picha

Sababu za kutokea uvimbe kwenye kizazi.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi,kwa kawaida tumesikia akina mama wengi wanalalamika kuhusu kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na wengine hawajui sababu zake kwa hiyo sababu zifuatazo ni za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Sababu za uvimbe kwenye kizazi.

1.kuongezeka kwa vichocheo vya homoni ambazo ni progesterone homoni na oestrogen homoni.

Hizi homoni kwa kawaida zinakuwepo kwenye mwili ila ikitokea zikaongezeka zaidi zinaweza kuleta madhara ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo hizi homoni zinapaswa kuwepo kwa kiwango maalumu sio kuzidi sana.

 

2. Kuwepo kwa ujauzito.

Kwa kawaida ujauzito uweza kusababisha kuwepo kwa uvimbe kwa sababu wakati wa kujifungua kuna uchafu mwingine ukibaki uweza kusababisha kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

 

3. Uzito na unene kupita kiasi.

Kwa wakati mwingine kuna kiasi cha uzito au unene kupita kiasi kwa sababu mwili ni kama umejaza vitu mbalimbali na ambavyo havina mazoezi kwa hiyo uendelee ujirunda ndani na hatimaye kusababisha uvimbe kwenye kizazi.

 

4. Kuwepo kwa mfumo usio sawa wa mishipa ya damu.

Kitendo cha kuwepo kwa mfumo usio sawa wa mishipa ya damu Usababisha uvimbe kwa sababu kwa wakati mwingine damu haiwezi kusafili kutoka sehemu moja kwenda nyingine na hali hii Usababisha uvimbe kwenye kizazi.

 

5. Sababu za kuridhi.

Kuna familia nyingine huwa na tatizo hili la kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na kufanya kila mtoto anayezaliwa kwenye familia hiyo kuwa nao hii ni kwa sababu familia hiyo inakuwa na uzalishaji wa homoni zisizofaa na kusababisha uvimba kwa kizazi.

 

6. Lishe isiyofaa 

Kuwepo kwa lishe isiyofaa nalo ni tatizo la kufanya uvimbe kwenye kizazi kwa sababu tunajuwa wazi kuwa chakula ni dawa kwa hiyo bila lishe ya muhimu kila ugonjwa utakushambulia. Kwa hiyo tunapaswa kutumia vyakula vya kutosha na vyenye lishe bora

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2737

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Mambo ya kuzingatia kwa mtoto mara tu anapozaliwa

Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.

Soma Zaidi...
Mda wa kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua

Posti hii inahusu zaidi mda ambao mama anapaswa kukaa bila kufanya tendo la ndoa mara tu baada ya kujifungua.

Soma Zaidi...
Madhara ya kutotoa huduma kwa Mama anayevuja damu baada ya kujifungua

Posti hii inahusu zaidi Madara ya kutomsaidia mama anayetokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

Soma Zaidi...
Kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi

Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi.

Soma Zaidi...
Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi

Posti hii inahusu msaada kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi, hizi ni huduma ambazo utolewa kwa wale wenye maumivu ya tumbo la hedhi.

Soma Zaidi...
Mimba iliyotunga nje

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya

Soma Zaidi...