Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n
1.Njia ya kwanza kabisa ni kutibu Ugonjwa huu mara tu unapoonekana.
Matibabu ni njia mojawapo ya pekee kuliko zote na wakati wa matibabu ni lazima kuachana na kujamiiana na pia wapenzi wote wawili wanapaswa kutibiwa au kama ni wanafamilia wanapaswa kutibiwa wote kwa sababu unapotibu mmoja unakuwa unafanya kazi bure, hivyo matibabu kwa wapenzi ni kitu cha lazima.
2. Dawa ambazo zinapaswa kutumika ni dawa inayoitwa benzathrine penicillin ambayo utolewa kwa dozi moja,au mtu kama ana mzio au aleji na benzathrine penicillin anaweza kutumia doxycycline gramu mia moja ambayo utumika mara mbili kwa siku dawa hii uenda mpaka siku kumi na tano.
3. Pia na dawa ya Erythromycin inaweza kutumika hasa kwa Mama wajawazito , nayo hii utumika kama kuna mtu mwenye mzio au aleji na dawa ya benzathrine penicillin na doxycycline,kwa hiyo hii ni nzuri hasa kwa wajawazito.
4. Kama Ugonjwa huu wa kaswende una mwaka zaidi ya mmoja daima tumia benzathrine penicillin G 2.4 MU kupitia kwenye nyama au kwa kitaalamu huitwa intramuscular kwa wiki tatu.
5. Baada ya kufahamu Ugonjwa huu wa kaswende ni vizuri kabisa kutumia matibabu kama tulivyoona ila matibabu haya yanapaswa kutumika kwa kuongozwa na wataalamu wa afya, usitumike matibabu haya kiholela kwa sababu unaweza kupata matatizo mbalimbali, kwa mfano kama una aleji na dawa fulani ukitumia na uko mazingira ya nyumbani ni shida na unaweza kuleta matatizo mbalimbali kwa hiyo ni vizuri kutumia wataalamu wa afya.
6. Vilevile tunapaswa kutoa elimu kwa umma au jamii nzima kama kuna kuongeza kwa Ugonjwa huu kwa sababu kwa wajawazito unaleta shida kubwa ambayo ni pamoja na kujifungua mtoto mfu au mtoto kuzaliwa akiwa na tatizo la macho, kwa hiyo matibabu ni lazima na yapo na Ugonjwa huu unatibika. Na tupunguze kuendekeza ugonjwa huu daima juwa na mpenzi mmoja na wa maisha hali huu utapunguza kuendelea kuwepo kwa janga hili.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Pepopunda ni ugonjwa hatari wa kutishia maisha unaosababishwa na sumu inayojulikana Kama tetanospasmin inayotolewa kwenye majeraha yaliyoambukizwa. Bakteria ya pepopunda huingia kwenye mwili wa mtoto mchanga kupitia kisiki cha kitovu ambacho kimekatwa na
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa upungufu wa Adrenali ni ugonjwa ambao hutokea wakati mwili wako hutoa kiasi cha kutosha cha homoni fulani zinazozalishwa na tezi zako za adrenali. ugonjwa huu hutokea katika makundi yote ya umri na huathiri
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo VVU huambukizwa
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi jinsi magonjwa yanavyosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya watu walio hatarini kupata fangasi
Soma Zaidi...Post hii inahusu Zaidi dalili za kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu, ni dalili ambazo zinaweza kujitokeza Kwa mgonjwa,Kwa hiyo baada ya kuona dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospital mara moja Kwa ajili ya matibabu.
Soma Zaidi...Anemia ya upungufu wa vitamini ni ukosefu wa seli nyekundu za damu zenye afya unaosababishwa na kiasi kidogo cha vitamini fulani kuliko kawaida.
Soma Zaidi...