Sababu za kushuka surat al Zilzalah

surat Zalzalah ni sura ya 99 katika mpangilio wa Quran, na ina aya 8. Sura hii imeteremshwa Madina ila pia kuna kauli zinathibitisha kuwa ni ya Makkah. Katika hadithi iliyopewa daraja la hassan na Imam Tirmidh Mtume S.A.W amesema kuwa kusoa surat Zilzalah

Asbab Nuzul Surat Zilzalah

Ama kuhusu sababu za kushuka sura hii, hakuna nukuu za kutosha kuonyesha hasa tukio ambalo lilitokea hata sura hii ikashushwa. Hata hivyo kutokana na maelezo ya Sa'id bin Jubair ni kuwa baada ya kushuka aya ya 8 ya surat Al insan watu walidhani kuwa wak=liotoa sadaka kidogo sana hawatalipwa na wengine wakadhani kuwa dhambi ndogo wanazozifanya hawataadhibiwa, hivyo Allah akashuka aya 7 na 8 katika surat al zilzalah.

 

Kutokana na maelezo Maelezo ya Sura hii kuwa ukifanya dhambi iwe ndogo kiasi gani utalipwa malipo yake, na ukifanya wema mdogo kiasi gani pia utalipwa. Ama kuhusu wema kuna maelezo mengine zaidi ni kuwa Quran inasibitisha kuwa wema hulipwa kwa marakumi zaidi ama zaidi ya hapo. Yaani mfano umetenda wema mmoja, basi Allah atazidisha kwa kumi malipo yake. Na huwenda akazidisha zaidi ya hapo hata mara mia saba kama Surat Al Baqarah inavyoeleza ama zaidi na zaidi.

 

Imesimuliwa Kutoka kwa Abdallah Inb Umar kuwa wakati sura hii iliposhuka Abubakar alikuwa amekaa, basi akaanza kulia. Mtume S.A.W akamuuliza "nikipi kinachokuliza ewe Abubakar? " Abubakar akajibu " ni hii sura " basi Mtume wa Allah akasema "lau kama nyinyi mngelikuwa si wenye hamkosei na hamfanyi madhambi basi Allah angeumbwa umma mwingine baada yenu ambao watu wake wanakosea na wanafanya madhambi na kisha wanataka msamaha na Allah atawasamehe"  

 

KIPENGELE CHA TAWHID:

Sura hii ukiisoma kwa mazingatio Ina mambo mengi ya kiimani tunapasa kuyaweka katika fahami zetu:

1. Ardhi itatetemeshwa na itoe kila kilichomo ndani yake marehemu na hazina zilizomo

2. Mwanadamu atapata hofu sana na kujiuliza ina nini hii ardhi

3. Siku ya kiyama Ardhi itatoa siri zote, itatoa ushahidi wa kila wema na uovu uliofanywa na mtu katika ardhi.

4. Allah ameipa idhini Ardhi ianze kutoa habari. katika surat Yasin Allah anatujulisha kuwa siku ya kiyama midomo yetu haitafanya kazi, yaani haitazungumza, ila Allah atazungumzishwa viungo na viseme yaliyo ya kweli, viungo hivyo ni kama mikono, ngozi na vinginevyo. Hivyo hivyo ardhi nayo itapewa idhini ya kuzungumza kweli tupu kila kilichofanywa na mwanadamu iwe kidogo aka kikubwa.

5. basi mwenye kufanya wema ama uovu ulio mdogo kama dhara basi atalipwa kama ni wema kwa wema na kama ni uovu kwa adhabu. Neno dhara hili leo linatafsiriwa kwa maana ya atom. Atom ni chembe ndoogo sana ambayo huwezi kuiona kwa macho ya kawaida kwa udogo wake. Hii inamaanisha kuwa hata kama wema ni mdogo kiasi gani utalipwa na hata kama uovu ni mdogo kiasi gani pia utalipwa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2950

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Sababu za kushuka kwa surat An-Nasr (idhaa jaa)

SURATUN-NASR Sura hii imeteremka wakati Mtume (s.

Soma Zaidi...
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...
Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?

Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya id-gham katika hukumu za tajwid

Hapa utajifunza kuhusu maana ya id-ghamu na aina zake.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kulaaniwa Bani Israil

Pamoja na kuteuliwa na Allah(s.

Soma Zaidi...
Hukumu ya Ikhfau katika tajwid

Ikh-fau ni moja ya hukumu za nun sakina na tanwin kwenye hukumu za Quran tajwid

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Darsa za Quran

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...