image

Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu

Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi.

Yaliyo Sunnah kuyafanya Siku ya Idd

Ni sunnah siku ya Idd kukoga, kuvalia nguo nzuri kuliko zote ulizo nazo na kupaka uturi (manukato) kwa wanaume. Pia ni sunnah siku ya Idd kupika vyakula na kuandaa vinywaji vizuri zaidi kuliko siku za kawaida. kwa wafugaji na wale wenye wasaa, ni sunah kumchinja mnyama aliye bora zaidi kuliko wengine katika mifugo yake kama tunavyojifunza katika hadith ifuatayo:

 


Amehadithia Hasan Asibbit (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) ametuamrisha katika Idd m bili kuvaa vizuri zaidi kadri tuw ezavyo, tupake uturi bora zaidi kuliko wote tulionao, na tuchinje wanyama wenye thamani zaidi kuliko wote tu lion a o. (A l-Ha kim).

 


Ni sunnah vile vile kuwakaribisha ndugu, marafiki, majirani, maskini, yatima na wengine wasiojiweza. Ni sunnah kuwatembelea ndugu, marafiki, majirani na wagonjwa. Ni sunnah vile vile kupeana zawadi.

 


Tahadhari Katika Siku ya Idd
Waislamu hawana budi kukumbuka kuwa sherehe za Kiislamu, makusudio yake na muundo wake, ni tofauti kabisa na sherehe zisizokuwa za Kiislamu. Sherehe za Kiislamu ni kilele cha kuonyesha shukrani zetu kwa Allah (s.w) kwa kutujaalia na kutuwezesha kutimiza wajibu wetu kwake katika kutekeleza ibada kubwa na nzito kama vile kufunga Ramadhani na kukamilisha Ibada ya Hija. Hivyo, sherehe hizi ni lazima ziambatane na kumshukuru, kumtukuza, kumtaja na kumkumbuka sana Allah (s.w).

 


Tunafahamu kuwa katika sherehe zisizokuwa za Kiislamu au zisizosherehekewa kwa mtazamo wa Kiislamu, ndio wakati ambao Allah (s.w) husahauliwa kuliko nyakati zote na ndio wakati ambao shetani hukumbukwa na kuadhimishwa kuliko nyakati zote. Kwa maana nyingine katika sherehe hizi watu hujiingiza kwa furaha na kicheko katika kumuasi Allah (s.w). Kutokana na uzoefu wetu sherehe hizi zimeambatana na ulevi, ngoma na mziki, mchanganyiko wa wanaume na wanawake, uzinifu na mengineyo kama haya.

 


Waislamu wanatahadharishwa sana wajiepushe na sherehe za namna hii, kwani zitawafanya wawe ni wenye kukufuru badala ya kuwa wenye kumshukuru Allah (s.w), kwa mafanikio hayo wanayo yasherehekea. Katika sherehe hizi za Idd Muislamu anatakiwa achukue hadhari kubwa katika kuchunga mipaka ya sherehe, kwani kumuasi Allah (s.w) katika siku ya Idd ni kosa kubwa sana mbele ya Allah kuliko kumuasi Allah (s.w) wakati mwingine, Mtume (s.a.w) amesema:
“Kumuasi Mwenyezi Mungu siku ya Idd ni sawa na kumuasi Mwenyezi Mungu siku ya Kiyama ”.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 851


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Kufunga Mwezi wa ramadhani kisheria
Soma Zaidi...

namna ya kuswali 6
Lugha ya Swala Lugha ya swala,kuanzia kwenye Takbira ya kuhirimia Swala mpaka kumalizia swala kwa Salaam, ni Kiarabu. Soma Zaidi...

Taratibu za ndoa ya kiislamu, hatua kwa hatua
Soma Zaidi...

Fiqh.
Kipengele hichi tutajifunza chimbuko la fiqh na maana ya figh. Soma Zaidi...

Utaratibu wa kutekeleza hija, matendo hatua kwa hatua, pamoja na kusherehekea sikuku baada ya hija
4. Soma Zaidi...

nyakati za swala
3. Soma Zaidi...

Masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat
Nguzo za uislamu, masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

kanunu na sheria za biashara katika islamu
Soma Zaidi...

Warithi wasio na mafungu maalumu katika uislamu
Hapa utajifunza watu wanaorithi bila ya kuwekewa mafungu maalumu au viwango maalumi vya kurithi. Soma Zaidi...

Zoezi la nne mada ya fiqh.
Maswali mbalimbali kuhusu fiqh. Soma Zaidi...

Maswali juu ya haki na uadilifu katika uislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...