picha

Tatizo la tezi koo

Posti hii inahusu zaidi tatizo la tezi koo, ni tatizo ambalo uwapata watu mbalimbali ambapo Usababisha koo kuvimba na mgonjwa huwa na maumivu mbalimbali na pengine mgonjwa upata kikohozi kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo.

Tatizo la tezi kwenye koo.

1. Kama tulivyokwisha tangulia kusema kwamba tatizo hili uwapata watu mbalimbali, na hasa uwapata sana watu wanaoishi sehemu zenye mikusanyiko mbalimbali na kuna wataalam mbalimbali ambazo wameweza kutoa takwimu kwamba ugonjwa huu uwapata watu wa kwenye machimbo kwa sababu ya matumizi ya vyakula vya kwenye mifuko ya nailoni ila sio hawa tu na wengine wanaweza kupata kwa sababu zifuatazo.

 

2. Kuna sababu ambazo utokea kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ya virus, kwa kawaida tunafahamu kwamba ugonjwa ambao usababishwa na virus ni vigumu kupona inawezekana ugonjwa ukaisha wenyewe au kwa wakati mwingine tunatibu dalili kama vile homa , kikohozi na miwasho kwenye koo kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.

 

3. Sababu nyingine ni pamoja na Maambukizi ya bakteria, kwa kawaida pengine kuvimba au Maambukizi kwenye koo usababishwa na kuwepo kwa Maambukizi ya bakteria, kwa kawaida kama Maambukizi yametokana na bakteria uponyaji ni rahisi kwa hiyo pamoja na kutibu dalili kama vile kutuliza homa, kutuliza maumivu, miwasho na kikohozi vile vile na antibiotics zinaweza kutumika na mtu akaomba kabisa na kuendelea na shughuli zake za kawaida.

 

4. Sababu nyingine ni pamoja na upungufu wa vitamini mbalimbali kwenye mwili.

Kwa kawaida tunafahamu matumizi ya vitamini kwenye mwili kwa hiyo kama vitamini vinakosa usababisha kuwepo kwa magonjwa kwenye koo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kutumia mboga mboga za majani,matunda na matumizi ya mlo kamili kwa kufanya hivyo tunaweza kuepuka kuwepo kwa maambukizi kwenye koo.

 

5. Upungufu wa kinga mwilini.

Kwa kawaida watu wenye upungufu wa kinga mwilini ushambuliaji na magonjwa mbalimbali kwa hiyo ni vizuri kabisa kutumia vidonge au dawa ili kuweza kuongeza kinga na kuzuia magonjwa kama ya koo.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2678

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

DALILI ZA MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kuwashwa, kutapika damu, moyo kuumwa, ukuaji hafifu, udhaifu na kuchoka

DALILI ZA MINYOO Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote.

Soma Zaidi...
ugonjwa wa Malaria dalili zake na chanzo chake.

Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa coma

Coma ni hali ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu ambayo inaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali Jeraha la Kichwa, Kiharusi, Uvimbe kwenye ubongo, ulevi wa dawa za kulevya au pombe, au hata ugonjwa wa msingi,

Soma Zaidi...
Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.

Posti hii inahusu kiungulia kwa wanawake wajawazito na tiba yake, ni ugonjwa au hali inayowapata wajawazito walio wengi kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa ,kwa kawaida Ugonjwa huu utokea kuanzia kwenye wiki ya pili mpaka mwaka mmoja na hapo Ugonjwa unakuwa bado haujaonesha Dalili na Dalili zikishaonekana ni vigumu kutibika.

Soma Zaidi...
Dalili za UKIMWI huonekana baada ya muda gani

Hapa utajifunza muda mabao dalili za VVU na UKIMWI huonekana, na kwa muda gani mgonjwa ataishi na UKIMWI bila ya kutumia ARV

Soma Zaidi...