Posti hii inahusu zaidi Dalili za uvimbe kwenye kizazi,hizi ni Dalili ambazo ujitokeza kwa akina mama ambao wana uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo endapo mama ameona Dalili kama hizi anapaswa kuwahi hospitali mara moja kwa uangalizi zaidi.
Dalili za uvimbe kwenye kizazi.
1. Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi.
Hii ni Dalili mojawapo ambayo inaweza kujitokeza kwa Mama au msichana ambaye hajaolewa, ikitokea damu ikaongezeka kupita kiasi kusiko kwa kawaida wakati wa hedhi ni Dalili mojawapo ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
2. Maumivu makali wakati wa hedhi.
Kwa wakati mwingine maumivu yanaweza kuwa makali kuliko kawaida au mtu mwingine anakuwa hana maumivu wakati wa hedhi ila ikitokea shida hizi ya kuwepo kwa uvimbe maumivu yanaanza kuwepo.
3. Kuvimba miguu.
Nayo ni Dalili ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi utaona mama au mdada yeyote amevimba miguu kwa hiyo anapaswa kwenda hospitalini kupima.
4. Maumivu wakati wa tendo la ndoa.
Kwa wenye matatizo ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi wanapatwa na maumivu wakati wa tendo la ndoa na kwa hiyo huwa hawana furaha wakati wa tendo ila ni maumivu tu.
5. Kuwepo kwa gesi tumboni .
Au kwa wakati mwingine mtu ujisikia kama amevimbiwa na tumbo linakaa limevimba kama vile linakuwa na gesi.
6. Kupata choo kigumu au kufunga choo kabisa .
Kwa kawaida mtu mwenye matatizo ya kuwepo kwa uvimbe huwa na matatizo ya kukosa choo na huko anakuwa anakula chakula kawaida na kwa wakati mwingine anahisi kwenda haja kubwa ila choo kigumu nakuwa kama kigumu sana.
7. Maumivu n kwenye mgongo.
Hili tatizo uwapata wanawake walio wengi na udhani ni mgongo inauma lakini baada ya kufanyiwa upasuaji na kutoa uvimbe kwenye kizazi maumivu haya hayatokeagi tena.
8. Maumivu kwenye miguu na miguu kuvimba.
Kwa wakati mwingine Maumivu yanakiwepo kwenye miguu na miguu uanza kuvimba .
9. Kuwepo kwa ugumba au uzazi wa shida.
Kwa wakati mwingine wa mama wengi wanaangalia kutafuta watoto na hawapati shida kubwa inakuwa kwenye kizazi na wakifanyiwa upasuaji wanaweza kupata watoto.
10. Maumivu kwenye nyonga.
Kwa wakati mwingine mama huwa anapata maumivu makali kwenye nyonga ambayo umfanya mama kulalamika kila wakati.
11.mimba kutoka mara kwa mara.
Ikitokea mama kabeba mimba, hizo mimba utoka mara kwa mara na wakati mwingine mama anaweza kuangaika mpaka pale atakappgundua tatizo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mbegu ambazo ni nzima na ambazo zina sifa ya kutungisha mimba kwa hiyo mbegu hizi utazigundua kwa kuwa na sifa zifuatazo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupima mimba kwa kutumia chumvi sukari na sabuni
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba,Ni mambo ya kuzingatia ili mama akija kubeba mimba awe mzima kimwili, ki afya na kisaikolojia na hivyo hivyo Mtoto atakayezaliwa atakuwa salama.
Soma Zaidi...Tofauti na mambo matano yaliyotajwa hapo juu kuwa yanapelekea ujauzito kutoka, kuna mambo mengine ambayo yanaweza kuuweka ujauzito kuwa hatarini.
Soma Zaidi...DALILI KUU ZA MIMBA (UJAUZITO) Watu wengi sana wamekuwa wakilalamika kuwa mimba zao zinatoka, ama kupotea bila ya kujulikana tatizo wala bila ya kuugua.
Soma Zaidi...