Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI
DALILI ZA VVU NA UKIMWI NI ZIPI?
Dalili za VVU na UKIMWI hutofautiana, kulingana na awamu ya maambukizo, muda kutoka maambukizo yalipotokea pia afya ya mtu kabla ya maambukizo.
Hatua ya kwanza ya maambukizi (Primary infection)
Watu wengi walioambukizwa na VVU hupata ugonjwa unaofanana na Homa ndani ya mwezi mmoja au miwili baada ya virusi kuingia mwilini. Hivyo kutengeneza dalili za awali za VVU na UKIMWI. Dalili hizi si lazima zimpate kila mtu, wapp wengine hawazipati kabisa. Sana dalili hizi hutokea wiki mbili toka kupata maambukizi mpaka wiki nne kisha hupotea. Kwa baadhi ya watu zinaweza kuanzia wiki ya kwanza, na wengine kuishia wiki ya sita. Dalili hizo ni:-
1.Kupatwa na homa.
2.Maumivu ya kichwa yasiyo na sababu
3.Maumivu ya misuli
4.Kuota upele
5.Kupatwa na baridi ama kuhisi baridi.
6.Kukauka na koo ama kupatwa na vidonda kooni.
7.Kupatwa na Vidonda vya kinywa au sehemu za siri
8.Kuvimba kwa Tezi za limfu kwenye mapaja, makwapa na haswa kwenye shingo
9.Mwili kuwa na Maumivu bila ya sababu maalumu.
10.Kutokwa na Jasho la usiku
11.Kuharisha
Ingawa katika kipindi hiki kiwango cha virusi sio rahisi kuviona kwa vipimo vya kawaida vinavyotumika kupima, lakini ni kuwa katika kipindi hiki kiwango cha virusi ni kingi sana kwenye damu, na muathirika anaweza kumuambukiza mwengine kwa urahisi sana. Baada ya wiki sita dalili hizi hupotea na hazitajirudia tena. Hapa virusi vitatulia ndani ya mwili kwa miaka mingi bila ya kuonyesha dalili yeyote ile, huku vukiendelea kuharibu kinga ya mwili kidogokidogo.
Hatuwa ya pili Toka kuambukizwa.
Kama tulivyoona dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza. Sasa hutokea kwa baadhi ya watu kuwa tezi za limfu zisivimbe wakati wa hatuwa ya kwanza, ila zikavimba katika hatuwa hii ya pili. Tofauti na hili hakuna dalili nyingine maalumu ya VVU katika hatuwa hii ya pili. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10. Kwa watu wengi ni kati ya miaka 4 mpaka 10 ila wengine mara chache hutokea ikawa chini ya hapo.
Baada ya maambukizi ya Awali
Hiki ni kipindi cha miaka kadhaa baada ya kuambukizwa. Katika wakati huu hakuna dalili ya VVU inayoonekana. Hata hivyo kadri iaka inavyosonga mbele ndivyo seli zinavyozidi kudhoofu. Wakati virusi vinaendelea kuongezeka na kuharibu seli za kinga, unaweza kupata maambukizo kidogo au ishara sugu na dalili kama vile:
1.Homa
2.Uchovu
3.Node za mtoki, kwapa, na shingo kuvimba – na hii ndio mara nyingi moja ya ishara za kwanza za maambukizo ya VVU
4.Kuhara
5.Kupungua uzito
6.Kikohozi
7.Kupumua kwa pumzi
Kuendelea kwa UKIMWI
Ikiwa hautapata matibabu maalumu ya ART na kutumia ARV mapema iwezekanavyo kwa ajili ya kuthibiti maambukizo yako ya VVU, ugonjwa huendelea hadi kufikia kuwa UKIMWI kwa takriban miaka 10. Wakati huu ukiwa na UKIMWI unakua, mfumo wako wa kinga umeharibiwa sana, na hivyo kukufanya uweze kuambukizwa na magonjwa nyemelezi – Mgonjwa nyemelezi ni magonjwa ambayo hayangemsumbua mtu aliye na kinga nzuri.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg
Soma Zaidi...Katika makala hii utakwenda kuzijuwa baadhi ya dalili za ukimwi ama HIV kwa mwanamke
Soma Zaidi...Posti hii utokea huduma ya kwanza kwa mtu aliye na shida ya kushindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo,
Soma Zaidi...Mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi hujitokeza sehemu yenye jeraha pia huonyesha wekundu wenye upele,Uvimbe na malengelenge.
Soma Zaidi...Hepatitis C ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoshambulia ini na kusababisha kuvimba. Watu wengi walioambukizwa na virusi vya Hepatitis C (HCV) hawana dalili. Kwa kweli, watu wengi hawajui kuwa wana maambukizi ya Hepatitis C hadi uharibifu wa ini
Soma Zaidi...Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini.unasababishwa na virusi ambavyo hutokea kwa mtu mwingine kwa njia mbalimbali
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili zinazoweza kujitokeza baada ya sehemu ya kupeleka taarifa kwenye ubongo imearibika, kwa hiyo mambo yafuatayo yakijitokeza utajua wazi kuwa kuna matatizo kwenye mfumo wa kupeleka taarifa kwenye ubongo.
Soma Zaidi...