Twahara

FIQH 1.

Twahara

FIQH
1.TWAHARA
Twahara ni neno la kiarabu lenye maana ya usafi au unadhifu. Na neno hili kisheria ni kuondoa yale yanayomzuilia mtu kuswali ambayo ni katika hdathi na najisi, kwa kutumia maji au vinavyosimama badala ya kukosekana kwa maji kama udongo.

Kuondoa najisi ni jambo la wajibu pindi mtu anapokumbuka na akiwa na uwezo wa kufanya hivyo. Kama aliposema Allah kumwambia Mtume (s.a.s): “na nguozako uzitwaharishe” (surat muzammil: 4). Na Mtume صليالله عليه وسلم amesema “haikubaliwi swala (iliyoswaliwa ) bila ya udhu”.

Kuwa twahara tofauti na kuwa ni jambo lililohimizwa sana kwenye uislamu hata Mtume صليالله عليه وسلم akasema: “uislamu ni usafi” ila pia kuna faida nyingi sana tunazipata kwa kutekeleza jambo hili:

1.Twahara ni sharti katika kuswihi kwa sala. Hadithi iliyopokelewa kutoka kwa Mtume صليالله عليه وسلم amesema:”haikubaliwi swala ya mtu aliyehuduthi (aliyejamba) mpaka atawadhe” (Bukhari na Muslim)

2.Allah amewasifia sana watu ambao wanakuwa twahara. Amesema Allah “hakika Allah anawapenda wenye kutubia na anawapenda wenye kuwa twahara” (Surat baqara aya 222).

3.Kuwa twahara ni sababu ya kutokuadhibiwa kaburini. Ni kuwa watu ambao hawajikingi na najisi kama mkojo na hawajitwaharishi wataadhibiwa makaburini. Imesimuliwa hadithi na Ibn Abas kuwa Mtume صليالله عليه وسلم alipita kwenye makaburi mawili kisha akasema : “hakika watu hawa (waliozikwa hapa ) wanadhibiwa, na si kwa makosa makubwa bali kwa hakika huyu mmoja alikuwa hajisafishi anapokojoa.….” (Ibn Majah N Abu daud na isnad ya hadithi ni sahihi)

Aina za twahara.
Basi tambua kuwa twahara ip katika makundi makuu mawili ambayo ni:

1.twahara haqiqiya: nayo ni ni kujitwaharisha na khabathi yaani najisi na inaweza kuwa kwenye mavazi au mwili.

2.Twahara hukmiyah: nayo ni kujitwaharisha na hadathi na hii inahusiana na mwili tu na aina hii imegawanyika katika makundi matatu ambayo ni:-
A)Twahara kubwa; ambayo ni kuonga (josho la kisheria)
B)Twahara ndogo; nayo ni kutawadha yaani udhu
C)Twahara iliyo badala ya aina mbili zilizotangulia nayo ni kutayamam, yaani kujitwaharisha kwa kutumia udongo.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2435

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Nini maana ya kusimamisha swala

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria.

Soma Zaidi...
Tofauti ya uchumi wa kiislamu na uchumi wa kikafiri

Uchumi wa kiislamu unatofautiana sana na uchumi wa kikafiri. Hapa utajifunza tofauti hizo.

Soma Zaidi...
Kumswalia maiti, masharti ya swala ya maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kumuandaa maiti baada ya kufa

Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Lengo la kusimamisha swala kwa mwanadamu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la kusimamisha swala.

Soma Zaidi...
Zoezi la 6 kusimamisha swala

Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala.

Soma Zaidi...