picha

Aina mbalimbali za mimba kutoka.

Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za mimba kutoka, hizi ni jinsi mimba inavyoonyesha dalili za kutoka na nyingine zinaweza kuonyesha dalili Ila kwa sababu ya huduma mbalimbali za kwanza hizo mimba zinaweza kudhibiiwa na mtoto akazaliwa.

Aina mbalimbali za mimba kutoka.

1. Kama tulivyoona kwenye utangulizi tunaweza kuona aina mbalimbali za mimba kutoka na dalili ambazo ujionyesha kwa namna Moja au nyingine, kwa hiyo zifuatazo ni aina mbalimbali za mimba kutoka.

 

 

 

2. Kuna mimba ambazo zinatishia kutoka ( threaten abortion).

 Hii ni aina mojawapo ya mimba kutaka kutoka ila mama akiwahi anaweza kusaidiwa  au kuzuia mimba hiyo isitoke , kwa kawaida mimba ya aina hiyo huwa na miezi sita, ikiwa mama ni mjamzito na akaona damu zinatoka ila kwa kawaida inakuwa ni ndogo kwa siku kama Ile inayotoka siku za mwezi au inawezekana ikawa ndogo yake na pia damu uendelea kutoka kidogo kidogo na panakuwepo na maumivu yasiyo ya Kawaida au kwa wanawake ambao wameshajifungua ni kama maumivu ya uchungu, ikiwa mama anaona hali kama hiyo awai hospital ni mimba Inayotishia kutoka ,  Mama akipata huduma haraka anaokoa  maisha ya   mtoto, mtoto anaendelea kukua na akafikia siku ya kuzaliwa  na anazaliwa kawaida tu.

 

 

 

 

 

2. Mimba ambayo inataka kutoka na hata juhudi zozote zikitolewa ni kazi Bure, kwa kitaamu huiitwa inevitable pregnant.

Hii ni aina ya mimba ambayo Ina dalili za kutoka kw  hata juhudi gani ziwekwe ni kazi Bure mimba ni lazima itoke tu,hii aina ya mimba ambayo ni tofauti na tuliyomaliza kuongelea hapo awali, kwa sababu mama anakuwa anatokwa na damu nyingi yakiandamana na maumivu yasiyo ya Kawaida na pia Mama anakuwa na maumivu makali ya mgongo na katika kumwangalia unaona kama mimba imeshaharibika , kwa hiyo mjamzito akiona dalili kama hii ni vizuri kwenda hospital Moja kwa Moja , kwa kawaida mimba za hivi huwa ni chini ya miezi sita, kwa hiyo jamii na wote waliomzunguka wanapaswa kumsaidia mama Ili aweze kwenda kupata matibabu kwa sababu kama mimba ikitoka akiwa nyumbani ni hatari kwa sababu Kuna vipande vipande vinaweza kubaki na kusababisha madhara makubwa kwa Mama.

 

 

 

 

 

3. Mimba ambayo imeshatoka ila Kuna vipanda vipande vimebaki.( Kwa kitaamu huiitwa incomplete abortion)

hii  ni aina ya mimba ambayo ikitoka Kuna baadhi ya vipande vipande vinabaki ndani ya mfuko wa uzazi wa Mama,au kwa wakati mwingine sehemu ya kondo la nyuma ubaki, hali hii utokea kwa akina Mama ambao dalili za kutoka kwa mimba utokea wakiwa nyumbani ila kwa sababu ya mazingira au matatizo ya kiuchumi ukazana au kujikaza na kuacha mimba ikatoka wakiwa nyumbani hali inayosababisha baadhi ya vipande kubaki na hali hii usababisha mama kuumia tumbo au pengine kuwepo kwa maambukizi ambayo kwa kitaamu huiitwa sepsis, kwa hiyo kwa ajili ya kuokoa maisha ya Mama ingawa mtoto ameshaondoka, kwa hiyo jamii inapaswa kujua na kuelewa kwamba pindi tu Mama anapobeba mimba maandalizi yanapaswa kuanza hasa ki uchumu kwa kutunza Hela ndogo ndogo Ili kuweza kuokoa maisha ya Mama na mtoto kwa sababu chochote kinaweza kutoka wakati wa ujauzito, kwa hiyo akina Mama wanapatwa na hali hii kwa sababu hawana ela ya kukidhi matibabu endapo mimba zikitoka wakiwa nyumbani hali inayopelekewa mimba kutoka kienyeji na vipande vipande vinabaki.

 

 

 

 

 

4. Mimba inayotoka ni vipande vipande vikatoka kabisa na kuisha.

Hii ni tofauti na mimba ambayo tumetoka kujadili aina hii ya mimba kwa kitaamu huiitwa complete abortion, Dalili za kutoka kwa mimba zote zinakuwepo kama vile maumivu makali ya tumbo, maumivu ya mgongo na kuwepo kwa uchungu, na hatimaye mimba utoka na inapotoka kila kitu kinatoka na hakuna kinachobaki na damu pia uacha kuvuja ndani ya mda mfupi, ila ubaki maumivu ya Kawaida tu ,kwa hali hii hata mama akiwa nyumbani hakuna shida kwa sababu kila kitu kimetoka ila ni vizuri kabisa kujihakikishia kama kila kitu kimetoka kwa kuwaona wataalamu wa afya au kwenda kituo cha afya kilicho karibu kwa ajili ya uangalizi. Kwa hiyo ni vizuri kabisa jamii inayomzunguka Mama kumpa ushirikiano wa kutoka katika hali ngumu kama hii.

 

 

 

 

 

5. Kuna mimba ambapo mtoto anafia tumboni akiwa chini ya miezi sita.

Hii uitwa aina mojawapo ya mimba kutoka kwa sababu mimba inakuwa chini ya miezi sita na mtoto anafia tumboni, hali hii utokea kwa sababu mbalimbali kama vile, labda maambukizi ya magonjwa kama vile kaswende, kisonono, malaria, UTI na maambukizi mbalimbali, au labda Mama kapigwa na kusababisha mtoto kufia tumboni, mimba za aina hii huwa na dalili mbalimbali kama vile mtoto kuhindwa kucheza, mapigo ya mtoto kutosikika na mama akilalia ubavu na mtoto uelekea huko na akibadilisha ubavu mwingine na mtoto ulalia huko hali hii umfanya Mama kuwa na wasiwasi, kwa hiyo Mama akiona dalili za hivyo ni vizuri kabisa kuwahi hospital Ili kuokoa maisha yake.

 

 

 

 

 

 

6. Mimba kutoka Kuna sababu mbalimbali ambazo usababisha kwa hiyo mama aikona dalili yoyote ya mimba kutoka ni vizuri kabisa kuwahi kituo cha afya ili kupata matibabu zaidi na pia ndugu waliomzunguka wanapaswa kumpatia ushirikiano nzuri Ili kuweza kumsaidia Mama akiwa katika hali hii.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/11/07/Monday - 05:53:54 pm Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 3181

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 web hosting    πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Namna ya kutibu ugumba kwa Mwanaume.

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutibu tatizo la ugumba kwa Mwanaume, ni njia ambazo utumiwa na wataalam mbalimbali Ili kuweza kutibu tatizo la ugumba kwa wanaume.

Soma Zaidi...
Ni ili sababu ya kutokea kwa tezi dume

Tezidume ni moja ya magonjwa hayari yanayotokea katika mwili wa mwanaume.Hapa nimekuandalia sababu za kutokea kwa tezi dume.

Soma Zaidi...
Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa

Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa

Soma Zaidi...
Dalili za mimba yenye uvimbe

Mimba ya tumbo - pia inajulikana kama hydatidiform mole - ni ugumu usiyo na kansa (benign) ambayo hutokea kwenye uterasi. Mimba ya molar huanza wakati yai linaporutubishwa, lakini badala ya mimba ya kawaida, yenye uwezo wa kutokea, plasenta hukua na kuwa

Soma Zaidi...
Nataka nijue Kuwa njia yakuzuia mimba wakati Wakufany tendo La ndoa

Je ungependa kuijuwa Njia ya kuzuia mimba wakati wa tendo la ndoa?. Posti hii itakwenda kukufundisha ujanja huu.

Soma Zaidi...
Mambo yanayodhihirisha afya ya nguvu za kiume

Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali yanayodhoofisha afya za wanaume, kwa wakati mwingine wanaume ukosa kujiamini kwa sababu ya mambo ambayo yanaadhiri afya za wanaume.

Soma Zaidi...
Dalili za kasoro ya moyo za kuzaliwa kwa watoto

Ikiwa mtoto wako ana kasoro ya moyo wa kuzaliwa, ina maana kwamba mtoto wako alizaliwa na tatizo katika muundo wa moyo wake. Baadhi ya kasoro za moyo za kuzaliwa kwa watoto ni rahisi na hazihitaji matibabu, kama vile tundu dogo kati ya chemba za moyo amb

Soma Zaidi...
Mambo muhimu ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia katika kipindi Cha ujauzito au mimba

Soma Zaidi...
Jinsi mimba inavyotungwa na namna ambavyo jinsia ya mtoto inavyotokea

Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaumeΒ  .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu.

Soma Zaidi...
Je mjamzito Uchungu ukikata inakuwaje

Hutokea uchungu wa kujifunguwa ukakati. Unadhani ni kitugani kinatokea.

Soma Zaidi...