Dalili za VVU/UKIMWI Ni zipi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI

DALILI ZA VVU NA UKIMWI NI ZIPI?

Dalili za VVU na UKIMWI hutofautiana, kulingana na awamu ya maambukizo, muda kutoka maambukizo yalipotokea pia afya ya mtu kabla ya maambukizo.

Hatua ya kwanza ya maambukizi (Primary infection)

 

Watu wengi walioambukizwa na VVU hupata ugonjwa unaofanana na Homa ndani ya mwezi mmoja au miwili baada ya virusi kuingia mwilini. Hivyo kutengeneza dalili za awali za VVU na UKIMWI. Dalili hizi si lazima zimpate kila mtu, wapp wengine hawazipati kabisa. Sana dalili hizi hutokea wiki mbili toka kupata maambukizi mpaka wiki nne kisha hupotea. Kwa baadhi ya watu zinaweza kuanzia wiki ya kwanza, na wengine kuishia wiki ya sita. Dalili hizo ni:-

 

 

1.Kupatwa na homa.

2.Maumivu ya kichwa yasiyo na sababu

3.Maumivu ya misuli

4.Kuota upele

5.Kupatwa na baridi ama kuhisi baridi.

6.Kukauka na koo ama kupatwa na vidonda kooni.

7.Kupatwa na Vidonda vya kinywa au sehemu za siri

8.Kuvimba kwa Tezi za limfu kwenye mapaja, makwapa na haswa kwenye shingo

9.Mwili kuwa na Maumivu bila ya sababu maalumu.

10.Kutokwa na Jasho la usiku

11.Kuharisha

 

Ingawa katika kipindi hiki kiwango cha virusi sio rahisi kuviona kwa vipimo vya kawaida vinavyotumika kupima, lakini ni kuwa katika kipindi hiki kiwango cha virusi ni kingi sana kwenye damu, na muathirika anaweza kumuambukiza mwengine kwa urahisi sana. Baada ya wiki sita dalili hizi hupotea na hazitajirudia tena. Hapa virusi vitatulia ndani ya mwili kwa miaka mingi bila ya kuonyesha dalili yeyote ile, huku vukiendelea kuharibu kinga ya mwili kidogokidogo.

 

 

Hatuwa ya pili Toka kuambukizwa.

Kama tulivyoona dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza. Sasa hutokea kwa baadhi ya watu kuwa tezi za limfu zisivimbe wakati wa hatuwa ya kwanza, ila zikavimba katika hatuwa hii ya pili. Tofauti na hili hakuna dalili nyingine maalumu ya VVU katika hatuwa hii ya pili. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10. Kwa watu wengi ni kati ya miaka 4 mpaka 10 ila wengine mara chache hutokea ikawa chini ya hapo.

 

 

Baada ya maambukizi ya Awali

Hiki ni kipindi cha miaka kadhaa baada ya kuambukizwa. Katika wakati huu hakuna dalili ya VVU inayoonekana. Hata hivyo kadri iaka inavyosonga mbele ndivyo seli zinavyozidi kudhoofu. Wakati virusi vinaendelea kuongezeka na kuharibu seli za kinga, unaweza kupata maambukizo kidogo au ishara sugu na dalili kama vile:

 

 

1.Homa

2.Uchovu

3.Node za mtoki, kwapa, na shingo kuvimba – na hii ndio mara nyingi moja ya ishara za kwanza za maambukizo ya VVU

4.Kuhara

5.Kupungua uzito

6.Kikohozi

7.Kupumua kwa pumzi

 

 

Kuendelea kwa UKIMWI

Ikiwa hautapata matibabu maalumu ya ART na kutumia ARV mapema iwezekanavyo kwa ajili ya kuthibiti maambukizo yako ya VVU, ugonjwa huendelea hadi kufikia kuwa UKIMWI kwa takriban miaka 10. Wakati huu ukiwa na UKIMWI unakua, mfumo wako wa kinga umeharibiwa sana, na hivyo kukufanya uweze kuambukizwa na magonjwa nyemelezi – Mgonjwa nyemelezi ni magonjwa ambayo hayangemsumbua mtu aliye na kinga nzuri.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2004

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Dalili za kuvunjika kwa nyonga

Kuvunjika kwa nyonga ni jeraha kubwa, na matatizo ambayo yanaweza kuhatarisha maisha. Hatari ya kupasuka kwa nyonga huongezeka na umri.

Soma Zaidi...
Je wiki 1 dalili zinaonyesha za maambukizi ya ukimwi na wiki 3 vipimo vinaweza kuonyesha Kama umeasilika

Muda ambao maambukizi ya virusi vya ukimwi kuonyesha dalili unaweza kutofautiana kutika mtu hadi mwingine.

Soma Zaidi...
Namna ya kuishi na vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuishi na vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUGUNDUA VIDONDA VYA TUMBO

NAMNA YA KUGUNDUA VIDONDA VYA TUMBO Ili kugundua vidonda, daktari wako anaweza kwanza kuchukua historia ya matibabu na kufanya uchunguzi wa mwili.

Soma Zaidi...
Sababu kuu za maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, Tumbo la ngiri na chango

Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu, na tumbo la ngiri kwa wanaume, na tumbo la chango kwa wanawake

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa gonoria (gonorrhea)

UGONJWA WA GONORIA NA DALILI ZAKE (GONORRHEA)Gonoria (gonorrhea) ni katika maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya ngono.

Soma Zaidi...
Namna ya kumsaidia mtoto mwenye UTI

Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.

Soma Zaidi...
Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?

kuwashwa na koo ni katika dalili za kuwa na maambukizi mwilini. Kuwa na maambukizi haimaanishi ni HIV ama UKIMWI laa hili ni neno pana. Hapa nitakujuza kwa ufupi kuhusu swali hilo la muulizaji kuwa anawashwa na koo.

Soma Zaidi...
Fahamu maambukizi ya kwenye mishipa ya Damu.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na ugonjwa ambao husababisha kuvimba kwa mishipa ya damu katika mwili wako wote. Ambao kitaalamu hujulikana Kama Behcet .

Soma Zaidi...