Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n
Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende.
1.Njia ya kwanza kabisa ni kutibu Ugonjwa huu mara tu unapoonekana.
Matibabu ni njia mojawapo ya pekee kuliko zote na wakati wa matibabu ni lazima kuachana na kujamiiana na pia wapenzi wote wawili wanapaswa kutibiwa au kama ni wanafamilia wanapaswa kutibiwa wote kwa sababu unapotibu mmoja unakuwa unafanya kazi bure, hivyo matibabu kwa wapenzi ni kitu cha lazima.
2. Dawa ambazo zinapaswa kutumika ni dawa inayoitwa benzathrine penicillin ambayo utolewa kwa dozi moja,au mtu kama ana mzio au aleji na benzathrine penicillin anaweza kutumia doxycycline gramu mia moja ambayo utumika mara mbili kwa siku dawa hii uenda mpaka siku kumi na tano.
3. Pia na dawa ya Erythromycin inaweza kutumika hasa kwa Mama wajawazito , nayo hii utumika kama kuna mtu mwenye mzio au aleji na dawa ya benzathrine penicillin na doxycycline,kwa hiyo hii ni nzuri hasa kwa wajawazito.
4. Kama Ugonjwa huu wa kaswende una mwaka zaidi ya mmoja daima tumia benzathrine penicillin G 2.4 MU kupitia kwenye nyama au kwa kitaalamu huitwa intramuscular kwa wiki tatu.
5. Baada ya kufahamu Ugonjwa huu wa kaswende ni vizuri kabisa kutumia matibabu kama tulivyoona ila matibabu haya yanapaswa kutumika kwa kuongozwa na wataalamu wa afya, usitumike matibabu haya kiholela kwa sababu unaweza kupata matatizo mbalimbali, kwa mfano kama una aleji na dawa fulani ukitumia na uko mazingira ya nyumbani ni shida na unaweza kuleta matatizo mbalimbali kwa hiyo ni vizuri kutumia wataalamu wa afya.
6. Vilevile tunapaswa kutoa elimu kwa umma au jamii nzima kama kuna kuongeza kwa Ugonjwa huu kwa sababu kwa wajawazito unaleta shida kubwa ambayo ni pamoja na kujifungua mtoto mfu au mtoto kuzaliwa akiwa na tatizo la macho, kwa hiyo matibabu ni lazima na yapo na Ugonjwa huu unatibika. Na tupunguze kuendekeza ugonjwa huu daima juwa na mpenzi mmoja na wa maisha hali huu utapunguza kuendelea kuwepo kwa janga hili.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π2 web hosting π3 Kitabu cha Afya π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Kitau cha Fiqh π6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Dalili za Minyoo kwa Watoto
βMinyoo ni tatizo la kawaida kwa watoto ambalo linaweza kuathiri ukuaji na afya zao kwa ujumla. Makala haya yataeleza dalili za kawaida za maambukizi ya minyoo, ukweli muhimu kuhusu tiba yake, na umuhimu wa usafi katika kuzuia tatizo hili.
Soma Zaidi...Vyakula Bora kwa Mtoto Anayekua
βLishe sahihi ni msingi mkuu wa ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili. Makala haya yataangazia vyakula muhimu vinavyopaswa kuwemo katika mlo wa mtoto, jinsi ya kuandaa mlo kamili, na ukweli wa kisayansi kuhusu virutubisho vinavyohitajika katika kila hatua ya ukuaji.
Soma Zaidi...Upele wa vipele (Shingles): Dalili na matibabu.
Upele wa vipele (Shingles), unaojulikana kitaalamu kama Herpes Zoster, ni ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kirusi kilekile kinachosababisha tetekuwanga (Chickenpox). Baada ya mtu kupona tetekuwanga, kirusi hicho hubaki kimejificha katika mfumo wa neva kwa miaka mingi. Kinapochochewa na kupungua kwa kinga ya mwili, uzee, au msongo wa mawazo, kirusi hujitokeza tena kama upele wa vipele. Makala haya yanaelezea dalili zake na jinsi ya kupata matibabu ya haraka.
Soma Zaidi...YAMINYOO NA ATHARI ZAO KIAF
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa degedege na dalili zake
Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo
Soma Zaidi...