Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu.
Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu. Ni vyema kujiweka tayari kisaikolojia kabla ya kushiriki tendo la ndoa. Kwa upande wa vyakula ni vyema kuchaguwa vyakula vilivyo salama kwa afya. Vyakula vyenye mafuta kupitiliza vinaweza kuleta athari mbaya kwa afya ya nguvu za kiume. Katika makala hii nitakuletea vyakula vitano ambavyo husaidia katika kuongeza hamu ya kushiriki tendo la ndoa:
Vyakula hivyo ni:
1. Vyakula vyenye arginine . Vyakula hivi vina ni vyakula vyenye chembechembe itambulikayo kama arginine. Ndani ya miili yetu arginine huweza kubadilishwa kuwa oxide ya nitric (nitric oxide). Arginine ni chembechembe za asidi ya amono (amino acid). vyakula vyenvye arginine ni kama maharage ya soya, mbegu za maboga, karanga, korosho, samaki, nyama, kuku na samaki.
Arginine imafaida nyingi sana mwilini. Chembechembe hii huweza kutibu tatizo la kusinyaa kwa uume kabla ya kumwaga, ama kusinyaa mapema, ama kugoma kabisa kusiama. Kama tatizo hili linahusiana na mishipa ya damua kama kuziba kwa mishiba ya damu basi arginine ni msaada mkubwa. Pia husaidia kuimarisha afya kwa wenye kisukari na wenye maradhi ya moyo hususani yanayohusiana na mishipa ya damu kama kujaa mafuta ama kuziba.
2. Vyakula vyenye phytochemical: vyakula hivi ni kama maepo (apples),mboga za apricots, broccoli, Brussels sprouts, kabichi (cabbage), karoto (carrots), cauliflower, kitunguu thaumu (garlic), mimea jamii ya kunde (legumes), kitunguu maji (onion), pilipili kali (red peppers), maharage ya soya (soybeans), viazi vitamu (sweet potatoes), na nyanya (tomatoes).
3. Vyakula vya fati iliyo salama kwa afya ya moyo. Afya ya moyo huchukuwa nafasi kubwa katika tendo la ndoa. Uzima wa moyo huweza kufanya damu kutembea vyama maeneo yote ya mwili hususani maeneo yanayohusika katika tendo la ndoa.
Miongoni mwa vyakula hivi ni palachichi. Ndani ya palachichi kuna fat, vitamini B6 asidi ya folik (folic acid) kwa hamoja hizi husaidia kuongeza nishati mwilini na kuimarisha afya katika kushiriki tendo la ndoa. Vyakula vingine ni kama aina flani ya samaki, mayai, mbegu za chia, chokleti, bidhaa za maziwa kama siagi n.k
4. Vyakula vyenye citrulline aina ya asidi za amini (amino acid): hii ni chembechembe inayopatikana kwenye vyakula hivi, mwili hubadilisha chembechembe hii ni kuwa arginine. Faida za arginine tumeshaziona hapo juu. Chemikali hizi pia husaidia katika kuufanya mwili uweze kuwa shwari (relax) kama vile viagra inavyofanya kazi.
Miongoni mwa vyakula hivi ni tikitimaji. Tunda hili lina citrulline kwa wingi sana tofauti na matunda mengi. Vyakula vingine ni kama maboga, matang n.k. citrulline pia husaidia katika kutanua misuli na kuboresha mishipa ya damu kufanya kazi vyema hivyo ni nzuri kwa wanaofanya mazoezi. Kwa upande wa afya ya tendo la ndoa husaidia katika kupeleka damu kwenye maeneo nyeti.
5. Vyakula vyenye Indole-3-carbinol: hii husaidia katika kuboresha homoni hasa kwa wanaume. Huweza kupatikana kwenye mboga za majani kama kabichi, broccoli na mboga nyinginezo. Tofauti na faida hizi pia huweza kusaidia katika kuzuia na kupunguza athari za saratani ya matiti, tumbo, na nyinginezo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Saratani ya matiti ji moja kati ya saratani zinazosumbuwa wqnawake wengi. Katika somo hili utajifunza chanzo cha kutokea saratani ya matiti
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wajawazito wanaweza kuzipata wakiwa na Dalli au tayari wana kifafa cha mimba.
Soma Zaidi...Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtoto alizaliwa na uzito mkubwa.
Soma Zaidi...Utawezaje kukabiliana na changamoto za ujauzito, je ni zipi changamoto hizo. Hapa nitakujuza.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia katika kipindi Cha ujauzito au mimba
Soma Zaidi...In fact there is a lot of signs and symptoms of pregnancy a mother experiences throughout pregnant. These signs may start to be revealed immediately after conception or in the first week after conception. A term pregnancy is traditionally calculated by mi
Soma Zaidi...Makala hii itakwenda kukufundisha baadhi ya dalili za uchungu kwa mama mjamzito.
Soma Zaidi...