Sasa UKIMWI unatokeaje?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo UKIMWI hutokea
SASA UKIMWI UNATOKEAJE?
Seli ndio matofali yaliyojengea miili yetu. Ndani ya miili yetu kuna aina nyingi za seli, na seli za damu. Ndani ya damu pekee kuna aina zisizopunguwa tatu za seli. Kuna seli hai nyekundu, nyeupe na seli sahani. Kila seli kati ya hizi ina kazi zake. Sasa hii seli hai nyeupe yenyewe ndio inakazi ya kupigana na vijidudu vya maradhi vinapoingia katika miili yetu. Vijidudu hivyo vinaweza kuwa bakteria, virusi ama fangasi. Seli hizi ndizo ambazo ambazo huitwa CD4.
Sasa virusi vya VVU vinapoingia mwilini vinaanza kuharibi hizi seli ambazo zinalinda mwili. Kawaida mtu anaweza kuwa na seli hizi 500 mapa 1500 katika kipimo kimoja. Sasa VVU vinaanza kuziharibu hizi na kupunguza idadi yake. Na kila seli hizi zikipunguwa ndipo mfumo wa kinga unavyoendelea kuharibika na ndivyo maradhi yanapozidi kupata nafasi ya kuingia mwilini.
Sasa endapo zimeharibiwa na kufika idadi ya 200 katika kipimo kimoja hapa mtu huyu ataambiwa ana Upungufu wa Kinga Mwilini yaani UKIMWI. Katika hatuwa hii mtu atakuwa akinyemelewa na maradhi nyemelezi kama fangasi, kifuwa kikuu, na mengineyo.
Endapo mgonjwa atatumia ARV mapema anaweza kukaa miaka mimngi sana bila ya kufikia hatuwa hii. Kuna umuhimu wa kutumia ARV mapema, sababu hizo ni kama:-
1.Kupungua maambukizi ya VVU
2.Kulinda afya ya mtu
3.Kupunguza uharibifu wa seli
4.Kulinda mwili dhidi ya maradhi nyemelezi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitau cha Fiqh π2 web hosting π3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 Kitabu cha Afya π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Baadhi ya maradhi yanayosababishwa na hali za maisha
Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya maradhi yanayosababishwa na hali za maisha
Soma Zaidi...Ukweli Kuhusu Kupima HIV Nyumbani
Katika jitihada za kuongeza kasi ya upimaji wa VVU, njia ya kupima nyumbani (HIV Self-Testing) imekuwa suluhisho muhimu linalotoa faragha na urahisi. Makala hii inachambua ukweli kuhusu jinsi vipimo hivi vinavyofanya kazi, usahihi wake, na umuhimu wa kuelewa matokeo unayopata ili kuhakikisha afya yako inalindwa kwa njia sahihi.
Soma Zaidi...βDalili za Mwanzoni za Virusi vya UKIMWI
βMakala haya yanatoa mwongozo kuhusu dalili za awali zinazoweza kujitokeza baada ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI (HIV). Tunasisitiza kuwa dalili hizi si mahususi kwa HIV pekee na njia pekee ya kujua hali yako ya afya ni kufanya vipimo vya maabara.
Soma Zaidi...Je mtu akapima ukimwi na kile kipimo kidogo .je kina usahihi au la ..na pia kama inaonyesha mistari miwili.
Hivi umeshawahi kuwazakuwa jekipimo cha HIV ni sahihi kwa kiasi gani. Unadhani huwa kinakoseaga kutoa majibu?
Soma Zaidi...Aina za saratani ( cancer)
Posti hii inahusu zaidi Aina za kansa, Kansa ni Aina ya ugonjwa unaosababishwa na kuzaliana kwa seli ambazo sio za kawaida.
Soma Zaidi...Ni zipi dalili za Ukimwi na ni zipi dalili za VVU
Ijuwe historia ya VVu, Dalili zake, tiba na vipimo vyake pia njia za kueneza VVU na UKIMWI
Soma Zaidi...