Post hii inahusu Zaidi dalili za kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu, ni dalili ambazo zinaweza kujitokeza Kwa mgonjwa,Kwa hiyo baada ya kuona dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospital mara moja Kwa ajili ya matibabu.
Dalili ambazo ujionyesha Kwa mgonjwa mweye usaha kwenye mapafu.
1. Mgonjwa anaanza kukohoa na pia makohozi uambatana na harufu mbaya pamoja na kuwa na rangi nyeusi, vile vile mgonjwa anatoa harufu mbaya. Haya utokea Kwa sababu ya kuwepo Kwa maambukizi kwenye mapafu .Kwa hiyo mgonjwa akiona dalili kama hizi ni lazima kupata matibabu mara moja ili kuweza kuepuka madhara mengine Zaidi kwenye mfumo wa hewa.
2. Vile vile mgonjwa anaweza kutapika damu hasa sehemu zenye usaha zinapopasuka na kuelekea kwenye mfumo mzima wa upumuaji usababisha mgonjwa kuanza kutapika,Kwa hiyo mara nyingi matapishi hayo uambatana na rangi nyeusi ambayo utoka kwenye mapafu.
3. Pia mgonjwa anaweza kuwa na homa za mara Kwa mara,kutetemeka na kuhisi baridi nyingi,kutokwa na jasho wakati wa usiku,kupumua vibaya na kuwepo na maumivu kwenye mapafu au kwenye kifua hayo yote utokea Kwa sababu ya kuwepo Kwa maambukizi kwenye mapafu.
4. Wakati wa kuangalia mgonjwa Kwa kutumia vifaa mbali mbali unaweza kusikia sauti mbaya pindi mgonjwa anapopumua na Kwa wakati mwingine sauti inakuwa kama vile ya kukoroma ni Kwa sababu ya kuwepo Kwa usaha kwenye pamoja na maambukizi kwenye mapafu.
5. Kwa wakati mwingine mgonjwa anaanza kupumua Kwa shida kubwa au utasikia analalamika kwamba hewa haitoshi ni Kwa sababu ya kutokuwepo Kwa mpangilio mzuri wa mfumo wa upumuaji Kwa sababu ya kuwepo Kwa maambukizi kwenye mapafu.
6. Kwa hiyo tunapaswa kupata tiba mara moja tunapopatwa na tatizo kama hili la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu ili kuokoa maisha ya wagonjwa Kwa sababu hali hii ni hatari.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inazungumzia sababu zinazopelekea kuumwa na kifua.
Soma Zaidi...Saratani ya Utumbo ni Saratani ya utumbo mpana (koloni), sehemu ya chini ya mfumo wako wa usagaji chakula. Kwa pamoja, mara nyingi hujulikana kama Saratani ya utumbo mpana. Visa vingi vya Saratani ya utumbo mpana huanza
Soma Zaidi...Je unapata dalili zisizoeleweka ni ni za mimba ama laa. Hapa nitakujuza hali baadhi ya wanawake zinazowatokea.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa vericose veini, hili ni tatizo ambalo utokea katika mzunguko wa damu hasa kwenye miguu.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.
Soma Zaidi...Makala hii inakwenda kukufahamishavkuhusu saratani yavkibifu cha mkojo.
Soma Zaidi...Swali hili limeulizwa na mdau mmoja. Kuwa endapo mtu atafanya ngono zembe na akapata virusi je ataweza kuambukiza.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mfumo wa mwili ambao huhusika na kusafirisha damu ,virutubisho na takamwili.mfumo huu unajumuisha damu,mishipa ya damu na moyo.moyo husukuma damu kupitia mishipa ya damu na kufika maeneo yote ya mwili.
Soma Zaidi...Homa hii inapatikana katika maeneo ya bonde la ufa barani Afrika na na Mashariki ya kati.
Soma Zaidi...