Posti hii inahusu kiungulia kwa wanawake wajawazito na tiba yake, ni ugonjwa au hali inayowapata wajawazito walio wengi kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito.
Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.
1. Kwanza kabisa kiungulia uwapo wanawake wajawazito wakiwa kwenye wiki kuanzia ya thelathini mpaka arobaini,hali huu utokea kwa sababu progesterone homoni inalegeza cardiac sphincter za tumboni na kusababisha acid kurudi kwenye oesophagus na kusababisha kiungulia, kwa hiyo wajawazito walipatwa na hali kama hizi hawapaswi kuogopa au kuwa na wasiwasi wajue kuwa ni kitu cha kawaida utokea na uisha tu baada ya kujifungua. Na pia wauguzi wanapaswa kuwaambia wazi wajawazito ili watambue Dalili kama hizi wakati wa ujauzito.
2. Hili kupunguza hali hii ya kiungulia wanawake wenye mimba wanapaswa kuepuka kuinama kwa mda mrefu wakati wanapokuwa wanafanya kazi zao za kila siku, kwa hiyo wanapaswa kujua hali yao kwa hiyo ni vizuri kufanya kazi wakiwa wamesimama pindi wakisikia hali ya kiungulia au wanaweza kuwekewa kiti au meza wakati wa kufanya kazi kama vile kuosha vyote na kufua wakafanya wakiwa wamesimama na pia wote waliowazunguka wanapaswa kujua hali huu na kuwasaidia akina mama wajawazito ili waweze kufanya kazi zao bila kuinama.
3. Kama hali ya kiungulia imezidi sana wajawazito wanapaswa kula chakula kidogo kidogo kwa siku ili kuepuka hali ya kupata kiungulia kwa mfano anaweza kula saa mbili, saa nne, saa sita, saa nane, saa kumi, saa kumi na mbili na kuendelea mpaka mda wa kulala, kwa kufanya hivyo anaweza kuepuka kupata kiungulia mara kwa mara, nimesema hivyo kwa sababu kuna akina mama wajawazito wanaopata kiungulia cha hali ya juu sana kuliko wengine na pia watu wa karibu wanapaswa kujua hili na kuona kuwa ni hali ya kawaida na kuendelea kumjali Mama katika kupambana na hali yake ya mda mfupi tu.
4. Pia wanawake wajawazito wanapaswa kulala wakiwa na mito ya kutosha ili kuepuka kiungulia na pia wajawazito kama hawajalala na mito ya kutosha wanaweza kuteseka sana wakati wa usiku au mda wowote wa kupumzika kwa hiyo wauguzi na wataalam wengine wa afya wanapaswa kumweleza mama huduma hii ya kutumia mito ili kupunguza kuwepo kwa kiungulia na pia watu wa karibu wa Mama mjamzito wanapaswa kuhakikisha kuwa Mama anapata mito kadiri ya uhitaji.
5. Pia hali huu ya kiungulia ikizidi hata kama ni kawaida kwa wajawazito wanaweza kwenda hospitalini, kwa maana kuna dawa ambazo utibu ugonjwa huu dawa hizi ni kama vile anti acid na sawa nyingine kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya, kwa hiyo tunapaswa kuwaambia ukweli pale hali ikizidi wajawazito wanapaswa kwenda hospitalini kupata dawa za kuwatuliza hali zao.
6. Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa wanawake wenye mimba Upata magonjwa madogo madogo kama kiungulia na wanapaswa kupata huduma za muhimu kwao kwa hiyo jamii inapaswa kuwaelewa na kuwahudumia kwa kadiri inavyowezekana na kuwa pamoja nao kwa sababu haya matatizo madogo kama kiungulia ni ya mda tu na Mama akijifungua yanapotea mara moja.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Kama una tatizo la midomo kuchubuka na kuwa myeupe ama kuwa na vidonda. Post hii inakwenda kuangalia swala hili.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za minyoo ya tumbo ambapo minyoo hawa husababishwa na mtu kula vyakula vichafu ambavyo havijaiva vizuri au maji machafu pia au bacteria.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatua au mbinu za kupambana na ugonjwa wa UTI kwa sababu ugonjwa huu umekuwa tishio kubwa kwa sasa kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali ili kuweza kupambana na Ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Shinikizo la chini la damu (hypotension) litaonekana kuwa jambo la kujitahidi. Hata hivyo, kwa watu wengi, shinikizo la chini la damu linaweza kusababisha dalili za Kizunguzungu na kuzirai. Katika hali mbaya, shinikizo la chini la damu linawez
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za kupunguza maumivu na kazi zake, ni dawa ambazo upunguza maumivu kwenye mwili wa binadamu.
Soma Zaidi...Maumivu ya matiti yanaweza kuanzia kidogo hadi makali. Inaweza kukuathiri siku chache tu kwa mwezi, kwa mfano kabla tu ya kipindi chako, au inaweza kudumu kwa siku saba au zaidi kila mwezi. Maumivu ya matiti yanaweza kukuathiri kabla tu ya kipindi chako
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya makunfi ya watu walio hatarini kupata UTI
Soma Zaidi...Posti hii inaonyesha dalili na Mambo Hatari yanayosababisha homa ya ini Kali ya pombe.
Soma Zaidi...Kaswende ni maambukizi ya bakteria kawaida huenezwa kwa kujamiiana pia ugonjwa huu hujulikana kama syphilis. Ugonjwa huu huanza kama kidonda kisicho na maumivu kwa kawaida kwenye sehemu zako za siri, rektamu au mdomo
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...