Aina mbalimbali za mimba kutoka.


image


Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za mimba kutoka, hizi ni jinsi mimba inavyoonyesha dalili za kutoka na nyingine zinaweza kuonyesha dalili Ila kwa sababu ya huduma mbalimbali za kwanza hizo mimba zinaweza kudhibiiwa na mtoto akazaliwa.


Aina mbalimbali za mimba kutoka.

1. Kama tulivyoona kwenye utangulizi tunaweza kuona aina mbalimbali za mimba kutoka na dalili ambazo ujionyesha kwa namna Moja au nyingine, kwa hiyo zifuatazo ni aina mbalimbali za mimba kutoka.

 

 

 

2. Kuna mimba ambazo zinatishia kutoka ( threaten abortion).

 Hii ni aina mojawapo ya mimba kutaka kutoka ila mama akiwahi anaweza kusaidiwa  au kuzuia mimba hiyo isitoke , kwa kawaida mimba ya aina hiyo huwa na miezi sita, ikiwa mama ni mjamzito na akaona damu zinatoka ila kwa kawaida inakuwa ni ndogo kwa siku kama Ile inayotoka siku za mwezi au inawezekana ikawa ndogo yake na pia damu uendelea kutoka kidogo kidogo na panakuwepo na maumivu yasiyo ya Kawaida au kwa wanawake ambao wameshajifungua ni kama maumivu ya uchungu, ikiwa mama anaona hali kama hiyo awai hospital ni mimba Inayotishia kutoka ,  Mama akipata huduma haraka anaokoa  maisha ya   mtoto, mtoto anaendelea kukua na akafikia siku ya kuzaliwa  na anazaliwa kawaida tu.

 

 

 

 

 

2. Mimba ambayo inataka kutoka na hata juhudi zozote zikitolewa ni kazi Bure, kwa kitaamu huiitwa inevitable pregnant.

Hii ni aina ya mimba ambayo Ina dalili za kutoka kw  hata juhudi gani ziwekwe ni kazi Bure mimba ni lazima itoke tu,hii aina ya mimba ambayo ni tofauti na tuliyomaliza kuongelea hapo awali, kwa sababu mama anakuwa anatokwa na damu nyingi yakiandamana na maumivu yasiyo ya Kawaida na pia Mama anakuwa na maumivu makali ya mgongo na katika kumwangalia unaona kama mimba imeshaharibika , kwa hiyo mjamzito akiona dalili kama hii ni vizuri kwenda hospital Moja kwa Moja , kwa kawaida mimba za hivi huwa ni chini ya miezi sita, kwa hiyo jamii na wote waliomzunguka wanapaswa kumsaidia mama Ili aweze kwenda kupata matibabu kwa sababu kama mimba ikitoka akiwa nyumbani ni hatari kwa sababu Kuna vipande vipande vinaweza kubaki na kusababisha madhara makubwa kwa Mama.

 

 

 

 

 

3. Mimba ambayo imeshatoka ila Kuna vipanda vipande vimebaki.( Kwa kitaamu huiitwa incomplete abortion)

hii  ni aina ya mimba ambayo ikitoka Kuna baadhi ya vipande vipande vinabaki ndani ya mfuko wa uzazi wa Mama,au kwa wakati mwingine sehemu ya kondo la nyuma ubaki, hali hii utokea kwa akina Mama ambao dalili za kutoka kwa mimba utokea wakiwa nyumbani ila kwa sababu ya mazingira au matatizo ya kiuchumi ukazana au kujikaza na kuacha mimba ikatoka wakiwa nyumbani hali inayosababisha baadhi ya vipande kubaki na hali hii usababisha mama kuumia tumbo au pengine kuwepo kwa maambukizi ambayo kwa kitaamu huiitwa sepsis, kwa hiyo kwa ajili ya kuokoa maisha ya Mama ingawa mtoto ameshaondoka, kwa hiyo jamii inapaswa kujua na kuelewa kwamba pindi tu Mama anapobeba mimba maandalizi yanapaswa kuanza hasa ki uchumu kwa kutunza Hela ndogo ndogo Ili kuweza kuokoa maisha ya Mama na mtoto kwa sababu chochote kinaweza kutoka wakati wa ujauzito, kwa hiyo akina Mama wanapatwa na hali hii kwa sababu hawana ela ya kukidhi matibabu endapo mimba zikitoka wakiwa nyumbani hali inayopelekewa mimba kutoka kienyeji na vipande vipande vinabaki.

 

 

 

 

 

4. Mimba inayotoka ni vipande vipande vikatoka kabisa na kuisha.

Hii ni tofauti na mimba ambayo tumetoka kujadili aina hii ya mimba kwa kitaamu huiitwa complete abortion, Dalili za kutoka kwa mimba zote zinakuwepo kama vile maumivu makali ya tumbo, maumivu ya mgongo na kuwepo kwa uchungu, na hatimaye mimba utoka na inapotoka kila kitu kinatoka na hakuna kinachobaki na damu pia uacha kuvuja ndani ya mda mfupi, ila ubaki maumivu ya Kawaida tu ,kwa hali hii hata mama akiwa nyumbani hakuna shida kwa sababu kila kitu kimetoka ila ni vizuri kabisa kujihakikishia kama kila kitu kimetoka kwa kuwaona wataalamu wa afya au kwenda kituo cha afya kilicho karibu kwa ajili ya uangalizi. Kwa hiyo ni vizuri kabisa jamii inayomzunguka Mama kumpa ushirikiano wa kutoka katika hali ngumu kama hii.

 

 

 

 

 

5. Kuna mimba ambapo mtoto anafia tumboni akiwa chini ya miezi sita.

Hii uitwa aina mojawapo ya mimba kutoka kwa sababu mimba inakuwa chini ya miezi sita na mtoto anafia tumboni, hali hii utokea kwa sababu mbalimbali kama vile, labda maambukizi ya magonjwa kama vile kaswende, kisonono, malaria, UTI na maambukizi mbalimbali, au labda Mama kapigwa na kusababisha mtoto kufia tumboni, mimba za aina hii huwa na dalili mbalimbali kama vile mtoto kuhindwa kucheza, mapigo ya mtoto kutosikika na mama akilalia ubavu na mtoto uelekea huko na akibadilisha ubavu mwingine na mtoto ulalia huko hali hii umfanya Mama kuwa na wasiwasi, kwa hiyo Mama akiona dalili za hivyo ni vizuri kabisa kuwahi hospital Ili kuokoa maisha yake.

 

 

 

 

 

 

6. Mimba kutoka Kuna sababu mbalimbali ambazo usababisha kwa hiyo mama aikona dalili yoyote ya mimba kutoka ni vizuri kabisa kuwahi kituo cha afya ili kupata matibabu zaidi na pia ndugu waliomzunguka wanapaswa kumpatia ushirikiano nzuri Ili kuweza kumsaidia Mama akiwa katika hali hii.



Sponsored Posts


  ๐Ÿ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ๐Ÿ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ๐Ÿ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ๐Ÿ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms โœ‰ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mwana mke wang mwezi wa 8 alipima mimba kwa kipimo cha mkojo ikaleta postive lina mwez wa 8 huo huo mwishoni akaingia period ndo ikawa mwisho had leo hii hajawahi ingia tena na kila mara tumbo linamuuma na akipima anakuta hana mimba
Inaweza kutokea ukapima mimbaikawa ipo, na baada ya wiki kadhaa unapima tena haipo. Hali hii unadhani inaweza kusababishwa na nini? Soma Zaidi...

image Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa
Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kushusha homoni za kiume.
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza homoni za kiume kwa akina dada. Soma Zaidi...

image Zifahamu fibroids (uvimbe kwenye via vya uzazi)
Posti hii inahusu zaidi fibroids au uvimbe kwenye via vya uzazi hasa hasa utokea kwenye tumbo la uzazi ambapo kwa kitaalamu huitwa uterusi, uvimbe huu ulitokea watu wengine huwa hawawezi kutambua Dalili zake mapema kwa hiyo leo tunapaswa kujua Dalili zake kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

image Uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama.
Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama na mtoto. Soma Zaidi...

image Mabadiliko ya via vya uzazi kwa Mama mjamzito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye via vya uzazi kwa wajawazito, tunajua kuwa Mama akibeba mimba tu kuna mabadiliko utokea katika sehemu mbalimbali za mwili. Soma Zaidi...

image Vyakula vinavyosaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone
Posti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo usaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone. Soma Zaidi...

image Tatizo la muingiliano wa majimaji ya Amniotic au seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito.
posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtoto kwenye uterasi wakati wa ujauzito au nyenzo za fetasi, kama vile nywele, zinapoingia kwenye damu ya mama. Amniotic Fluid Embolism ina uwezekano mkubwa wa kutokea wakati wa kuzaa au mara tu baadaye. Soma Zaidi...

image Sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusiana na kubalehe kwa msichana na mvulana.
Kubaleheร‚ย ni wakati mwili wa mtoto unapoanza kubadilika na kuwa wa mtu mzima (balehe) hivi karibuni. Kubalehe ambao huanza kabla ya umri wa miaka 8 kwa wasichana na kabla ya umri wa miaka 9 kwa wavulana. Soma Zaidi...