Sababu za kutokea uvimbe kwenye kizazi.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi,kwa kawaida tumesikia akina mama wengi wanalalamika kuhusu kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na wengine hawajui sababu zake kwa hiyo sababu zifuatazo ni za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
Sababu za uvimbe kwenye kizazi.
1.kuongezeka kwa vichocheo vya homoni ambazo ni progesterone homoni na oestrogen homoni.
Hizi homoni kwa kawaida zinakuwepo kwenye mwili ila ikitokea zikaongezeka zaidi zinaweza kuleta madhara ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo hizi homoni zinapaswa kuwepo kwa kiwango maalumu sio kuzidi sana.
2. Kuwepo kwa ujauzito.
Kwa kawaida ujauzito uweza kusababisha kuwepo kwa uvimbe kwa sababu wakati wa kujifungua kuna uchafu mwingine ukibaki uweza kusababisha kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
3. Uzito na unene kupita kiasi.
Kwa wakati mwingine kuna kiasi cha uzito au unene kupita kiasi kwa sababu mwili ni kama umejaza vitu mbalimbali na ambavyo havina mazoezi kwa hiyo uendelee ujirunda ndani na hatimaye kusababisha uvimbe kwenye kizazi.
4. Kuwepo kwa mfumo usio sawa wa mishipa ya damu.
Kitendo cha kuwepo kwa mfumo usio sawa wa mishipa ya damu Usababisha uvimbe kwa sababu kwa wakati mwingine damu haiwezi kusafili kutoka sehemu moja kwenda nyingine na hali hii Usababisha uvimbe kwenye kizazi.
5. Sababu za kuridhi.
Kuna familia nyingine huwa na tatizo hili la kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na kufanya kila mtoto anayezaliwa kwenye familia hiyo kuwa nao hii ni kwa sababu familia hiyo inakuwa na uzalishaji wa homoni zisizofaa na kusababisha uvimba kwa kizazi.
6. Lishe isiyofaa
Kuwepo kwa lishe isiyofaa nalo ni tatizo la kufanya uvimbe kwenye kizazi kwa sababu tunajuwa wazi kuwa chakula ni dawa kwa hiyo bila lishe ya muhimu kila ugonjwa utakushambulia. Kwa hiyo tunapaswa kutumia vyakula vya kutosha na vyenye lishe bora
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 web hosting 👉3 ai web app 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Siku za hatari, siku za kubeba mimba
Hizi ni siku hatari kwa mwanamke ambazo ni ahisi kwake kubeba mimba, siku nitakueleza ni zipi na ni zipi sifa zake
Soma Zaidi...Upungufu wa homoni ya estrogen
Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa Mama
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.
Soma Zaidi...Njia za kumsafisha Mama aliyetoa mimba.
Post hii inahusu njia safi za kumsafisha Mama ambaye ametoa mimba au mtoto amefia tumboni.
Soma Zaidi...Utaratibu wa kushiriki tendo la ndoa kwa wajawazito
Jifunze muda ambao mjamzito hatatkiwa kishiriki tendo la ndoa. je kuna madhara kwa mjamzito kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Kwa nini hujapata siku zako za hedhi.
Unaweza kupitiliza siku zako za hedhi kwa sababu nyingi. Post hii itakueleza ni kwa nini umechelewa kupata siku zako.
Soma Zaidi...