Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n
Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende.
1.Njia ya kwanza kabisa ni kutibu Ugonjwa huu mara tu unapoonekana.
Matibabu ni njia mojawapo ya pekee kuliko zote na wakati wa matibabu ni lazima kuachana na kujamiiana na pia wapenzi wote wawili wanapaswa kutibiwa au kama ni wanafamilia wanapaswa kutibiwa wote kwa sababu unapotibu mmoja unakuwa unafanya kazi bure, hivyo matibabu kwa wapenzi ni kitu cha lazima.
2. Dawa ambazo zinapaswa kutumika ni dawa inayoitwa benzathrine penicillin ambayo utolewa kwa dozi moja,au mtu kama ana mzio au aleji na benzathrine penicillin anaweza kutumia doxycycline gramu mia moja ambayo utumika mara mbili kwa siku dawa hii uenda mpaka siku kumi na tano.
3. Pia na dawa ya Erythromycin inaweza kutumika hasa kwa Mama wajawazito , nayo hii utumika kama kuna mtu mwenye mzio au aleji na dawa ya benzathrine penicillin na doxycycline,kwa hiyo hii ni nzuri hasa kwa wajawazito.
4. Kama Ugonjwa huu wa kaswende una mwaka zaidi ya mmoja daima tumia benzathrine penicillin G 2.4 MU kupitia kwenye nyama au kwa kitaalamu huitwa intramuscular kwa wiki tatu.
5. Baada ya kufahamu Ugonjwa huu wa kaswende ni vizuri kabisa kutumia matibabu kama tulivyoona ila matibabu haya yanapaswa kutumika kwa kuongozwa na wataalamu wa afya, usitumike matibabu haya kiholela kwa sababu unaweza kupata matatizo mbalimbali, kwa mfano kama una aleji na dawa fulani ukitumia na uko mazingira ya nyumbani ni shida na unaweza kuleta matatizo mbalimbali kwa hiyo ni vizuri kutumia wataalamu wa afya.
6. Vilevile tunapaswa kutoa elimu kwa umma au jamii nzima kama kuna kuongeza kwa Ugonjwa huu kwa sababu kwa wajawazito unaleta shida kubwa ambayo ni pamoja na kujifungua mtoto mfu au mtoto kuzaliwa akiwa na tatizo la macho, kwa hiyo matibabu ni lazima na yapo na Ugonjwa huu unatibika. Na tupunguze kuendekeza ugonjwa huu daima juwa na mpenzi mmoja na wa maisha hali huu utapunguza kuendelea kuwepo kwa janga hili.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 web hosting 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 ai web app 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
je..! naweza kuambukizwa fangasi kwa kujamiiana na mtu mwenye fangasi?
Je ukifanya mapenz na mtu mweny aina hi ya fangasi na akawa anayo maambukizi ya ukimwi.
Soma Zaidi...Dalili na ishara za anemia ya minyoo
Posti hii inshusiana na dalili za anemia ya minyoo
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa UTI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ugonjwa wa UTI
Soma Zaidi...Maradhi ya Ini na dalili zake, na vipi utajikinga nayo
MAGONJWA YA INI NA DALILIZAKE, NA KUKABILIANA NAYO Ini ni katika viungo vikuu katika mwili wa binadamu.
Soma Zaidi...Namna ya kujikinga na VVU/UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza namna mbalimbali za kujikinga na VVU/UKIMWI
Soma Zaidi...Je daktari hizo dalili zamwanzo za HIV hazioneshi kama mwili kupungua
Dalili za HIV zina utofauti na dalili za UKIMWI. Kwani HIV huwezakuonyesha dalili wiki ya pili hadi ya sita baada ya kuathirika kisha zinapotea, lakini dalili za UKIMWI huwezakutokea baada ya miaka 5 hadi 10.
Soma Zaidi...