picha

Vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri,kwa sababu siku kwa siku kuna magonjwa mengi yanayotokea kwenye sehemu za siri ila kuna vyanzo mbalimbali ambavyo usababisha kuwepo kwa magonjwa kwenye sehemu mbalimbali za siri

Vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

1. Kuna matumizi ya njia za uzazi wa mpango kwa kutumia vitanzi.

Kwa kawaida kwenye njia ya via vya uzazi hapatakuwi kitu chochote kuwepo isipokuwa kama kuna mimba na mfumo mzima wa mzunguko wa damu ila kwa matumizi ya njia za uzazi wa mpango kama vile kuwepo kwa vitanzi ambayo vina kemikali mbalimbali ambazo uzuia mimba kutungwa, kwa sababu ya kuwepo kwa kemikali hizo usababisha kiasi kikubwa cha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali kwenye sehemu za siri.kwa hiyo katika matumizi ya vitanzi ni vizuri kuwasiliana na wataalamu wa afya ili kuweza kupata matumizi sahihi.

 

2. Kubadilisha wapenzi mara kwa mara.

Kuna tabia ya watu wanaobadilisha wapenzi mara kwa mara , kumbuka wapenzi hao kila mtu ana ugonjwa wake kwa hiyo katika matumizi ya wapenzi hao bila kutumia kinga usababisha kuwepo kwa magonjwa ya siri.

 

3. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwa na mpenzi mmoja kama haujaolewa au ukiamua kuchepuka ni lazima kutumia kinga ili kuweza kuepukana na magonjwa ya siri kwa hiyo ni vizuri kabisa kupata hata matibabu na ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya ili kuweza kuepukana na madhara ya kuwepo kwa magonjwa kwenye sehemu za siri.

 

4. Matumizi ya bidhaa za marashi na aina yoyote ya vipodozi kwenye sehemu za siri.

Kuna tamaduni au utaratibu ambao unagundulika kila siku ambapo wanawake wanapenda kuweka mafuta na maradhi kwenye sehemu za siri ili kuweza kuwa kufurahisha wanaume zao, haya manukato na marashi usababisha kuua bakteria walio wazuri na kusababisha kuwepo kwa Ugonjwa kwenye sehemu za siri.

 

5. Kunyonywa kwenye sehemu za siri.

Kwa sababu ya maendeleo ya sayansi na teknolojia kuna kila aina ya vitu vinaibuka kila siku ambapo wanaume wengi wanapofanya ngono au wanapojamiiana mwanaume umnyonya mwanamke ili kuweza kusisimua hisia ,kwa hiyo mwanaume uweka bakteria wa mdomo wake kwenye uke ambapo Usababisha kuwepo kwa bakteria wa mdomo kwenye uke na kusababisha magonjwa kwenye sehemu za siri.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2360

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Madhara ya kichaa cha mbwa

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtu hajatibiwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisonono

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisonono, ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Neisseria gonococcal.

Soma Zaidi...
Athari za ugonjwa wa Dondakoo

Posti hii inahusu zaidi athari za ugonjwa wa Dondakoo,hali hii utokea iwapo ugonjwa haukutibiwa mapema au umetibiwa lakini bado Kuna matokea hasi ambayo yanaweza kujitokeza kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi kwenye mapafu

Posti hii inaonyesha dalili za fangasi kwenye mapafu.

Soma Zaidi...
Watu walio hatarini kupata ugonjwa wa pumu

Kila mtu anaweza kupata ugonjwa wa pumu, hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi kupata pumu.

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa pombe wakati Mtoto akiwa tumboni

Ugonjwa wa ulevi wakati Mtoto akiwa tumboni (fetasi) ni hali ya mtoto inayotokana na unywaji pombe wakati wa ujauzito wa mama. Ugonjwa wa pombe wa fetasi husababisha uharibifu wa ubongo na matatizo ya ukuaji.

Soma Zaidi...