Allah(s.w) kwa kadri ya uwezo wake na kila wakati awe anaomba dua ifu atayo:



“... Mola wangu! Nizidishie elimu.” (20:114)





                   



Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 577

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?

Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.

Soma Zaidi...
Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku

Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.

Soma Zaidi...
KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamh juu ya ibada

Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada

Soma Zaidi...
Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama

عَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَيْضًا قَالَ: " بَيْنَمَا نَحْنُ جُلُوسٌ عِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ذَاتَ يَوْمٍ، إذْ ?...

Soma Zaidi...
NGUZO ZA IMAN

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ...

Soma Zaidi...