Menu



Aina mbalimbali za mimba kutoka.

Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za mimba kutoka, hizi ni jinsi mimba inavyoonyesha dalili za kutoka na nyingine zinaweza kuonyesha dalili Ila kwa sababu ya huduma mbalimbali za kwanza hizo mimba zinaweza kudhibiiwa na mtoto akazaliwa.

Aina mbalimbali za mimba kutoka.

1. Kama tulivyoona kwenye utangulizi tunaweza kuona aina mbalimbali za mimba kutoka na dalili ambazo ujionyesha kwa namna Moja au nyingine, kwa hiyo zifuatazo ni aina mbalimbali za mimba kutoka.

 

 

 

2. Kuna mimba ambazo zinatishia kutoka ( threaten abortion).

 Hii ni aina mojawapo ya mimba kutaka kutoka ila mama akiwahi anaweza kusaidiwa  au kuzuia mimba hiyo isitoke , kwa kawaida mimba ya aina hiyo huwa na miezi sita, ikiwa mama ni mjamzito na akaona damu zinatoka ila kwa kawaida inakuwa ni ndogo kwa siku kama Ile inayotoka siku za mwezi au inawezekana ikawa ndogo yake na pia damu uendelea kutoka kidogo kidogo na panakuwepo na maumivu yasiyo ya Kawaida au kwa wanawake ambao wameshajifungua ni kama maumivu ya uchungu, ikiwa mama anaona hali kama hiyo awai hospital ni mimba Inayotishia kutoka ,  Mama akipata huduma haraka anaokoa  maisha ya   mtoto, mtoto anaendelea kukua na akafikia siku ya kuzaliwa  na anazaliwa kawaida tu.

 

 

 

 

 

2. Mimba ambayo inataka kutoka na hata juhudi zozote zikitolewa ni kazi Bure, kwa kitaamu huiitwa inevitable pregnant.

Hii ni aina ya mimba ambayo Ina dalili za kutoka kw  hata juhudi gani ziwekwe ni kazi Bure mimba ni lazima itoke tu,hii aina ya mimba ambayo ni tofauti na tuliyomaliza kuongelea hapo awali, kwa sababu mama anakuwa anatokwa na damu nyingi yakiandamana na maumivu yasiyo ya Kawaida na pia Mama anakuwa na maumivu makali ya mgongo na katika kumwangalia unaona kama mimba imeshaharibika , kwa hiyo mjamzito akiona dalili kama hii ni vizuri kwenda hospital Moja kwa Moja , kwa kawaida mimba za hivi huwa ni chini ya miezi sita, kwa hiyo jamii na wote waliomzunguka wanapaswa kumsaidia mama Ili aweze kwenda kupata matibabu kwa sababu kama mimba ikitoka akiwa nyumbani ni hatari kwa sababu Kuna vipande vipande vinaweza kubaki na kusababisha madhara makubwa kwa Mama.

 

 

 

 

 

3. Mimba ambayo imeshatoka ila Kuna vipanda vipande vimebaki.( Kwa kitaamu huiitwa incomplete abortion)

hii  ni aina ya mimba ambayo ikitoka Kuna baadhi ya vipande vipande vinabaki ndani ya mfuko wa uzazi wa Mama,au kwa wakati mwingine sehemu ya kondo la nyuma ubaki, hali hii utokea kwa akina Mama ambao dalili za kutoka kwa mimba utokea wakiwa nyumbani ila kwa sababu ya mazingira au matatizo ya kiuchumi ukazana au kujikaza na kuacha mimba ikatoka wakiwa nyumbani hali inayosababisha baadhi ya vipande kubaki na hali hii usababisha mama kuumia tumbo au pengine kuwepo kwa maambukizi ambayo kwa kitaamu huiitwa sepsis, kwa hiyo kwa ajili ya kuokoa maisha ya Mama ingawa mtoto ameshaondoka, kwa hiyo jamii inapaswa kujua na kuelewa kwamba pindi tu Mama anapobeba mimba maandalizi yanapaswa kuanza hasa ki uchumu kwa kutunza Hela ndogo ndogo Ili kuweza kuokoa maisha ya Mama na mtoto kwa sababu chochote kinaweza kutoka wakati wa ujauzito, kwa hiyo akina Mama wanapatwa na hali hii kwa sababu hawana ela ya kukidhi matibabu endapo mimba zikitoka wakiwa nyumbani hali inayopelekewa mimba kutoka kienyeji na vipande vipande vinabaki.

 

 

 

 

 

4. Mimba inayotoka ni vipande vipande vikatoka kabisa na kuisha.

Hii ni tofauti na mimba ambayo tumetoka kujadili aina hii ya mimba kwa kitaamu huiitwa complete abortion, Dalili za kutoka kwa mimba zote zinakuwepo kama vile maumivu makali ya tumbo, maumivu ya mgongo na kuwepo kwa uchungu, na hatimaye mimba utoka na inapotoka kila kitu kinatoka na hakuna kinachobaki na damu pia uacha kuvuja ndani ya mda mfupi, ila ubaki maumivu ya Kawaida tu ,kwa hali hii hata mama akiwa nyumbani hakuna shida kwa sababu kila kitu kimetoka ila ni vizuri kabisa kujihakikishia kama kila kitu kimetoka kwa kuwaona wataalamu wa afya au kwenda kituo cha afya kilicho karibu kwa ajili ya uangalizi. Kwa hiyo ni vizuri kabisa jamii inayomzunguka Mama kumpa ushirikiano wa kutoka katika hali ngumu kama hii.

 

 

 

 

 

5. Kuna mimba ambapo mtoto anafia tumboni akiwa chini ya miezi sita.

Hii uitwa aina mojawapo ya mimba kutoka kwa sababu mimba inakuwa chini ya miezi sita na mtoto anafia tumboni, hali hii utokea kwa sababu mbalimbali kama vile, labda maambukizi ya magonjwa kama vile kaswende, kisonono, malaria, UTI na maambukizi mbalimbali, au labda Mama kapigwa na kusababisha mtoto kufia tumboni, mimba za aina hii huwa na dalili mbalimbali kama vile mtoto kuhindwa kucheza, mapigo ya mtoto kutosikika na mama akilalia ubavu na mtoto uelekea huko na akibadilisha ubavu mwingine na mtoto ulalia huko hali hii umfanya Mama kuwa na wasiwasi, kwa hiyo Mama akiona dalili za hivyo ni vizuri kabisa kuwahi hospital Ili kuokoa maisha yake.

 

 

 

 

 

 

6. Mimba kutoka Kuna sababu mbalimbali ambazo usababisha kwa hiyo mama aikona dalili yoyote ya mimba kutoka ni vizuri kabisa kuwahi kituo cha afya ili kupata matibabu zaidi na pia ndugu waliomzunguka wanapaswa kumpatia ushirikiano nzuri Ili kuweza kumsaidia Mama akiwa katika hali hii.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2385

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Ni ipi hasa siku ambayo nitafute ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kutafuta ujauzito

Soma Zaidi...
Mbinu za kuwakinga watoto na saratani.

Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo tunaweza kuzitumia ili kuwakinga watoto dhidi ya saratani, kama tulivyotangulia kusema kwamba saratani ya watoto mara nyingi Usababishwa na akina Mama hasa kwa sababu ya mtindo wa maisha wakati wa ujauzito kwa hiyo tun

Soma Zaidi...
Je mjamzito Uchungu ukikata inakuwaje

Hutokea uchungu wa kujifunguwa ukakati. Unadhani ni kitugani kinatokea.

Soma Zaidi...
siku za kupata mimba

Makala hii inakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata mimba na dalili za siku hizo.

Soma Zaidi...
mkewang alikuwa anasumbuliwa na tumbo kama siku tatu lika tuliya saivi analalamika kiuno na mgongo vina muuma nini tatizo tockt

Maumivu ya tumbo nakiuno kwa mwanamke yanahitaji uangalizi wakina. Kwani kuna sababu nyingi ambazo zinawezakuwa ni chanzo.

Soma Zaidi...
Nimetoka kufanya tendo la ndoa ghafla tumbo likaanza kukaza upande wa kushoto na kutoka maji yenye uzito wa kawaida kama ute mengi je hii itakuwa ni nini

Maumivu yavtumbo huwenda yakachanganya sana, Keane yanahusianana sababu nyingi sana. Kina baadhi ya watu hupata na maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa ama punde tu baada ya kumaliza.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kunyonyesha mtoto

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kunyonyesha mtoto, kunyonyesha ni kitendo cha Mama kutumia titi lake Ili kuweza kumpatia mtoto lishe kwa kipindi chote ambacho Mama upaswa kutumia kwa kunyonyesha mtoto wake kwa hiyo Kuna faida ambazo mama uzipata kutoka

Soma Zaidi...
Njia za kutibu mbegu dhaifu.

Posti hii inahusu zaidi njia za kutibu mbegu dhaifu, ni njia ambazo utumika kutibu mbegu ambazo ni dhaifu ili kuweza kuondoa tatizo hili ambalo limewakumba wanaume wengi na kusababisha madhara makubwa kwenye ndoa au familia.

Soma Zaidi...
Mabaka yanayowasha chini ya matiti.

Posti hii inahusu zaidi mabaka yanayowasha chini ya matiti, ni ugonjwa ambao uwapata wanawake walio wengi na wengine hawajapata jibu Sababu zake ni zipi na pengine uchukua hatua za kutumia miti shamba wakidai juwa hospitalini nugonjwa huu hautibiwa, ila n

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha uume kutoa maji meupe bila muwasho,na tiba yake ni ipi

Je unasumbuliwa na Majimaji kwenye uume. Je unapata miwasho, ama maumivu wakati wakukojoa.

Soma Zaidi...