Sababu za kushuka surat al bayyinah

Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane.

Surat al bayyinah imeshuka Madina kwa maelezo ya Jamhuri ya wanazuoni akiwemo Ibn Abas.   Hata hivyo wapo ambao wamesema imeshuka Makka kwa kauli ya Yahya Ibn Sallaam (Tafsir qurtub). 

 

Sura hii iliposhuka Mtume s. a.w aliamrishwa amsomee Ubayya. 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ لِأُبَيِّ بْنِ كَعْبٍ: "إِنَّ اللَّهَ أَمَرَنِي أَنْ أَقْرَأَ عَلَيْكَ: " لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَرُوا " قَالَ: وَسَمَّانِي لَكَ؟ قَالَ: "نَعَمْ". فَبَكَى.
وَرَوَاهُ الْبُخَارِيُّ، وَمُسْلِمٌ، وَالتِّرْمِذِيُّ، وَالنَّسَائِيُّ، مِنْ حَدِيثِ شُعْبَةَ، بِهِ  .

 

Imepokewa hadithi kutoka kwa Anas Ibn Malik kuwa amesema Mtume s.a. w kumwambia Ubayya Ibn Ka‘ab "Hakika Allah ameniamuru nikusomee (sura hii)  lam yakun ladhiina kafaruu" akasema Ubayya "na nimetajwa kwa jina? " akasema Mtume "naam" hapo akalia kwa furaha (Bukhari na Muslim). 

 

Sababu za kushuka sura hii

Hakuna tukio maalumu lilopelekea kushuka sura hii. Hata hivyo sura ipo wazi inaonyesha dhahiri kike ambacho kilikuwa kikiaminiwa na ahalul kitab na washirikina. 

 

Sura inaeleza kuwa hapo awali Ahalul kitab na washirikina walikuwa wakiamini kuwa atakuja mtume wa Mwisho. Mahubiri haya yalikuwa yakitolewa na Mayahudi na Wakristo kuwaambia waumini wao na waarabu. 

 

Lakini Mtume wa mwisho alipokuja wakamkataa na kumpinga. Alikuwa wakipinga ukweli kwa sababu ya chuki zao. 

Allah anasema katika sura hii: - 

(وَمَا تَفَرَّقَ ٱلَّذِینَ أُوتُوا۟ ٱلۡكِتَـٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَاۤءَتۡهُمُ ٱلۡبَیِّنَةُ)
[Surah Al-Bayyinah 4]

Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana.

 

Mwisho kwa uovu huu wa kufarikiana na haki baada ya kuwajia bayana (uwazi na ukweli wa mambo) Allah amewaahidi kukaa maisha ya Motoni milele. 

 

Fadhila za sura hii

kuhusu fadhila za sura hii,  kuna hadithi nyingi lakini zinatikiwa shaka usahihi wake. Miongoni mwazo kuna inayosema kuwa sura hii haisomwi na mtu mnafiki wala mtu ambaye ana shaka juu ya Mwenyezi Mungu na kuwa Malaika wanaosoma sura hii na mwenye kuisoma Allah atampa Malaina wamuhifadhi…. Hadithi hii sio sahihi. Angalia Matini ya hadithi hapo chini. 

 

عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى الله: (لو يعلم الناس ما في [لَمْ يَكُنِ [الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ،، لَعَطَّلُوا الْأَهْلَ وَالْمَالَ، فَتَعَلَّمُوهَا) فَقَالَ رَجُلٌ مِنْ خُزَاعَةَ: وَمَا فِيهَا مِنَ الْأَجْرِ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟ قَالَ: (لَا يَقْرَؤُهَا مُنَافِقٌ أَبَدًا، وَلَا عَبْدٌ فِي قَلْبِهِ شَكٌّ فِي اللَّهِ. وَاللَّهِ إِنَّ الْمَلَائِكَةَ المقربين يقرءونها  Ù…نذ خلق الله السموات وَالْأَرْضَ مَا يَفْتُرُونَ مِنْ قِرَاءَتِهَا. وَمَا مِنْ عَبْدٍ يَقْرَؤُهَا إِلَّا بَعَثَ اللَّهُ إِلَيْهِ مَلَائِكَةً يَحْفَظُونَهُ فِي دِينِهِ وَدُنْيَاهُ، وَيَدْعُونَ لَهُ بِالْمَغْفِرَةِ وَالرَّحْمَةِ (. قَالَ الْحَضْرَمِيُّ: فَجِئْتُ إِلَى أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ نُمَيْرٍ، فَأَلْقَيْتُ هَذَا الْحَدِيثَ عَلَيْهِ، فقال: هذا قَدْ كَفَانَا مَئُونَتَهُ، فَلَا تَعُدْ إِلَيْهِ. قَالَ ابْنُ الْعَرَبِيِّ:" رَوَى إِسْحَاقُ بْنُ بِشْرٍ الْكَاهِلِيُّ عن مالك ابن أَنَسٍ، عَنْ يَحْيَى بْنِ سَعِيدٍ، عَنِ ابْنِ الْمُسَيَّبِ: عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، عَنِ النَّبِيِّ ï·º: (لَوْ يَعْلَمُ النَّاسُ مَا فِي [لَمْ يَكُنْ [الَّذِينَ كَفَرُوا لَعَطَّلُوا الْأَهْلَ وَالْمَالَ وَلَتَعَلَّمُوهَا) . حَدِيثٌ بَاطِلٌ

Angalia Tafsir Qurtub

 

Khabari njema kwa waumini

Mwisho sura inatia habari za furaha kuwa waliamini na kufanya vitendo vizuri yaani amali njema malipo yao ni pepo na wakae humo milele. 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 3059

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 web hosting    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Quran na sayansi

3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran??

Soma Zaidi...
Hoja juu ya kukubalika hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa

Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya.

Soma Zaidi...
HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA QALQALA

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Quran Tafsiri kwa Kiswahili

Tafsiri ya quran kw akiswahili, imeandikw ana Shekh Ali Muhsin al-Barwani

Soma Zaidi...
Adabu za kusikiliza quran

ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Fatiha

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu srat al fatiha, faida zake na maudhui zake

Soma Zaidi...