Dalili za VVU/UKIMWI Ni zipi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI

DALILI ZA VVU NA UKIMWI NI ZIPI?

Dalili za VVU na UKIMWI hutofautiana, kulingana na awamu ya maambukizo, muda kutoka maambukizo yalipotokea pia afya ya mtu kabla ya maambukizo.

Hatua ya kwanza ya maambukizi (Primary infection)

 

Watu wengi walioambukizwa na VVU hupata ugonjwa unaofanana na Homa ndani ya mwezi mmoja au miwili baada ya virusi kuingia mwilini. Hivyo kutengeneza dalili za awali za VVU na UKIMWI. Dalili hizi si lazima zimpate kila mtu, wapp wengine hawazipati kabisa. Sana dalili hizi hutokea wiki mbili toka kupata maambukizi mpaka wiki nne kisha hupotea. Kwa baadhi ya watu zinaweza kuanzia wiki ya kwanza, na wengine kuishia wiki ya sita. Dalili hizo ni:-

 

 

1.Kupatwa na homa.

2.Maumivu ya kichwa yasiyo na sababu

3.Maumivu ya misuli

4.Kuota upele

5.Kupatwa na baridi ama kuhisi baridi.

6.Kukauka na koo ama kupatwa na vidonda kooni.

7.Kupatwa na Vidonda vya kinywa au sehemu za siri

8.Kuvimba kwa Tezi za limfu kwenye mapaja, makwapa na haswa kwenye shingo

9.Mwili kuwa na Maumivu bila ya sababu maalumu.

10.Kutokwa na Jasho la usiku

11.Kuharisha

 

Ingawa katika kipindi hiki kiwango cha virusi sio rahisi kuviona kwa vipimo vya kawaida vinavyotumika kupima, lakini ni kuwa katika kipindi hiki kiwango cha virusi ni kingi sana kwenye damu, na muathirika anaweza kumuambukiza mwengine kwa urahisi sana. Baada ya wiki sita dalili hizi hupotea na hazitajirudia tena. Hapa virusi vitatulia ndani ya mwili kwa miaka mingi bila ya kuonyesha dalili yeyote ile, huku vukiendelea kuharibu kinga ya mwili kidogokidogo.

 

 

Hatuwa ya pili Toka kuambukizwa.

Kama tulivyoona dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza. Sasa hutokea kwa baadhi ya watu kuwa tezi za limfu zisivimbe wakati wa hatuwa ya kwanza, ila zikavimba katika hatuwa hii ya pili. Tofauti na hili hakuna dalili nyingine maalumu ya VVU katika hatuwa hii ya pili. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10. Kwa watu wengi ni kati ya miaka 4 mpaka 10 ila wengine mara chache hutokea ikawa chini ya hapo.

 

 

Baada ya maambukizi ya Awali

Hiki ni kipindi cha miaka kadhaa baada ya kuambukizwa. Katika wakati huu hakuna dalili ya VVU inayoonekana. Hata hivyo kadri iaka inavyosonga mbele ndivyo seli zinavyozidi kudhoofu. Wakati virusi vinaendelea kuongezeka na kuharibu seli za kinga, unaweza kupata maambukizo kidogo au ishara sugu na dalili kama vile:

 

 

1.Homa

2.Uchovu

3.Node za mtoki, kwapa, na shingo kuvimba – na hii ndio mara nyingi moja ya ishara za kwanza za maambukizo ya VVU

4.Kuhara

5.Kupungua uzito

6.Kikohozi

7.Kupumua kwa pumzi

 

 

Kuendelea kwa UKIMWI

Ikiwa hautapata matibabu maalumu ya ART na kutumia ARV mapema iwezekanavyo kwa ajili ya kuthibiti maambukizo yako ya VVU, ugonjwa huendelea hadi kufikia kuwa UKIMWI kwa takriban miaka 10. Wakati huu ukiwa na UKIMWI unakua, mfumo wako wa kinga umeharibiwa sana, na hivyo kukufanya uweze kuambukizwa na magonjwa nyemelezi – Mgonjwa nyemelezi ni magonjwa ambayo hayangemsumbua mtu aliye na kinga nzuri.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2256

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Mzio (aleji) na Dalili zake

Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Dalili za malaria

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya dalili za maralia

Soma Zaidi...
Athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa wajawazito

Post inahusu zaidi athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa wajawazito au ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri.ugonjwa huu uleta madhara kwa wajawazito kama tutakavyoona

Soma Zaidi...
Presha ya kushuka/hypotension

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka/ hypotension

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa upungufu wa Adrenali.

Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa upungufu wa Adrenali ni ugonjwa ambao hutokea wakati mwili wako hutoa kiasi cha kutosha cha homoni fulani zinazozalishwa na tezi zako za adrenali. ugonjwa huu hutokea katika makundi yote ya umri na huathiri

Soma Zaidi...
Hatua za Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.

Posti hii inahusu zaidi hatua mbalimbali za Ugonjwa wa Ukimwi, kawaida Ugonjwa huu huwa na hatua kuu nne ila kila hatua huwa na sifa zake kwa hiyo tunapaswa kujua hatua za Ugonjwa huu na kujaribu kuzuia maambukizi yasisambae kabisa.

Soma Zaidi...
Dalili za sukari kupungua mwilini (Hypoglycemia)

sukari kupungua mwilini (Hypoglycemia) huhusishwa kwa kawaida na matibabu ya Kisukari. Hata hivyo, hali mbalimbali, nyingi zikiwa nadra, zinaweza kusababisha sukari ya chini ya damu kwa watu wasio na Kisukari. Kama vile Homa, Hy

Soma Zaidi...
Namna ya kujikinga na ugonjwa wa madonda ya koo

Post hii inahusu zaidi namna ya kuzuia ugonjwa wa madonda ya koo,ni njia ambazo usaidia katika kujikinga na ugonjwa wa madonda ya koo.

Soma Zaidi...
Njia za kuondokana na fangasi

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.

Soma Zaidi...
Dalili za mkojo mchafu na rangi za mkojo na mkojo mchafu

Hapautajifunza rangi kuu za mkojo na dalili zako kiafya, mkojo mchafu na dalili zake

Soma Zaidi...