Dalili za uvimbe kwenye kizazi
Posti hii inahusu zaidi Dalili za uvimbe kwenye kizazi,hizi ni Dalili ambazo ujitokeza kwa akina mama ambao wana uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo endapo mama ameona Dalili kama hizi anapaswa kuwahi hospitali mara moja kwa uangalizi zaidi.
Dalili za uvimbe kwenye kizazi.
1. Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi.
Hii ni Dalili mojawapo ambayo inaweza kujitokeza kwa Mama au msichana ambaye hajaolewa, ikitokea damu ikaongezeka kupita kiasi kusiko kwa kawaida wakati wa hedhi ni Dalili mojawapo ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
2. Maumivu makali wakati wa hedhi.
Kwa wakati mwingine maumivu yanaweza kuwa makali kuliko kawaida au mtu mwingine anakuwa hana maumivu wakati wa hedhi ila ikitokea shida hizi ya kuwepo kwa uvimbe maumivu yanaanza kuwepo.
3. Kuvimba miguu.
Nayo ni Dalili ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi utaona mama au mdada yeyote amevimba miguu kwa hiyo anapaswa kwenda hospitalini kupima.
4. Maumivu wakati wa tendo la ndoa.
Kwa wenye matatizo ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi wanapatwa na maumivu wakati wa tendo la ndoa na kwa hiyo huwa hawana furaha wakati wa tendo ila ni maumivu tu.
5. Kuwepo kwa gesi tumboni .
Au kwa wakati mwingine mtu ujisikia kama amevimbiwa na tumbo linakaa limevimba kama vile linakuwa na gesi.
6. Kupata choo kigumu au kufunga choo kabisa .
Kwa kawaida mtu mwenye matatizo ya kuwepo kwa uvimbe huwa na matatizo ya kukosa choo na huko anakuwa anakula chakula kawaida na kwa wakati mwingine anahisi kwenda haja kubwa ila choo kigumu nakuwa kama kigumu sana.
7. Maumivu n kwenye mgongo.
Hili tatizo uwapata wanawake walio wengi na udhani ni mgongo inauma lakini baada ya kufanyiwa upasuaji na kutoa uvimbe kwenye kizazi maumivu haya hayatokeagi tena.
8. Maumivu kwenye miguu na miguu kuvimba.
Kwa wakati mwingine Maumivu yanakiwepo kwenye miguu na miguu uanza kuvimba .
9. Kuwepo kwa ugumba au uzazi wa shida.
Kwa wakati mwingine wa mama wengi wanaangalia kutafuta watoto na hawapati shida kubwa inakuwa kwenye kizazi na wakifanyiwa upasuaji wanaweza kupata watoto.
10. Maumivu kwenye nyonga.
Kwa wakati mwingine mama huwa anapata maumivu makali kwenye nyonga ambayo umfanya mama kulalamika kila wakati.
11.mimba kutoka mara kwa mara.
Ikitokea mama kabeba mimba, hizo mimba utoka mara kwa mara na wakati mwingine mama anaweza kuangaika mpaka pale atakappgundua tatizo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 web hosting 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 ai web app 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Madhara ya kupungua kwa homoni ya projestron
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa homoni ya projestron ikipungua mwilini na pia kuweza kutambua dalili za kupungua kwa homoni hii ya progesterone.
Soma Zaidi...Samahani nilikua naomba niulize swali mimi imepita miezi mitatu sioni hedhi na wala sioni dalili ya kuwa na mimba unaweza ukaniambia tatizo la kuwa na hali hii
Kama na wewe unasumbuliwa na hali ya kupitiliza siku zako post hii itakusaidia.
Soma Zaidi...Zifahamu sababu za kuziba kwa mrija wa kizazi.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuziba kwa mrija wa kizazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapian tube, ni sababu ambazo ufanya mirija ya follapian tube kuziba.
Soma Zaidi...Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa
Utajifunza sababua zinazopelekea kuhisi maumivu makali ya tumbo baada ya kumaliza tendo la ndoa
Soma Zaidi...