Twahara

FIQH 1.

Twahara

FIQH
1.TWAHARA
Twahara ni neno la kiarabu lenye maana ya usafi au unadhifu. Na neno hili kisheria ni kuondoa yale yanayomzuilia mtu kuswali ambayo ni katika hdathi na najisi, kwa kutumia maji au vinavyosimama badala ya kukosekana kwa maji kama udongo.

Kuondoa najisi ni jambo la wajibu pindi mtu anapokumbuka na akiwa na uwezo wa kufanya hivyo. Kama aliposema Allah kumwambia Mtume (s.a.s): “na nguozako uzitwaharishe” (surat muzammil: 4). Na Mtume صليالله عليه وسلم amesema “haikubaliwi swala (iliyoswaliwa ) bila ya udhu”.

Kuwa twahara tofauti na kuwa ni jambo lililohimizwa sana kwenye uislamu hata Mtume صليالله عليه وسلم akasema: “uislamu ni usafi” ila pia kuna faida nyingi sana tunazipata kwa kutekeleza jambo hili:

1.Twahara ni sharti katika kuswihi kwa sala. Hadithi iliyopokelewa kutoka kwa Mtume صليالله عليه وسلم amesema:”haikubaliwi swala ya mtu aliyehuduthi (aliyejamba) mpaka atawadhe” (Bukhari na Muslim)

2.Allah amewasifia sana watu ambao wanakuwa twahara. Amesema Allah “hakika Allah anawapenda wenye kutubia na anawapenda wenye kuwa twahara” (Surat baqara aya 222).

3.Kuwa twahara ni sababu ya kutokuadhibiwa kaburini. Ni kuwa watu ambao hawajikingi na najisi kama mkojo na hawajitwaharishi wataadhibiwa makaburini. Imesimuliwa hadithi na Ibn Abas kuwa Mtume صليالله عليه وسلم alipita kwenye makaburi mawili kisha akasema : “hakika watu hawa (waliozikwa hapa ) wanadhibiwa, na si kwa makosa makubwa bali kwa hakika huyu mmoja alikuwa hajisafishi anapokojoa.….” (Ibn Majah N Abu daud na isnad ya hadithi ni sahihi)

Aina za twahara.
Basi tambua kuwa twahara ip katika makundi makuu mawili ambayo ni:

1.twahara haqiqiya: nayo ni ni kujitwaharisha na khabathi yaani najisi na inaweza kuwa kwenye mavazi au mwili.

2.Twahara hukmiyah: nayo ni kujitwaharisha na hadathi na hii inahusiana na mwili tu na aina hii imegawanyika katika makundi matatu ambayo ni:-
A)Twahara kubwa; ambayo ni kuonga (josho la kisheria)
B)Twahara ndogo; nayo ni kutawadha yaani udhu
C)Twahara iliyo badala ya aina mbili zilizotangulia nayo ni kutayamam, yaani kujitwaharisha kwa kutumia udongo.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2524

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Nafasi ya serikali katika ugawaji

Serikali ina nafasi katika kufanya mgawanyiko katika uchumi.

Soma Zaidi...
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Funga za Sunnah na umuhimu wake

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Uzuri wa Benki za kiislamu

Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine?

Soma Zaidi...
Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu

- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.

Soma Zaidi...
Mambo yanayotenguwa udhu

Post hiibinakwenda kukufundisha mambo ambayo yanaharibu udhu.

Soma Zaidi...
Mambo yanayodhaniwa kuwa yanaharibu funga lakini hayaharibu

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...