Ugonjwa wa kisonono
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisonono, ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Neisseria gonococcal.
Ugonjwa wa kisonono.
1.ugonjwa wa kisonono ni ugonjwa wa zinaa ambao usambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana na mtu aliye na Ugonjwa huo bila kutumia kinga, kwa hiyo mdudu huyu uishi kwenye via vya uzazi.
2. Ugonjwa huu uwapata wanawake na wanaume ila kwa kiasi kikubwa wanaume waliotahiriwa wanapata kwa asilimia kidogo ukilinganisha na wale waliotahiriwa, kwa hiyo ni vizuri kabisa kufanya tohara ili kuweza kupunguza Maambukizi.
3. Vile vile Ugonjwa huu unatibika kwa hiyo baada ya kuihisi Dalili ni vizuri kabisa kutafuta matibabu kwa hiyo kuna dawa muhimu kwa ajili ya kutibu Ugonjwa huu dawa Zenyewe ni kama vile zimegawanyika katika makundi mawili kundi la kwanza na kundi la pili.
4. Kundi la kwanza ni Norflaxacin yenye milligram mia tano inamezwa kwa mara moja, nyingine ni ciproflaxino yenye milligram mia tano inamezwa mara moja, nyingine ni oflaxacin yenye milligram mia nne na yenyewe inamezwa kwa mara moja, nyingine ni levofloxacine milligram mia mbili hamsini na yenyewe ni mara moja na nyingine ni certriaxone milligram Mia mbili na hamsini na nyingine ni enoxacine yenye milligram mia nne. Pia dawa za sehemu ya kwanza zisipotibu vizuri za sehemu ya pili zinaweza kutumika.
5. Dawa za sehemu ya pili au kwa kitaalamu huitwa second line utumika kama first line imegoma dawa hizo ni kama cefixime milligram mia nne, cefoxitin milligram mbili ambazo utumiwa kupitia kwenye mirija ya damu, nyingine ni cefotaxime ambayo upitishwa kwenye nyama au kwa kitaalamu ni intramuscular, nyingine ni arythromysine gram Moja.
6. Kwa hiyo dawa hizi utumika kutibu kisonono pia utumika kwa ushauri wa wataalamu wa afya usipende kuzitumia kiholela kwa sababu Kuna antibiotics zenye nguvu ukizitumia kiholela unaweza kujaribu bakteria ambao ni walinzi kwenye mwili. Pia ukija kutumia dawa hizi kwa kutibu kisonono ni lazima kwanza upime ugonjwa kama unao ndo unaanza kutumia, usitumie bila kupima
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Fahamu Ugonjwa wa hepatitis C
Hepatitis C ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoshambulia ini na kusababisha kuvimba. Watu wengi walioambukizwa na virusi vya Hepatitis C (HCV) hawana dalili. Kwa kweli, watu wengi hawajui kuwa wana maambukizi ya Hepatitis C hadi uharibifu wa ini
Soma Zaidi...Ugonjwa wa bakteria unaoambukizwa na kupe.
Ugonjwa wa bakteria unaoambukizwa na kupe ambao husababisha dalili kama za mafua. Dalili na ishara za Ugonjwa huu ni kati ya kuumwa na mwili kidogo hadi homa kali na kwa kawaida huonekana ndani ya wiki moja au mbili baada ya kuumwa na kupe. Njia bora ya
Soma Zaidi...Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n
Soma Zaidi...Yajue magonjwa ya jicho
Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya jicho,ni Magonjwa ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za jicho kwa mfano kwenye retina,kuaribu mishipa ya retina ,macho kuwa makavu na pia mtoto wa jicho, hali hii ya magonjwa ya macho Usababisha madhara mbalimbali kama
Soma Zaidi...Sababu za maumivu wakati wa kujamiiana
​Maumivu wakati wa kujamiiana (kitaalamu dyspareunia) ni tatizo linalowasumbua wanawake wengi, ingawa mara nyingi halizungumzwi wazi kutokana na unyanyapaa au aibu. Maumivu haya yanaweza kusababishwa na sababu za kisaikolojia, matatizo ya kimwili, au mabadiliko ya kihomoni. Makala haya yanachambua vyanzo vikuu vya maumivu hayo na kutoa ukweli wa kisayansi (Fact Check) ili kukusaidia kujua hatua za kuchukua.
Soma Zaidi...Njia za kuondokana na fangasi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Soma Zaidi...