Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.
Posti hii inahusu kiungulia kwa wanawake wajawazito na tiba yake, ni ugonjwa au hali inayowapata wajawazito walio wengi kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito.
Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.
1. Kwanza kabisa kiungulia uwapo wanawake wajawazito wakiwa kwenye wiki kuanzia ya thelathini mpaka arobaini,hali huu utokea kwa sababu progesterone homoni inalegeza cardiac sphincter za tumboni na kusababisha acid kurudi kwenye oesophagus na kusababisha kiungulia, kwa hiyo wajawazito walipatwa na hali kama hizi hawapaswi kuogopa au kuwa na wasiwasi wajue kuwa ni kitu cha kawaida utokea na uisha tu baada ya kujifungua. Na pia wauguzi wanapaswa kuwaambia wazi wajawazito ili watambue Dalili kama hizi wakati wa ujauzito.
2. Hili kupunguza hali hii ya kiungulia wanawake wenye mimba wanapaswa kuepuka kuinama kwa mda mrefu wakati wanapokuwa wanafanya kazi zao za kila siku, kwa hiyo wanapaswa kujua hali yao kwa hiyo ni vizuri kufanya kazi wakiwa wamesimama pindi wakisikia hali ya kiungulia au wanaweza kuwekewa kiti au meza wakati wa kufanya kazi kama vile kuosha vyote na kufua wakafanya wakiwa wamesimama na pia wote waliowazunguka wanapaswa kujua hali huu na kuwasaidia akina mama wajawazito ili waweze kufanya kazi zao bila kuinama.
3. Kama hali ya kiungulia imezidi sana wajawazito wanapaswa kula chakula kidogo kidogo kwa siku ili kuepuka hali ya kupata kiungulia kwa mfano anaweza kula saa mbili, saa nne, saa sita, saa nane, saa kumi, saa kumi na mbili na kuendelea mpaka mda wa kulala, kwa kufanya hivyo anaweza kuepuka kupata kiungulia mara kwa mara, nimesema hivyo kwa sababu kuna akina mama wajawazito wanaopata kiungulia cha hali ya juu sana kuliko wengine na pia watu wa karibu wanapaswa kujua hili na kuona kuwa ni hali ya kawaida na kuendelea kumjali Mama katika kupambana na hali yake ya mda mfupi tu.
4. Pia wanawake wajawazito wanapaswa kulala wakiwa na mito ya kutosha ili kuepuka kiungulia na pia wajawazito kama hawajalala na mito ya kutosha wanaweza kuteseka sana wakati wa usiku au mda wowote wa kupumzika kwa hiyo wauguzi na wataalam wengine wa afya wanapaswa kumweleza mama huduma hii ya kutumia mito ili kupunguza kuwepo kwa kiungulia na pia watu wa karibu wa Mama mjamzito wanapaswa kuhakikisha kuwa Mama anapata mito kadiri ya uhitaji.
5. Pia hali huu ya kiungulia ikizidi hata kama ni kawaida kwa wajawazito wanaweza kwenda hospitalini, kwa maana kuna dawa ambazo utibu ugonjwa huu dawa hizi ni kama vile anti acid na sawa nyingine kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya, kwa hiyo tunapaswa kuwaambia ukweli pale hali ikizidi wajawazito wanapaswa kwenda hospitalini kupata dawa za kuwatuliza hali zao.
6. Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa wanawake wenye mimba Upata magonjwa madogo madogo kama kiungulia na wanapaswa kupata huduma za muhimu kwao kwa hiyo jamii inapaswa kuwaelewa na kuwahudumia kwa kadiri inavyowezekana na kuwa pamoja nao kwa sababu haya matatizo madogo kama kiungulia ni ya mda tu na Mama akijifungua yanapotea mara moja.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitau cha Fiqh π2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π3 ai web app π4 Bongolite - Game zone - Play free game π5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?
Dalili za mimba zinaweza kuanzia kuonekana mapema ndani ya wiki ya kwanza, japo sio rahisi nabhakuna uthibitishobwa uhakika juu ya kauli hii. Makala hii itakwebda kujibubswali la msingi la muuulizaji kama maumivu ya tumbo ni dalili ya ujauzito.
Soma Zaidi...Njia za Kuongeza Mbegu za Kiume
βUzazi wa mwanaume unategemea kwa kiasi kikubwa ubora na wingi wa mbegu za kiume. Makala haya yanalenga kutoa mwongozo wa njia za asili na mabadiliko ya mtindo wa maisha yanayoweza kusaidia kuongeza uzalishaji na kuboresha ubora wa mbegu hizo.
Soma Zaidi...Huduma kwa walio na matatizo ya asili nyingi mwilini
Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wale ambao tayari wameshakuwa na tatizo la asidi mwilini, ni njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza tatizo hili au Mgonjwa anapoendelea kupata matibabu.
Soma Zaidi...Dalili za ukosefu wa misuli.
Posti hii inahusu dalili za ukosefu wa misuli. ukosefu wa udhibiti wa misuli wakati wa harakati za hiari, kama vile kutembea au kuokota vitu. Ishara ya hali ya msingi, Ataxia inaweza kuathiri harakati, hotuba, harakati za jicho na kumeza.
Soma Zaidi...Mazoea ya utoto na athari zake kwenye afya ya akili ya mtu mzima.
βUtoto ni kipindi muhimu cha maendeleo ambapo msingi wa tabia, hisia, na utambuzi huwekwa. Makala haya yanachunguza uhusiano wa kina kati ya uzoefu wa utotoni na ustawi wa kisaikolojia katika utu uzima. Kwa kutumia mtazamo wa kitaalamu, tunachambua jinsi mifumo ya malezi inavyoathiri jinsi mtu anavyojenga mahusiano, anavyokabiliana na msongo wa mawazo, na anavyojiheshimu.
Soma Zaidi...Dalili za fangasi Mdomoni.
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za fangasi Mdomoni kwa watoto, vijana, watu wazima na mama wanaonyonyeshwa.
Soma Zaidi...