Ugonjwa wa kisonono
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisonono, ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Neisseria gonococcal.
Ugonjwa wa kisonono.
1.ugonjwa wa kisonono ni ugonjwa wa zinaa ambao usambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana na mtu aliye na Ugonjwa huo bila kutumia kinga, kwa hiyo mdudu huyu uishi kwenye via vya uzazi.
2. Ugonjwa huu uwapata wanawake na wanaume ila kwa kiasi kikubwa wanaume waliotahiriwa wanapata kwa asilimia kidogo ukilinganisha na wale waliotahiriwa, kwa hiyo ni vizuri kabisa kufanya tohara ili kuweza kupunguza Maambukizi.
3. Vile vile Ugonjwa huu unatibika kwa hiyo baada ya kuihisi Dalili ni vizuri kabisa kutafuta matibabu kwa hiyo kuna dawa muhimu kwa ajili ya kutibu Ugonjwa huu dawa Zenyewe ni kama vile zimegawanyika katika makundi mawili kundi la kwanza na kundi la pili.
4. Kundi la kwanza ni Norflaxacin yenye milligram mia tano inamezwa kwa mara moja, nyingine ni ciproflaxino yenye milligram mia tano inamezwa mara moja, nyingine ni oflaxacin yenye milligram mia nne na yenyewe inamezwa kwa mara moja, nyingine ni levofloxacine milligram mia mbili hamsini na yenyewe ni mara moja na nyingine ni certriaxone milligram Mia mbili na hamsini na nyingine ni enoxacine yenye milligram mia nne. Pia dawa za sehemu ya kwanza zisipotibu vizuri za sehemu ya pili zinaweza kutumika.
5. Dawa za sehemu ya pili au kwa kitaalamu huitwa second line utumika kama first line imegoma dawa hizo ni kama cefixime milligram mia nne, cefoxitin milligram mbili ambazo utumiwa kupitia kwenye mirija ya damu, nyingine ni cefotaxime ambayo upitishwa kwenye nyama au kwa kitaalamu ni intramuscular, nyingine ni arythromysine gram Moja.
6. Kwa hiyo dawa hizi utumika kutibu kisonono pia utumika kwa ushauri wa wataalamu wa afya usipende kuzitumia kiholela kwa sababu Kuna antibiotics zenye nguvu ukizitumia kiholela unaweza kujaribu bakteria ambao ni walinzi kwenye mwili. Pia ukija kutumia dawa hizi kwa kutibu kisonono ni lazima kwanza upime ugonjwa kama unao ndo unaanza kutumia, usitumie bila kupima
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Bongolite - Game zone - Play free game π2 kitabu cha Simulizi π3 Simulizi za Hadithi Audio π4 web hosting π5 Kitau cha Fiqh π6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Arthritis (Maumivu ya viungo): Vyakula vya kusaidia kupunguza maumivu.
βArthritis, au uvimbe wa viungo, ni hali sugu inayoweza kusababisha maumivu makali, ugumu wa kusonga, na kupungua kwa ubora wa maisha. Ingawa dawa za kitaalamu ni muhimu, lishe sahihi ina jukumu kubwa katika kupunguza uvimbe wa ndani (inflammation) na kupunguza maumivu. Makala haya yanachambua kwa kina vyakula bora zaidi vya kusaidia wagonjwa wa arthritis na jinsi ya kuviingiza kwenye mlo wako wa kila siku.
Soma Zaidi...Dalili za kisukari na njia za kuzuia kisukari
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisakari, dalili zake,na namna ya kujikinga usipate kisukari au Kama tayari unakisukari ukijikinga madhara yanapungua au kupona kabisa.Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwa
Soma Zaidi...ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA
Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo.
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa schizophrenia
Schizophrenia ni ugonjwa wa akili ambao huathiri jinsi mtu anavyofikiri, kuhisi, na kuamua. Dalili za schizophrenia zinaweza kuwa kama ifuatavyo hapo chini
Soma Zaidi...Sababu kuu za maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, Tumbo la ngiri na chango
Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, na tumbo la ngiri kwa wanaume, na tumbo la chango kwa wanawake
Soma Zaidi...