Dalili za uvimbe kwenye kizazi
Posti hii inahusu zaidi Dalili za uvimbe kwenye kizazi,hizi ni Dalili ambazo ujitokeza kwa akina mama ambao wana uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo endapo mama ameona Dalili kama hizi anapaswa kuwahi hospitali mara moja kwa uangalizi zaidi.
Dalili za uvimbe kwenye kizazi.
1. Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi.
Hii ni Dalili mojawapo ambayo inaweza kujitokeza kwa Mama au msichana ambaye hajaolewa, ikitokea damu ikaongezeka kupita kiasi kusiko kwa kawaida wakati wa hedhi ni Dalili mojawapo ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
2. Maumivu makali wakati wa hedhi.
Kwa wakati mwingine maumivu yanaweza kuwa makali kuliko kawaida au mtu mwingine anakuwa hana maumivu wakati wa hedhi ila ikitokea shida hizi ya kuwepo kwa uvimbe maumivu yanaanza kuwepo.
3. Kuvimba miguu.
Nayo ni Dalili ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi utaona mama au mdada yeyote amevimba miguu kwa hiyo anapaswa kwenda hospitalini kupima.
4. Maumivu wakati wa tendo la ndoa.
Kwa wenye matatizo ya kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi wanapatwa na maumivu wakati wa tendo la ndoa na kwa hiyo huwa hawana furaha wakati wa tendo ila ni maumivu tu.
5. Kuwepo kwa gesi tumboni .
Au kwa wakati mwingine mtu ujisikia kama amevimbiwa na tumbo linakaa limevimba kama vile linakuwa na gesi.
6. Kupata choo kigumu au kufunga choo kabisa .
Kwa kawaida mtu mwenye matatizo ya kuwepo kwa uvimbe huwa na matatizo ya kukosa choo na huko anakuwa anakula chakula kawaida na kwa wakati mwingine anahisi kwenda haja kubwa ila choo kigumu nakuwa kama kigumu sana.
7. Maumivu n kwenye mgongo.
Hili tatizo uwapata wanawake walio wengi na udhani ni mgongo inauma lakini baada ya kufanyiwa upasuaji na kutoa uvimbe kwenye kizazi maumivu haya hayatokeagi tena.
8. Maumivu kwenye miguu na miguu kuvimba.
Kwa wakati mwingine Maumivu yanakiwepo kwenye miguu na miguu uanza kuvimba .
9. Kuwepo kwa ugumba au uzazi wa shida.
Kwa wakati mwingine wa mama wengi wanaangalia kutafuta watoto na hawapati shida kubwa inakuwa kwenye kizazi na wakifanyiwa upasuaji wanaweza kupata watoto.
10. Maumivu kwenye nyonga.
Kwa wakati mwingine mama huwa anapata maumivu makali kwenye nyonga ambayo umfanya mama kulalamika kila wakati.
11.mimba kutoka mara kwa mara.
Ikitokea mama kabeba mimba, hizo mimba utoka mara kwa mara na wakati mwingine mama anaweza kuangaika mpaka pale atakappgundua tatizo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 web hosting 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
MAUMIVU WAKATI WA TENDO LA NDOA
Maumivu wakati wa tendo la ndoa kitaalamu huitwa dyspareunia.
Soma Zaidi...Nia za kupima ujauzito ukiwa nyumbani, Njia kuu 10 za kiasili za kupima mimba changa
Kuna njia nyingi zinatajwa zinapima mimba kama chumvi, sukari, mafuta na sabuni. Hata hivyo zipo njia zaidi ya 10 za kiasili za kupima ujauzito. Utajifunza hapa zote
Soma Zaidi...Umuhimu wa uzazi wa mpango kwa Mama
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.
Soma Zaidi...Mambo yanayopunguza nguvu za kiume
Posti hii inaelezea kuhusiana na nguvu za kiume zinavyopungua na Ni Mambo gani yanayofanya zipungue
Soma Zaidi...Imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba
Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...