picha

Sasa UKIMWI unatokeaje?

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo UKIMWI hutokea

SASA UKIMWI UNATOKEAJE?

Seli ndio matofali yaliyojengea miili yetu. Ndani ya miili yetu kuna aina nyingi za seli, na seli za damu. Ndani ya damu pekee kuna aina zisizopunguwa tatu za seli. Kuna seli hai nyekundu, nyeupe na seli sahani. Kila seli kati ya hizi ina kazi zake. Sasa hii seli hai nyeupe yenyewe ndio inakazi ya kupigana na vijidudu vya maradhi vinapoingia katika miili yetu. Vijidudu hivyo vinaweza kuwa bakteria, virusi ama fangasi. Seli hizi ndizo ambazo ambazo huitwa CD4.

 

Sasa virusi vya VVU vinapoingia mwilini vinaanza kuharibi hizi seli ambazo zinalinda mwili. Kawaida mtu anaweza kuwa na seli hizi 500 mapa 1500 katika kipimo kimoja. Sasa VVU vinaanza kuziharibu hizi na kupunguza idadi yake. Na kila seli hizi zikipunguwa ndipo mfumo wa kinga unavyoendelea kuharibika na ndivyo maradhi yanapozidi kupata nafasi ya kuingia mwilini.

 

Sasa endapo zimeharibiwa na kufika idadi ya 200 katika kipimo kimoja hapa mtu huyu ataambiwa ana Upungufu wa Kinga Mwilini yaani UKIMWI. Katika hatuwa hii mtu atakuwa akinyemelewa na maradhi nyemelezi kama fangasi, kifuwa kikuu, na mengineyo.

 

Endapo mgonjwa atatumia ARV mapema anaweza kukaa miaka mimngi sana bila ya kufikia hatuwa hii. Kuna umuhimu wa kutumia ARV mapema, sababu hizo ni kama:-

1.Kupungua maambukizi ya VVU

2.Kulinda afya ya mtu

3.Kupunguza uharibifu wa seli

4.Kulinda mwili dhidi ya maradhi nyemelezi

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2347

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 web hosting     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Kuchelewa kwa hedhi: Sababu 10 zinazoweza kuwa nje ya mimba.

Kuchelewa kwa hedhi ni hali inayowatokea wanawake wengi katika hatua mbalimbali za maisha yao. Ingawa ujauzito ndiyo sababu inayofikiriwa mara ya kwanza, kuna sababu nyingine nyingi za kibiolojia, kisaikolojia, na kiafya zinazoweza kuvuruga mzunguko wa hedhi. Makala hii inaangazia sababu 10 kuu zinazopelekea mzunguko wako kutokwenda kama ulivyozoea.

Soma Zaidi...
Dalili za Kisukari kwa Watu Wazima

Makala hii inaelezea dalili za ugonjwa wa kisukari kwa watu wazima, sababu zake na namna ya kujikinga.

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni

Post hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni, ni njia zinazotumika kuzuia maambukizi kwenye nephroni

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kushoto

Zijuwe sababu kuu zinazokufanya ukahisi maumivu makali ya tumbo kwa chini upande wa kushoto

Soma Zaidi...
Kucha langu LA mguu linang'ooka...nini chaweza kuwa tatizo

Je na wewe unasumbukiwa na kunggoka jwa kucha. Tatizo limekunaza una muda gani nalo?

Soma Zaidi...
Dalili za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...