Vyanzo vya kuharibika kwa mimba ya miezi kuanzia 0-3
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu, kwa sababu hii ni miezi ya kwanza kabisa Kuna sababu au vyanzo vya kuharibika kwa mimba katika kipindi hiki.
Vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu.
1. Sababu ya kwanza ni kitendo cha homoni kutokuwa sawa kwa sababu katika kipindi hiki ni wakati ambao homoni nyingi uwepo Ili kuhakikisha kazi mbalimbali zinafanyika kama vile kutengeneza kondo la nyuma kama homoni haziko sawa mimba inaweza kutoka.
2. Sababu za vinasa Saba
Hizi ni sababu ambazo uchangiwa na wazazi wenyewe anaweza kuwa baba au mama , ndio usababisha mimba kutoka kwa kipindi hiki.
3. Matumizi ya dawa kiholela.
Kuna tabia ya kutumia dawa kiholela bila kupata ushauri wa daktari katika kipindi hiki hasa akina Mama wengi uchanganya madawa Kuna madaw ya kienyeji na ya hospital hasa matumizi ya madawa ya malaria , usababisha mimba kutoka.
4. Maambukizi ya magonjwa.
Kuna tabia ya maambukizi ya magonjwa kama vile kisonono, kaswende na maambukizi kwenye mlango wa kizazi kama maambukizi haya hayakugundukika mapema na kitibiea usababisha mimba kutoka.
5. Pia Kuna maambukizi kwenye mfuko wa uzazi.
Kuna wakati mwingine maambukizi kwenye mfuko wa uzazi usababisha mimba kutoka kwa sababu unakuta sehemu mbalimbali za kizazi zimeshambuliwa hali ambayo usababisha mimba kutoka.
6. Kuwepo kwa uvimbe.
Pia na hili ni Mojawapo ya tatizo kwa Sababu kama kwenye mfuko wa uzazi Kuna uvimbe mama hawezi kubeba mtoto kwenye mfuko huo kwa sababu utakuta uvimbe huo unashika sehemu mbalimbali ambapo mtoto anapaswa kuwepo.
7. Uvutaji wa sigara kupita kiasi na unywaji wa pombe kupita kiasi usababisha mimba kutoka kwa sababu ya kuwepo kwa nicotine na kemikali mbalimbali za pombe.
8. Kufanya kazi ngumu na kubeba mizigo mizito.
Pia kazi ngumu Nazo usababisha kutoka kwa mimba kwa sababu ni vigumu kabisa mimba kustahimili kwa mama anayefanya kazi hizo ngumu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 web hosting 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Mabadiliko ya via vya uzazi kwa Mama mjamzito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye via vya uzazi kwa wajawazito, tunajua kuwa Mama akibeba mimba tu kuna mabadiliko utokea katika sehemu mbalimbali za mwili.
Soma Zaidi...Dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku ya 7 Hadi ya 14
Soma Zaidi...tuseme nilifanya ngono jana na leo nipata period,je kuna uwezekano wa kupata mimba
Mimba inatungwa katika siku maalumu na hazizidi 10. Sio kila ukishiriki tendo unaweza pata mimba. Je unaweza kupata mimba baada ya kushiriki tendo wiki moja kabla ya kuingia hedhi?
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kabla ya kupata hedhi
Je unasumbuliwa na maumivu ya tumbo. Unadhani ni dalili za mimba na ukapima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Je tumbo huanza kukua baada ya mda gan?
Ni Swali kila mjamzito anataka kujiuliza hasa akiwa katika mimba ya kwanza. Wengine wanataka kujuwa ni muda gani anujuwe mavazi makubwa. Kama na wewe unataka kujuwa muda ambao tumbo huwa kubwa, endelea kusoma.
Soma Zaidi...Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?
Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?
Soma Zaidi...