image

KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.

KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)

KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)


Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.w). Vitabu vya Allah (s.w) vimeshushwa kupitia kwa Mitume mbali mbali.


“Kwa hakika tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na tukaviteremsha Vitabu na uadilifu pamoja nao, ili watu wasimamie uadilifu...” (57:25).
Vitabu vya Allah (s.w) ni vingi lakini tunavyovifahamu ni vile vilivyotajwa katika Qur-an kama ifuatavyo:


Suhufi kwa Ibrahimu (a.s)


Taurati kwa Mussa (a.s)



Zaburi kwa Daud (a.s)



Injili kwa Issa (a.s)



Qur-an kwa Muhammad (s.a.w)


Lengo la kushushwa Vitabu vya Allah (s.w)Iimebainishwa wazi katika Qur-an kuwa vitabu vya Allah (s.w) vimeshushwa kupitia kwa Mitume wake ili kuwaongoza wanaadamu katika njia iliyonyooka. Njia iliyonyooka ni ile inayomuwezesha mwanaadamu kumuabudu Allah (s.w) katika kila kipengele cha maisha yake kwa kipindi chote cha uhai wake hapa ulimwenguni. Allah (s.w) amechukua ahadi ya kuwaletea watu mwongozo tangu awali pale alipowashusha wazazi wetu, Adamu (a.s) na mkewe (Hawwah) hapa ardhini kama tunavyojifunza katika Qur-an:



“Tukasema, shukeni humo nyote, na kama ukikufikieni uw ongozi utokao kw angu, basi w atakaoufuata uw ongozi wangu huo haitakuwa hofu juu yao wala haw atahuzunika.


Lakini wenye kukufuru na kuyakadhibisha maneno yetu, hao ndio watakaokuwa watu wa Motoni, humo watakaa milele”. (2:38-39).
Ahadi hii ameitekeleza Allah (s.w) kwa kuwaleta Mitume mbali mbali baada ya Adamu (a.s) na kuwashushia vitabu vyenye Uongozi na nuru. Qur-an inasisitiza:


“Hakika tuliteremsha Taurat yenye Uongozi na Nuru..” (5:44)


“Na tukawafuatishia (Mitume hao) Issa bin Maryam kuyahakikisha yaliyokuwa kabla yake katika Taurat, na tukampa Injili iliyomo ndani yake Uongozi na nuru.” (5:46 )



“Ni mw ezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa katika (mwezi) huo (hii) Qur-an ili iwe Uongozi kwa watu na hoja zilizo wazi za Uongozi wa upambanui




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 358


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Kujiepusha na Shirk
Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s. Soma Zaidi...

Mambo ya lazima kufanyiwa maiti ya muislamu
Mambo ya faradhi kuhusu maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil
Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s. Soma Zaidi...

Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab
Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu. Soma Zaidi...

Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.
Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu. Soma Zaidi...

Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir
Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu. Soma Zaidi...

Ni ipi maana ya Imani katika Uislamu, na ni zipi sifa za muumini.
Katika Uislamu imani inanguzo kuu 6.Pia muumini anatakiwa ajipambe na sifa za waumini. Posti hii itakufundisha kuhusu imani katika Uislamu. Soma Zaidi...

Mafundisho ya Mitume
Mafundisho ya mitume ni eneo lingine linalo thibitisha kuwepo Allah (s. Soma Zaidi...

Ndoto ya Nabii Yusufu(a.s) Yatimia
Yusufu(a. Soma Zaidi...

Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)
Nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu) Soma Zaidi...