Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n
1.Njia ya kwanza kabisa ni kutibu Ugonjwa huu mara tu unapoonekana.
Matibabu ni njia mojawapo ya pekee kuliko zote na wakati wa matibabu ni lazima kuachana na kujamiiana na pia wapenzi wote wawili wanapaswa kutibiwa au kama ni wanafamilia wanapaswa kutibiwa wote kwa sababu unapotibu mmoja unakuwa unafanya kazi bure, hivyo matibabu kwa wapenzi ni kitu cha lazima.
2. Dawa ambazo zinapaswa kutumika ni dawa inayoitwa benzathrine penicillin ambayo utolewa kwa dozi moja,au mtu kama ana mzio au aleji na benzathrine penicillin anaweza kutumia doxycycline gramu mia moja ambayo utumika mara mbili kwa siku dawa hii uenda mpaka siku kumi na tano.
3. Pia na dawa ya Erythromycin inaweza kutumika hasa kwa Mama wajawazito , nayo hii utumika kama kuna mtu mwenye mzio au aleji na dawa ya benzathrine penicillin na doxycycline,kwa hiyo hii ni nzuri hasa kwa wajawazito.
4. Kama Ugonjwa huu wa kaswende una mwaka zaidi ya mmoja daima tumia benzathrine penicillin G 2.4 MU kupitia kwenye nyama au kwa kitaalamu huitwa intramuscular kwa wiki tatu.
5. Baada ya kufahamu Ugonjwa huu wa kaswende ni vizuri kabisa kutumia matibabu kama tulivyoona ila matibabu haya yanapaswa kutumika kwa kuongozwa na wataalamu wa afya, usitumike matibabu haya kiholela kwa sababu unaweza kupata matatizo mbalimbali, kwa mfano kama una aleji na dawa fulani ukitumia na uko mazingira ya nyumbani ni shida na unaweza kuleta matatizo mbalimbali kwa hiyo ni vizuri kutumia wataalamu wa afya.
6. Vilevile tunapaswa kutoa elimu kwa umma au jamii nzima kama kuna kuongeza kwa Ugonjwa huu kwa sababu kwa wajawazito unaleta shida kubwa ambayo ni pamoja na kujifungua mtoto mfu au mtoto kuzaliwa akiwa na tatizo la macho, kwa hiyo matibabu ni lazima na yapo na Ugonjwa huu unatibika. Na tupunguze kuendekeza ugonjwa huu daima juwa na mpenzi mmoja na wa maisha hali huu utapunguza kuendelea kuwepo kwa janga hili.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Post hii inahusu magonjwa yasiyo ya kuambukizwa,haya ni magonjwa ambayo hayawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda mwingine
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kichaa cha mbwa,au kwa kitaalamu huitwa rabies, utokea pale mtu anapongatwa na mnyama ambaye ni jamii ya mtu au mbwa mwenyewe
Soma Zaidi...Post hii inahusu dalili za mtu Mwenye ugonjwa wa kisukari, dalili hizi zinaweza kujitokeza Moja kwa Moja mtu akagundua kuwa ana Ugonjwa wa kisukari.zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kisukari.
Soma Zaidi...Hawa huweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenda maeneo mengine nyeti sana ya mwili.
Soma Zaidi...Mbu ni katika wadudu ambao husababisja vifo vya maelfu kila mwaka, na mamilioni ya watu wanaathirika na maradhi yaletwayo na mbu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mtu mwenye kiungulia,ni tiba ambayo mtu anapaswa kutumia kama ana tatizo la kiungulia
Soma Zaidi...AINA ZA MINYOO Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa.
Soma Zaidi...je na wewe ni mmoja katika wenye maumivu ya tumbo upande mmoja?. Basi post hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako.
Soma Zaidi...