Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.

Posti hii inahusu kiungulia kwa wanawake wajawazito na tiba yake, ni ugonjwa au hali inayowapata wajawazito walio wengi kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito.

Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.

1. Kwanza kabisa kiungulia uwapo wanawake wajawazito wakiwa kwenye wiki kuanzia ya thelathini mpaka arobaini,hali huu utokea kwa sababu progesterone homoni inalegeza cardiac sphincter za tumboni  na kusababisha acid kurudi kwenye oesophagus na kusababisha kiungulia, kwa hiyo wajawazito walipatwa na hali kama hizi hawapaswi kuogopa au kuwa na wasiwasi wajue kuwa ni kitu cha kawaida utokea na uisha tu baada ya kujifungua. Na pia wauguzi wanapaswa kuwaambia wazi wajawazito ili watambue Dalili kama hizi wakati wa ujauzito.

 

2. Hili kupunguza hali hii ya kiungulia wanawake wenye mimba wanapaswa kuepuka  kuinama kwa mda mrefu  wakati wanapokuwa wanafanya kazi zao za kila siku, kwa hiyo wanapaswa kujua hali yao kwa hiyo ni vizuri kufanya kazi wakiwa wamesimama pindi wakisikia hali ya kiungulia au wanaweza kuwekewa kiti au meza wakati wa kufanya kazi kama vile kuosha vyote na kufua wakafanya wakiwa wamesimama na pia wote waliowazunguka wanapaswa kujua hali huu na kuwasaidia akina mama wajawazito ili waweze kufanya kazi zao bila kuinama.

 

3. Kama hali ya kiungulia imezidi sana wajawazito wanapaswa kula chakula kidogo kidogo kwa siku ili kuepuka hali ya kupata kiungulia kwa mfano anaweza kula saa mbili, saa nne, saa sita, saa nane, saa kumi, saa kumi na mbili na kuendelea mpaka mda wa kulala, kwa kufanya hivyo anaweza kuepuka kupata kiungulia mara kwa mara, nimesema hivyo kwa sababu kuna akina mama wajawazito wanaopata kiungulia cha hali ya juu sana kuliko wengine na pia watu wa karibu wanapaswa kujua hili na kuona kuwa ni hali ya kawaida na kuendelea kumjali Mama katika kupambana na hali yake ya mda mfupi tu.

 

4. Pia wanawake wajawazito wanapaswa kulala wakiwa na mito ya kutosha ili kuepuka kiungulia na pia wajawazito kama hawajalala na mito ya kutosha wanaweza kuteseka sana wakati wa usiku au mda wowote wa kupumzika kwa hiyo wauguzi na wataalam wengine wa afya wanapaswa kumweleza mama huduma hii ya kutumia mito ili kupunguza kuwepo kwa kiungulia na pia watu wa karibu wa Mama mjamzito wanapaswa kuhakikisha kuwa Mama anapata mito kadiri ya uhitaji.

 

5. Pia hali huu ya kiungulia ikizidi hata kama ni kawaida kwa wajawazito wanaweza kwenda hospitalini, kwa maana kuna dawa ambazo utibu ugonjwa huu dawa hizi ni kama vile  anti acid na sawa nyingine kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya, kwa hiyo tunapaswa kuwaambia ukweli pale hali ikizidi wajawazito wanapaswa kwenda hospitalini kupata dawa za kuwatuliza hali zao.

 

6. Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa wanawake wenye mimba Upata magonjwa madogo madogo kama kiungulia na wanapaswa kupata huduma za muhimu kwao kwa hiyo jamii inapaswa kuwaelewa na kuwahudumia kwa kadiri inavyowezekana na kuwa pamoja nao kwa sababu haya matatizo madogo kama kiungulia ni ya mda tu na Mama akijifungua yanapotea mara moja.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1206

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Dalili za kisukari na njia za kuzuia kisukari

Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisakari, dalili zake,na namna ya kujikinga usipate kisukari au Kama tayari unakisukari ukijikinga madhara yanapungua au kupona kabisa.Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwa

Soma Zaidi...
Sasa UKIMWI unatokeaje?

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo UKIMWI hutokea

Soma Zaidi...
Dalili za maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za maumivu ya jino

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha kizunguzungu?

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu

Soma Zaidi...
vidonda vya tumbo, dalili zake, chanzo chake na tiba yake

Makala hii itakwenda kukupa elimu juu ya vidonda vya tumbo, nini hasa chanzo chake, vipi vinatokea ni zipi dalili zake, ni zipi njia za kujilinda dhidi ya vidonda vya tumbo. Pia tutaangalia matibabu ya kutibi vidonda vya tumbo.

Soma Zaidi...
Vyanzo vya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyanzo vya minyoo

Soma Zaidi...
Namna ya kugundua mtu mwenye kaswende.

Post hii inahusu zaidi njia za kumgundua mgonjwa wa kaswende, njia hizi utumika baada ya kuongea na mgonjwa kuhusu maisha yake hasa kujamiiana na watu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Tatizo la kujaa mate mdomoni nimeambiwa nina minyoo

Mie ni kijana wa kiume umri 33, nna tatizo la kujaa mate mdomoni nimeambiwa nna minyoo lakini hata nikinywa dawa sioni afadhali, niliona labda ni pombe nikapumzika kunywa tatizo lipo pale pale japo nisipokunywa haliwi kwa ukubwa ule ila lipo.

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya koo

Saratani ya Koo inarejelea Vivimbe vya Saratani vinavyotokea kwenye koo lako (koromeo), sanduku la sauti (larynx) au tonsils.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kabla ya upasuaji,

Upasuaji ni kundi la ki medical linalohusu kutoa kiungo kisichohitajika kwenye mwili.

Soma Zaidi...