Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.
Posti hii inahusu kiungulia kwa wanawake wajawazito na tiba yake, ni ugonjwa au hali inayowapata wajawazito walio wengi kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito.
Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.
1. Kwanza kabisa kiungulia uwapo wanawake wajawazito wakiwa kwenye wiki kuanzia ya thelathini mpaka arobaini,hali huu utokea kwa sababu progesterone homoni inalegeza cardiac sphincter za tumboni na kusababisha acid kurudi kwenye oesophagus na kusababisha kiungulia, kwa hiyo wajawazito walipatwa na hali kama hizi hawapaswi kuogopa au kuwa na wasiwasi wajue kuwa ni kitu cha kawaida utokea na uisha tu baada ya kujifungua. Na pia wauguzi wanapaswa kuwaambia wazi wajawazito ili watambue Dalili kama hizi wakati wa ujauzito.
2. Hili kupunguza hali hii ya kiungulia wanawake wenye mimba wanapaswa kuepuka kuinama kwa mda mrefu wakati wanapokuwa wanafanya kazi zao za kila siku, kwa hiyo wanapaswa kujua hali yao kwa hiyo ni vizuri kufanya kazi wakiwa wamesimama pindi wakisikia hali ya kiungulia au wanaweza kuwekewa kiti au meza wakati wa kufanya kazi kama vile kuosha vyote na kufua wakafanya wakiwa wamesimama na pia wote waliowazunguka wanapaswa kujua hali huu na kuwasaidia akina mama wajawazito ili waweze kufanya kazi zao bila kuinama.
3. Kama hali ya kiungulia imezidi sana wajawazito wanapaswa kula chakula kidogo kidogo kwa siku ili kuepuka hali ya kupata kiungulia kwa mfano anaweza kula saa mbili, saa nne, saa sita, saa nane, saa kumi, saa kumi na mbili na kuendelea mpaka mda wa kulala, kwa kufanya hivyo anaweza kuepuka kupata kiungulia mara kwa mara, nimesema hivyo kwa sababu kuna akina mama wajawazito wanaopata kiungulia cha hali ya juu sana kuliko wengine na pia watu wa karibu wanapaswa kujua hili na kuona kuwa ni hali ya kawaida na kuendelea kumjali Mama katika kupambana na hali yake ya mda mfupi tu.
4. Pia wanawake wajawazito wanapaswa kulala wakiwa na mito ya kutosha ili kuepuka kiungulia na pia wajawazito kama hawajalala na mito ya kutosha wanaweza kuteseka sana wakati wa usiku au mda wowote wa kupumzika kwa hiyo wauguzi na wataalam wengine wa afya wanapaswa kumweleza mama huduma hii ya kutumia mito ili kupunguza kuwepo kwa kiungulia na pia watu wa karibu wa Mama mjamzito wanapaswa kuhakikisha kuwa Mama anapata mito kadiri ya uhitaji.
5. Pia hali huu ya kiungulia ikizidi hata kama ni kawaida kwa wajawazito wanaweza kwenda hospitalini, kwa maana kuna dawa ambazo utibu ugonjwa huu dawa hizi ni kama vile anti acid na sawa nyingine kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya, kwa hiyo tunapaswa kuwaambia ukweli pale hali ikizidi wajawazito wanapaswa kwenda hospitalini kupata dawa za kuwatuliza hali zao.
6. Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa wanawake wenye mimba Upata magonjwa madogo madogo kama kiungulia na wanapaswa kupata huduma za muhimu kwao kwa hiyo jamii inapaswa kuwaelewa na kuwahudumia kwa kadiri inavyowezekana na kuwa pamoja nao kwa sababu haya matatizo madogo kama kiungulia ni ya mda tu na Mama akijifungua yanapotea mara moja.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 ai web app 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Vimelea vya tumbo (Minyoo): Dalili za kuwepo mwilini na tiba.
Vimelea vya tumbo, maarufu kama minyoo, ni tatizo la kiafya linaloathiri watu wa rika zote, likichangia kwa kiasi kikubwa utapiamlo na upungufu wa damu. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu jinsi ya kutambua dalili za maambukizi, taratibu za utambuzi hospitalini, na mikakati madhubuti ya tiba na kinga ili kudumisha afya ya mfumo wa mmeng'enyo wa chakula.
Soma Zaidi...SABABU ZA KUTOKEA KWA VIDONDA VYA TUMBO
SABABU ZA KUTOKEA KWA VIDONDA VYA TUMBO Sababu za kawaida za vidonda vya tumbo ni maambukizo na bakteria Helicobacter pylori (H.
Soma Zaidi...Jinsi ya kutoa huduma ya kwanz akwa liyeshambuliwa na pumu
Hii ni huduma ya kwanza kwa aliyeshambuliwa na pumu katika mazingira ambayo ni mbali na kituo cha afya, na hakuna dawa.
Soma Zaidi...Sababu za maumivu wakati wa kujamiiana
​Maumivu wakati wa kujamiiana (kitaalamu dyspareunia) ni tatizo linalowasumbua wanawake wengi, ingawa mara nyingi halizungumzwi wazi kutokana na unyanyapaa au aibu. Maumivu haya yanaweza kusababishwa na sababu za kisaikolojia, matatizo ya kimwili, au mabadiliko ya kihomoni. Makala haya yanachambua vyanzo vikuu vya maumivu hayo na kutoa ukweli wa kisayansi (Fact Check) ili kukusaidia kujua hatua za kuchukua.
Soma Zaidi...Kucha langu LA mguu linang'ooka...nini chaweza kuwa tatizo
Je na wewe unasumbukiwa na kunggoka jwa kucha. Tatizo limekunaza una muda gani nalo?
Soma Zaidi...Uzito kupita kiasi (Obesity): Hatari zake kiafya.
Uzito kupita kiasi, au unene uliokithiri (obesity), si suala la mwonekano wa nje pekee, bali ni changamoto kubwa ya kiafya inayoongeza hatari ya kupata magonjwa sugu ambayo yanaweza kupunguza umri wa kuishi. Hali hii hutokea wakati kiasi cha mafuta mwilini kinapozidi kiwango cha kawaida na kuanza kuathiri utendaji kazi wa viungo muhimu. Makala haya yanaelezea hatari za kiafya zinazohusiana na uzito kupita kiasi na umuhimu wa kuchukua hatua za haraka ili kulinda afya yako.
Soma Zaidi...