Sababu za kushuka surat al Zilzalah

surat Zalzalah ni sura ya 99 katika mpangilio wa Quran, na ina aya 8. Sura hii imeteremshwa Madina ila pia kuna kauli zinathibitisha kuwa ni ya Makkah. Katika hadithi iliyopewa daraja la hassan na Imam Tirmidh Mtume S.A.W amesema kuwa kusoa surat Zilzalah

Asbab Nuzul Surat Zilzalah

Ama kuhusu sababu za kushuka sura hii, hakuna nukuu za kutosha kuonyesha hasa tukio ambalo lilitokea hata sura hii ikashushwa. Hata hivyo kutokana na maelezo ya Sa'id bin Jubair ni kuwa baada ya kushuka aya ya 8 ya surat Al insan watu walidhani kuwa wak=liotoa sadaka kidogo sana hawatalipwa na wengine wakadhani kuwa dhambi ndogo wanazozifanya hawataadhibiwa, hivyo Allah akashuka aya 7 na 8 katika surat al zilzalah.

 

Kutokana na maelezo Maelezo ya Sura hii kuwa ukifanya dhambi iwe ndogo kiasi gani utalipwa malipo yake, na ukifanya wema mdogo kiasi gani pia utalipwa. Ama kuhusu wema kuna maelezo mengine zaidi ni kuwa Quran inasibitisha kuwa wema hulipwa kwa marakumi zaidi ama zaidi ya hapo. Yaani mfano umetenda wema mmoja, basi Allah atazidisha kwa kumi malipo yake. Na huwenda akazidisha zaidi ya hapo hata mara mia saba kama Surat Al Baqarah inavyoeleza ama zaidi na zaidi.

 

Imesimuliwa Kutoka kwa Abdallah Inb Umar kuwa wakati sura hii iliposhuka Abubakar alikuwa amekaa, basi akaanza kulia. Mtume S.A.W akamuuliza "nikipi kinachokuliza ewe Abubakar? " Abubakar akajibu " ni hii sura " basi Mtume wa Allah akasema "lau kama nyinyi mngelikuwa si wenye hamkosei na hamfanyi madhambi basi Allah angeumbwa umma mwingine baada yenu ambao watu wake wanakosea na wanafanya madhambi na kisha wanataka msamaha na Allah atawasamehe"  

 

KIPENGELE CHA TAWHID:

Sura hii ukiisoma kwa mazingatio Ina mambo mengi ya kiimani tunapasa kuyaweka katika fahami zetu:

1. Ardhi itatetemeshwa na itoe kila kilichomo ndani yake marehemu na hazina zilizomo

2. Mwanadamu atapata hofu sana na kujiuliza ina nini hii ardhi

3. Siku ya kiyama Ardhi itatoa siri zote, itatoa ushahidi wa kila wema na uovu uliofanywa na mtu katika ardhi.

4. Allah ameipa idhini Ardhi ianze kutoa habari. katika surat Yasin Allah anatujulisha kuwa siku ya kiyama midomo yetu haitafanya kazi, yaani haitazungumza, ila Allah atazungumzishwa viungo na viseme yaliyo ya kweli, viungo hivyo ni kama mikono, ngozi na vinginevyo. Hivyo hivyo ardhi nayo itapewa idhini ya kuzungumza kweli tupu kila kilichofanywa na mwanadamu iwe kidogo aka kikubwa.

5. basi mwenye kufanya wema ama uovu ulio mdogo kama dhara basi atalipwa kama ni wema kwa wema na kama ni uovu kwa adhabu. Neno dhara hili leo linatafsiriwa kwa maana ya atom. Atom ni chembe ndoogo sana ambayo huwezi kuiona kwa macho ya kawaida kwa udogo wake. Hii inamaanisha kuwa hata kama wema ni mdogo kiasi gani utalipwa na hata kama uovu ni mdogo kiasi gani pia utalipwa.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2608

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

As-Sab nuzul

Sababu za kuteremshwa baadhi ya sura Katika darsa hii tutaangalia sababu za kushuka kwa aya na sura ndani ya quran.

Soma Zaidi...
Ni ipi aya ya mwisho kushuka katika Quran?

Maulamaa katika elimu ya Quran wametofautiana juu ya aya ya mwisho kushuka. Hata hivyo hapa nitakutajia ambayo imependekezwa zaidi

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al-Fiyl

Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat At-Takaathur

Wanazuoni wengi zaidi wanakubaliana ya kuwa sura hii surat At-Takaathur ilishuka Makka, na hizi ndio sababu za kushuka kwa sura hii

Soma Zaidi...
Quran si njozi za mvurugano alizoota Mtume Muhammad

(ii)Dai kuwa Qur-an ni zao la njozi za Mtume (s.

Soma Zaidi...
Hukumu za Tajwid katika usomaji wa bismillah (basmalah)

Hapa utajifunza kanuni za tajwid katika kusoma bismillah au basmalah.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al qadir

Asbab nuzul surat al qadi. Hii ni sura ya 97 katika mpangilio wa mashaf. Surat al qadir imeteremshwa Madina na ina aya 5.

Soma Zaidi...