Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu

Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi.

Yaliyo Sunnah kuyafanya Siku ya Idd

Ni sunnah siku ya Idd kukoga, kuvalia nguo nzuri kuliko zote ulizo nazo na kupaka uturi (manukato) kwa wanaume. Pia ni sunnah siku ya Idd kupika vyakula na kuandaa vinywaji vizuri zaidi kuliko siku za kawaida. kwa wafugaji na wale wenye wasaa, ni sunah kumchinja mnyama aliye bora zaidi kuliko wengine katika mifugo yake kama tunavyojifunza katika hadith ifuatayo:

 


Amehadithia Hasan Asibbit (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) ametuamrisha katika Idd m bili kuvaa vizuri zaidi kadri tuw ezavyo, tupake uturi bora zaidi kuliko wote tulionao, na tuchinje wanyama wenye thamani zaidi kuliko wote tu lion a o. (A l-Ha kim).

 


Ni sunnah vile vile kuwakaribisha ndugu, marafiki, majirani, maskini, yatima na wengine wasiojiweza. Ni sunnah kuwatembelea ndugu, marafiki, majirani na wagonjwa. Ni sunnah vile vile kupeana zawadi.

 


Tahadhari Katika Siku ya Idd
Waislamu hawana budi kukumbuka kuwa sherehe za Kiislamu, makusudio yake na muundo wake, ni tofauti kabisa na sherehe zisizokuwa za Kiislamu. Sherehe za Kiislamu ni kilele cha kuonyesha shukrani zetu kwa Allah (s.w) kwa kutujaalia na kutuwezesha kutimiza wajibu wetu kwake katika kutekeleza ibada kubwa na nzito kama vile kufunga Ramadhani na kukamilisha Ibada ya Hija. Hivyo, sherehe hizi ni lazima ziambatane na kumshukuru, kumtukuza, kumtaja na kumkumbuka sana Allah (s.w).

 


Tunafahamu kuwa katika sherehe zisizokuwa za Kiislamu au zisizosherehekewa kwa mtazamo wa Kiislamu, ndio wakati ambao Allah (s.w) husahauliwa kuliko nyakati zote na ndio wakati ambao shetani hukumbukwa na kuadhimishwa kuliko nyakati zote. Kwa maana nyingine katika sherehe hizi watu hujiingiza kwa furaha na kicheko katika kumuasi Allah (s.w). Kutokana na uzoefu wetu sherehe hizi zimeambatana na ulevi, ngoma na mziki, mchanganyiko wa wanaume na wanawake, uzinifu na mengineyo kama haya.

 


Waislamu wanatahadharishwa sana wajiepushe na sherehe za namna hii, kwani zitawafanya wawe ni wenye kukufuru badala ya kuwa wenye kumshukuru Allah (s.w), kwa mafanikio hayo wanayo yasherehekea. Katika sherehe hizi za Idd Muislamu anatakiwa achukue hadhari kubwa katika kuchunga mipaka ya sherehe, kwani kumuasi Allah (s.w) katika siku ya Idd ni kosa kubwa sana mbele ya Allah kuliko kumuasi Allah (s.w) wakati mwingine, Mtume (s.a.w) amesema:
“Kumuasi Mwenyezi Mungu siku ya Idd ni sawa na kumuasi Mwenyezi Mungu siku ya Kiyama ”.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1501

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Kusimamisha Swala na kuamrisha mema

Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii.

Soma Zaidi...
NI KWA NINI TUNASWALI?, NI UPI UMUHIMU WA KUSWALI NA NI ZIPI FADHILA ZA KUSWALI

Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.

Soma Zaidi...
Kuzika-namna ya kuzika hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
HUKUMU YA KUUWA MTU (KUMWAGA DAMU) KWENYE UISLAMU

عَنْ ابْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم "لَا يَحِلُّ دَمُ امْرِئٍ مُسْلِمٍ [ يشهد أن ل?...

Soma Zaidi...
Kujitwaharisha kutokana na najisi

Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi.

Soma Zaidi...
Ni upi umuhimu wa kufunga katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kufunga kiroho, kiafya na kijamii.

Soma Zaidi...