Menu



VYAKULA VYA KUONGEZA HAMU YA TENDO LA NDOA NA NGUVU ZA KIUME

Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu.

VYAKULA VYA KUONGEZA HAMU YA TENDO LA NDOA NA NGUVU ZA KIUME

Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume na hamu ya tendo la ndoa

Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu. Ni vyema kujiweka tayari kisaikolojia kabla ya kushiriki tendo la ndoa. Kwa upande wa vyakula ni vyema kuchaguwa vyakula vilivyo salama kwa afya. Vyakula vyenye mafuta kupitiliza vinaweza kuleta athari mbaya kwa afya ya nguvu za kiume. Katika makala hii nitakuletea vyakula vitano ambavyo husaidia katika kuongeza hamu ya kushiriki tendo la ndoa:

 

Vyakula hivyo ni:

1. Vyakula vyenye arginine . Vyakula hivi vina ni vyakula vyenye  chembechembe itambulikayo kama arginine. Ndani ya miili yetu arginine huweza kubadilishwa kuwa oxide ya nitric (nitric oxide). Arginine ni chembechembe za asidi ya amono (amino acid). vyakula vyenvye arginine ni kama maharage ya soya, mbegu za maboga, karanga, korosho, samaki, nyama, kuku na samaki.

 

Arginine imafaida nyingi sana mwilini. Chembechembe hii huweza kutibu tatizo la kusinyaa kwa uume kabla ya kumwaga, ama kusinyaa mapema, ama kugoma kabisa kusiama. Kama tatizo hili linahusiana na mishipa ya damua kama kuziba kwa mishiba ya damu basi arginine ni msaada mkubwa. Pia husaidia kuimarisha afya kwa wenye kisukari na wenye maradhi ya moyo hususani yanayohusiana na mishipa ya damu kama kujaa mafuta ama kuziba.

 

2. Vyakula vyenye phytochemical: vyakula hivi ni kama maepo (apples),mboga za  apricots, broccoli, Brussels sprouts, kabichi (cabbage), karoto (carrots), cauliflower, kitunguu thaumu (garlic), mimea jamii ya kunde (legumes), kitunguu maji (onion), pilipili kali (red peppers), maharage ya soya (soybeans), viazi vitamu (sweet potatoes), na nyanya (tomatoes).

 

3. Vyakula vya fati iliyo salama kwa afya ya moyo. Afya ya moyo huchukuwa nafasi kubwa katika tendo la ndoa. Uzima wa moyo huweza kufanya damu kutembea vyama maeneo yote ya mwili hususani maeneo yanayohusika katika tendo la ndoa.

 

Miongoni mwa vyakula hivi ni palachichi. Ndani ya palachichi kuna fat, vitamini B6 asidi ya folik (folic acid) kwa hamoja hizi husaidia kuongeza nishati mwilini na kuimarisha afya katika kushiriki tendo la ndoa. Vyakula vingine ni kama aina flani ya samaki, mayai, mbegu za chia, chokleti, bidhaa za maziwa kama siagi n.k

 

4. Vyakula vyenye  citrulline aina ya asidi za amini (amino acid): hii ni chembechembe inayopatikana kwenye vyakula hivi, mwili hubadilisha chembechembe hii ni kuwa arginine. Faida za arginine tumeshaziona hapo juu. Chemikali hizi pia husaidia katika kuufanya mwili uweze kuwa shwari (relax) kama vile viagra inavyofanya kazi.

 

Miongoni mwa vyakula hivi ni tikitimaji. Tunda hili lina  citrulline kwa wingi sana tofauti na matunda mengi. Vyakula vingine ni kama maboga, matang n.k.  citrulline pia husaidia katika kutanua misuli na kuboresha mishipa ya damu kufanya kazi vyema hivyo ni nzuri kwa wanaofanya mazoezi. Kwa upande wa afya ya tendo la ndoa husaidia katika kupeleka damu kwenye maeneo nyeti.

 

5. Vyakula vyenye Indole-3-carbinol: hii husaidia katika kuboresha homoni hasa kwa wanaume. Huweza kupatikana kwenye mboga za majani kama kabichi, broccoli na mboga nyinginezo. Tofauti na faida hizi pia huweza kusaidia katika kuzuia na kupunguza athari za saratani ya matiti, tumbo, na nyinginezo.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2501

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mabadiliko kwenye uke wa Mama pale anapobeba mimba.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye uke wa Mama pale anapobeba tu mimba, Mama anapobeba mimba Kuna mabadiliko Katika uke wa Mama kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Fahamu Faida za Uzazi wa mpango

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Faida za Uzazi wa mpango. Uzazi wa mpango ni huduma ambazo hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kulia

Soma Zaidi...
Ijue kazi ya homoni ya HCG wakati wa kupima mimba.

Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya HCG katika kupima mimba, HCG maana yake ni human chorionic gonadotropin ni homoni ambayo uonekanekana kwenye mkojo na damu kama mtu ana mimba.

Soma Zaidi...
Sababu za mwanamke kukosa hamu ya tendo la ndoa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mwanamke kukosa tendo la ndoa, ni sababu ambazo uwakuta wanawake wengi unakuta mama yuko kwenye ndoa ila hana hata hamu ya lile tendo la ndoa hali ambayo umfanya mwanamke kuona kitendo cha tendo la ndoa ni unyanyasaji au

Soma Zaidi...
Faida za uzazi wa mpango kwa watu wenye ugonjwa wa Ukimwi

Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.

Soma Zaidi...
Sifa za siku za kupata mimba

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya sifa za siku za kupata mimba

Soma Zaidi...
Dalili za kupata uvimbe kwenye kizazi (fibroid)

Post hii inaenda kufundisha kuhusiana na uvimbe wa kizazi kwa wanawake. Uvimbe wa kizazi no uvimbe ambao hutokea kwenye tumbo la kizazi ambao unaweza kuwa ndan ya kizazi uvimbe huu ndan ya mwanamke hujulikana kama (uterine myoma au fibroid). Uvi

Soma Zaidi...
Yajue madhara ya kutoa mimba mara Kwa mara

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa wale wenye tabia ya kutoa mimba mara Kwa mara .

Soma Zaidi...