Tafsiri na mafunzo ya sura zilizochaguliwa - Saratul-fiyl
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)
6.2. Tafsiri na Mafunzo ya Sura Zilizochaguliwa.
- Suratul-Fiyl (105): Imeteremshwa Makkah, Ina Aya Tano.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
- Jee, huoni jinsi Mola wako alivyowafanya watu wa ndovu (tembo)?
- Jee, hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
- Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi.
- Wakawapiga kwa vijiwe vya udongo wa motoni.
- Akawafanya kama majani yaliyoliwa (na kutemwa).
Mafunzo kwa Ufupi.
- Mwenyezi Mungu (s.w) ni Muweza wa kila kitu.
- Viumbe vyote viko katika Milki ya Mwenyezi Mungu (s.w) na ni Majeshi yake yaliyotayari kumtumikia ipasavyo.
- Nusura na Msaada wa Mwenyezi Mungu (s.w) hupatikana muda wowote watu watakapomuamini na kumtegemea ipasavyo.
- Kuangamizwa kwa Abraha na jeshi lake na Jeshi asilolijua wala kulitegemea ni dalili ya Kuwepo Mwenyezi Mungu (s.w).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 web hosting 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Sababu za kushuka surat at Takaathur
Kuwa na tamaa huhitaji vitu vya watu si jambo jema. Ila kama tamaa hii itakuhamasisha na wewe kutafuta kitu hicho, kwa uwezo ambao Allah amekupa bila ha kuvuka mipaka yake, hili sio tatizo. Sura hii itakufundisha mengi
Soma Zaidi...KISA CHA TEMBO KATIKA QURAN, KUHUSU ABRAHA KUTAKA KUVUNJA AL-KABA NYUMBBA YA aLLAH
KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji.
Soma Zaidi...surat al mauun
SURATUL-MAM’UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat..
Soma Zaidi...Nini maana ya Iqlab katika hukumu za tajwid
Hapa utajifunza maana ya iqlab katika usomaji wa Quran kwa tajwid
Soma Zaidi...Sababu za kshuka surat al Asr
Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo…
Soma Zaidi...