Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n
1.Njia ya kwanza kabisa ni kutibu Ugonjwa huu mara tu unapoonekana.
Matibabu ni njia mojawapo ya pekee kuliko zote na wakati wa matibabu ni lazima kuachana na kujamiiana na pia wapenzi wote wawili wanapaswa kutibiwa au kama ni wanafamilia wanapaswa kutibiwa wote kwa sababu unapotibu mmoja unakuwa unafanya kazi bure, hivyo matibabu kwa wapenzi ni kitu cha lazima.
2. Dawa ambazo zinapaswa kutumika ni dawa inayoitwa benzathrine penicillin ambayo utolewa kwa dozi moja,au mtu kama ana mzio au aleji na benzathrine penicillin anaweza kutumia doxycycline gramu mia moja ambayo utumika mara mbili kwa siku dawa hii uenda mpaka siku kumi na tano.
3. Pia na dawa ya Erythromycin inaweza kutumika hasa kwa Mama wajawazito , nayo hii utumika kama kuna mtu mwenye mzio au aleji na dawa ya benzathrine penicillin na doxycycline,kwa hiyo hii ni nzuri hasa kwa wajawazito.
4. Kama Ugonjwa huu wa kaswende una mwaka zaidi ya mmoja daima tumia benzathrine penicillin G 2.4 MU kupitia kwenye nyama au kwa kitaalamu huitwa intramuscular kwa wiki tatu.
5. Baada ya kufahamu Ugonjwa huu wa kaswende ni vizuri kabisa kutumia matibabu kama tulivyoona ila matibabu haya yanapaswa kutumika kwa kuongozwa na wataalamu wa afya, usitumike matibabu haya kiholela kwa sababu unaweza kupata matatizo mbalimbali, kwa mfano kama una aleji na dawa fulani ukitumia na uko mazingira ya nyumbani ni shida na unaweza kuleta matatizo mbalimbali kwa hiyo ni vizuri kutumia wataalamu wa afya.
6. Vilevile tunapaswa kutoa elimu kwa umma au jamii nzima kama kuna kuongeza kwa Ugonjwa huu kwa sababu kwa wajawazito unaleta shida kubwa ambayo ni pamoja na kujifungua mtoto mfu au mtoto kuzaliwa akiwa na tatizo la macho, kwa hiyo matibabu ni lazima na yapo na Ugonjwa huu unatibika. Na tupunguze kuendekeza ugonjwa huu daima juwa na mpenzi mmoja na wa maisha hali huu utapunguza kuendelea kuwepo kwa janga hili.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya ugonjwa wa vericose veini, ni visababishi mbalimbali ambavyo utokea kwenye mtindo wa maisha kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Afya ya tumbo ni ishara tosha ya umadhibuti wa afya ya mtu. Maradhi mengi wanayouguwa watu chanzo kile mti anachokula. Yapo maradhi sugu kama saratani ambayo husababishwa pia na vyakula. Post hii itakwenda kujibu swalo la muulizaji kuhusu maumivu ya tumbo
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia kuaribika kwa figo, hizi ni njia zinazotumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuaribika kwa figo na hasa wale ambao hawajapata tatizo hili wazitumie ili tuone kama tutaweza kupunguza tatizo hili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu sababu za mwanamke kuumwa tumbo chini ya kitovu, ni tatizo ambalo limewapata wanawake wengi na pengine sababu ni vigumu kupata au pengine zinapatikana lakini kwa kuchelewa hali ambayo usababisha madhara mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za maambukizi kwenye nephroni, ni vitu vinavyosababisha mabukizi kwenye nephroni.
Soma Zaidi...Kipindupindu ni ugonjwa wa bakteria ambao kawaida huenezwa kupitia maji machafu. Kipindupindu husababisha Kuhara na Upungufu wa maji mwilini.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo dalili zake na namna ya kumsaidia mgonjwa mwenye tatizo hilo.
Soma Zaidi...Post yetu ya Leo inaenda kutufundisha kuhusiana na uvimbe wa korodani moja au ambayo kitaalamu huitwa EPIDIDYMITIS. EPIDIDYMITIS ni ugonjwa unaoathiri mfumo wa kiume wa uzazi. Epididymis ni mrija (tube) uliyoko nyuma ya korodani ambayo mbegu za kiume
Soma Zaidi...Je unasumbuliwa na tatizo la kukosa nguvu, kuchoka ama kuhisi viungi vinelegea. Endelea na post hii.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ugonjwa wa UTI
Soma Zaidi...