Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu

Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi.

Yaliyo Sunnah kuyafanya Siku ya Idd

Ni sunnah siku ya Idd kukoga, kuvalia nguo nzuri kuliko zote ulizo nazo na kupaka uturi (manukato) kwa wanaume. Pia ni sunnah siku ya Idd kupika vyakula na kuandaa vinywaji vizuri zaidi kuliko siku za kawaida. kwa wafugaji na wale wenye wasaa, ni sunah kumchinja mnyama aliye bora zaidi kuliko wengine katika mifugo yake kama tunavyojifunza katika hadith ifuatayo:

 


Amehadithia Hasan Asibbit (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) ametuamrisha katika Idd m bili kuvaa vizuri zaidi kadri tuw ezavyo, tupake uturi bora zaidi kuliko wote tulionao, na tuchinje wanyama wenye thamani zaidi kuliko wote tu lion a o. (A l-Ha kim).

 


Ni sunnah vile vile kuwakaribisha ndugu, marafiki, majirani, maskini, yatima na wengine wasiojiweza. Ni sunnah kuwatembelea ndugu, marafiki, majirani na wagonjwa. Ni sunnah vile vile kupeana zawadi.

 


Tahadhari Katika Siku ya Idd
Waislamu hawana budi kukumbuka kuwa sherehe za Kiislamu, makusudio yake na muundo wake, ni tofauti kabisa na sherehe zisizokuwa za Kiislamu. Sherehe za Kiislamu ni kilele cha kuonyesha shukrani zetu kwa Allah (s.w) kwa kutujaalia na kutuwezesha kutimiza wajibu wetu kwake katika kutekeleza ibada kubwa na nzito kama vile kufunga Ramadhani na kukamilisha Ibada ya Hija. Hivyo, sherehe hizi ni lazima ziambatane na kumshukuru, kumtukuza, kumtaja na kumkumbuka sana Allah (s.w).

 


Tunafahamu kuwa katika sherehe zisizokuwa za Kiislamu au zisizosherehekewa kwa mtazamo wa Kiislamu, ndio wakati ambao Allah (s.w) husahauliwa kuliko nyakati zote na ndio wakati ambao shetani hukumbukwa na kuadhimishwa kuliko nyakati zote. Kwa maana nyingine katika sherehe hizi watu hujiingiza kwa furaha na kicheko katika kumuasi Allah (s.w). Kutokana na uzoefu wetu sherehe hizi zimeambatana na ulevi, ngoma na mziki, mchanganyiko wa wanaume na wanawake, uzinifu na mengineyo kama haya.

 


Waislamu wanatahadharishwa sana wajiepushe na sherehe za namna hii, kwani zitawafanya wawe ni wenye kukufuru badala ya kuwa wenye kumshukuru Allah (s.w), kwa mafanikio hayo wanayo yasherehekea. Katika sherehe hizi za Idd Muislamu anatakiwa achukue hadhari kubwa katika kuchunga mipaka ya sherehe, kwani kumuasi Allah (s.w) katika siku ya Idd ni kosa kubwa sana mbele ya Allah kuliko kumuasi Allah (s.w) wakati mwingine, Mtume (s.a.w) amesema:
“Kumuasi Mwenyezi Mungu siku ya Idd ni sawa na kumuasi Mwenyezi Mungu siku ya Kiyama ”.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1596

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Mafungu ya mirathi katika uislamu

Mafungu ya urithi yaliyotajwa katika haya sita yafutayo:1.

Soma Zaidi...
Nini kifanyike baada ya mazishi ya kiislamu

Huu ni utaratibu unaotakiwa kufanyika baada ya kuzika.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na ria na masimbulizi

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Je manii ni twahara au najisi?

Post hii itakwenda kukufundisha hukumu ya manii kuwa ni twahara ama ni najis

Soma Zaidi...
Namna lengo la zakat linavyofikiwa

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Utaijuwaje kama swala yako imekubalika

Hapa tunakwenda kuona jinsi ya kuzitathmini swala zetu.

Soma Zaidi...
Msimamo wa uislamu juu ya utumwa

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...