picha

Sasa UKIMWI unatokeaje?

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo UKIMWI hutokea

SASA UKIMWI UNATOKEAJE?

Seli ndio matofali yaliyojengea miili yetu. Ndani ya miili yetu kuna aina nyingi za seli, na seli za damu. Ndani ya damu pekee kuna aina zisizopunguwa tatu za seli. Kuna seli hai nyekundu, nyeupe na seli sahani. Kila seli kati ya hizi ina kazi zake. Sasa hii seli hai nyeupe yenyewe ndio inakazi ya kupigana na vijidudu vya maradhi vinapoingia katika miili yetu. Vijidudu hivyo vinaweza kuwa bakteria, virusi ama fangasi. Seli hizi ndizo ambazo ambazo huitwa CD4.

 

Sasa virusi vya VVU vinapoingia mwilini vinaanza kuharibi hizi seli ambazo zinalinda mwili. Kawaida mtu anaweza kuwa na seli hizi 500 mapa 1500 katika kipimo kimoja. Sasa VVU vinaanza kuziharibu hizi na kupunguza idadi yake. Na kila seli hizi zikipunguwa ndipo mfumo wa kinga unavyoendelea kuharibika na ndivyo maradhi yanapozidi kupata nafasi ya kuingia mwilini.

 

Sasa endapo zimeharibiwa na kufika idadi ya 200 katika kipimo kimoja hapa mtu huyu ataambiwa ana Upungufu wa Kinga Mwilini yaani UKIMWI. Katika hatuwa hii mtu atakuwa akinyemelewa na maradhi nyemelezi kama fangasi, kifuwa kikuu, na mengineyo.

 

Endapo mgonjwa atatumia ARV mapema anaweza kukaa miaka mimngi sana bila ya kufikia hatuwa hii. Kuna umuhimu wa kutumia ARV mapema, sababu hizo ni kama:-

1.Kupungua maambukizi ya VVU

2.Kulinda afya ya mtu

3.Kupunguza uharibifu wa seli

4.Kulinda mwili dhidi ya maradhi nyemelezi

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2353

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 ai web app     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Vimelea vya tumbo (Minyoo): Dalili za kuwepo mwilini na tiba.

Vimelea vya tumbo, maarufu kama minyoo, ni tatizo la kiafya linaloathiri watu wa rika zote, likichangia kwa kiasi kikubwa utapiamlo na upungufu wa damu. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu jinsi ya kutambua dalili za maambukizi, taratibu za utambuzi hospitalini, na mikakati madhubuti ya tiba na kinga ili kudumisha afya ya mfumo wa mmeng'enyo wa chakula.

Soma Zaidi...
Unene kupita kiasi wakati wa ujauzito: Athari zake.

Uzito wa mwili wakati wa ujauzito una nafasi muhimu sana katika afya ya mama na mtoto. Ingawa ni kawaida kupata uzito wakati wa kulea mimba, unene uliopitiliza (Obesity) kabla au wakati wa ujauzito huleta changamoto za kiafya zinazoweza kuwa hatari. Makala hii inaangazia athari za unene uliokithiri na jinsi unavyoweza kuathiri mchakato wa ujauzito na uzazi kwa ujumla.

Soma Zaidi...
Dalili za jeraha kali kwenye ubongo

Posti hii inahusu zaidi dalili za jeraha kali kwenye ubongo, ni majeraha ambayo utokea kwenye ubongo pale ambapo mtu anapata ajali au amepigwa na kitu chochote kigumu kichwni, zifuatazo ni dalili za jeraha kali kwenye ubongo

Soma Zaidi...
Mzio (aleji) na Dalili zake

Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisonono

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisonono, ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Neisseria gonococcal.

Soma Zaidi...
Kukosa usingizi (Insomnia): Sababu na njia za kutatua.

Kukosa usingizi, au insomnia, ni tatizo linalomfanya mtu ashindwe kupata usingizi wa kutosha au usingizi wenye ubora, licha ya kuwa na fursa ya kupumzika. Hali hii haileti uchovu tu, bali pia huathiri umakini kazini, hali ya hisia, na afya ya jumla ya mwili. Makala haya yanachunguza visababishi vikuu vya ukosefu wa usingizi na kutoa mbinu za kisayansi unazoweza kutumia ili kurejesha utaratibu wako wa kulala

Soma Zaidi...