Sababu za kushuka surat al bayyinah

Sababu za kushuka surat al bayyinah

Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Surat al bayyinah imeshuka Madina kwa maelezo ya Jamhuri ya wanazuoni akiwemo Ibn Abas.   Hata hivyo wapo ambao wamesema imeshuka Makka kwa kauli ya Yahya Ibn Sallaam (Tafsir qurtub). 

 

Sura hii iliposhuka Mtume s. a.w aliamrishwa amsomee Ubayya. 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ لِأُبَيِّ بْنِ كَعْبٍ: "إِنَّ اللَّهَ أَمَرَنِي أَنْ أَقْرَأَ عَلَيْكَ: " لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَرُوا " قَالَ: وَسَمَّانِي لَكَ؟ قَالَ: "نَعَمْ". فَبَكَى.
وَرَوَاهُ الْبُخَارِيُّ، وَمُسْلِمٌ، وَالتِّرْمِذِيُّ، وَالنَّسَائِيُّ، مِنْ حَدِيثِ شُعْبَةَ، بِهِ  .

 

Imepokewa hadithi kutoka kwa Anas Ibn Malik kuwa amesema Mtume s.a. w kumwambia Ubayya Ibn Ka‘ab "Hakika Allah ameniamuru nikusomee (sura hii)  lam yakun ladhiina kafaruu" akasema Ubayya "na nimetajwa kwa jina? " akasema Mtume "naam" hapo akalia kwa furaha (Bukhari na Muslim). 

 

Sababu za kushuka sura hii

Hakuna tukio maalumu lilopelekea kushuka sura hii. Hata hivyo sura ipo wazi inaonyesha dhahiri kike ambacho kilikuwa kikiaminiwa na ahalul kitab na washirikina. 

 

Sura inaeleza kuwa hapo awali Ahalul kitab na washirikina walikuwa wakiamini kuwa atakuja mtume wa Mwisho. Mahubiri haya yalikuwa yakitolewa na Mayahudi na Wakristo kuwaambia waumini wao na waarabu. 

 

Lakini Mtume wa mwisho alipokuja wakamkataa na kumpinga. Alikuwa wakipinga ukweli kwa sababu ya chuki zao. 

Allah anasema katika sura hii: - 

(وَمَا تَفَرَّقَ ٱلَّذِینَ أُوتُوا۟ ٱلۡكِتَـٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَاۤءَتۡهُمُ ٱلۡبَیِّنَةُ)
[Surah Al-Bayyinah 4]

Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana.

 

Mwisho kwa uovu huu wa kufarikiana na haki baada ya kuwajia bayana (uwazi na ukweli wa mambo) Allah amewaahidi kukaa maisha ya Motoni milele. 

 

Fadhila za sura hii

kuhusu fadhila za sura hii,  kuna hadithi nyingi lakini zinatikiwa shaka usahihi wake. Miongoni mwazo kuna inayosema kuwa sura hii haisomwi na mtu mnafiki wala mtu ambaye ana shaka juu ya Mwenyezi Mungu na kuwa Malaika wanaosoma sura hii na mwenye kuisoma Allah atampa Malaina wamuhifadhi…. Hadithi hii sio sahihi. Angalia Matini ya hadithi hapo chini. 

 

عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى الله: (لو يعلم الناس ما في [لَمْ يَكُنِ [الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ،، لَعَطَّلُوا الْأَهْلَ وَالْمَالَ، فَتَعَلَّمُوهَا) فَقَالَ رَجُلٌ مِنْ خُزَاعَةَ: وَمَا فِيهَا مِنَ الْأَجْرِ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟ قَالَ: (لَا يَقْرَؤُهَا مُنَافِقٌ أَبَدًا، وَلَا عَبْدٌ فِي قَلْبِهِ شَكٌّ فِي اللَّهِ. وَاللَّهِ إِنَّ الْمَلَائِكَةَ المقربين يقرءونها  Ù…نذ خلق الله السموات وَالْأَرْضَ مَا يَفْتُرُونَ مِنْ قِرَاءَتِهَا. وَمَا مِنْ عَبْدٍ يَقْرَؤُهَا إِلَّا بَعَثَ اللَّهُ إِلَيْهِ مَلَائِكَةً يَحْفَظُونَهُ فِي دِينِهِ وَدُنْيَاهُ، وَيَدْعُونَ لَهُ بِالْمَغْفِرَةِ وَالرَّحْمَةِ (. قَالَ الْحَضْرَمِيُّ: فَجِئْتُ إِلَى أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ نُمَيْرٍ، فَأَلْقَيْتُ هَذَا الْحَدِيثَ عَلَيْهِ، فقال: هذا قَدْ كَفَانَا مَئُونَتَهُ، فَلَا تَعُدْ إِلَيْهِ. قَالَ ابْنُ الْعَرَبِيِّ:" رَوَى إِسْحَاقُ بْنُ بِشْرٍ الْكَاهِلِيُّ عن مالك ابن أَنَسٍ، عَنْ يَحْيَى بْنِ سَعِيدٍ، عَنِ ابْنِ الْمُسَيَّبِ: عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، عَنِ النَّبِيِّ ï·º: (لَوْ يَعْلَمُ النَّاسُ مَا فِي [لَمْ يَكُنْ [الَّذِينَ كَفَرُوا لَعَطَّلُوا الْأَهْلَ وَالْمَالَ وَلَتَعَلَّمُوهَا) . حَدِيثٌ بَاطِلٌ

Angalia Tafsir Qurtub

 

Khabari njema kwa waumini

Mwisho sura inatia habari za furaha kuwa waliamini na kufanya vitendo vizuri yaani amali njema malipo yao ni pepo na wakae humo milele. 

 

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2674

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa
Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa

Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya.

Soma Zaidi...
mgawanyiko katika quran
mgawanyiko katika quran

MGAWANYIKO KATIKA QURAN Juzuu, Sura, Aya, Manzil, Qara Wataalamu wa elimu za Qurani katika fani za uandishi na usomaji wameigawanya Qurani katika mafungu ili kuwezesha urahisi kwa wasomaji wa qurani.

Soma Zaidi...
Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?
Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?

Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet

Soma Zaidi...
IDGHAAM KATIKA LAAM
IDGHAAM KATIKA LAAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Aina saba za Viraa vya usomaji wa Quran
Aina saba za Viraa vya usomaji wa Quran

Post hii inakwenda kukuorodheshea aina saba za viraka vya usomaji wa Quran.

Soma Zaidi...
Fadhila za kusoma surat al Kahaf siku ya Ijumaa
Fadhila za kusoma surat al Kahaf siku ya Ijumaa

Je unajuwa ni kwa nini unatakiwa usikose kusoma surat al Kahaf siku ya ijumaa. Makala hii itakujibu swali hili

Soma Zaidi...