Sababu za kushuka surat al bayyinah

Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane.

Surat al bayyinah imeshuka Madina kwa maelezo ya Jamhuri ya wanazuoni akiwemo Ibn Abas.   Hata hivyo wapo ambao wamesema imeshuka Makka kwa kauli ya Yahya Ibn Sallaam (Tafsir qurtub). 

 

Sura hii iliposhuka Mtume s. a.w aliamrishwa amsomee Ubayya. 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ لِأُبَيِّ بْنِ كَعْبٍ: "إِنَّ اللَّهَ أَمَرَنِي أَنْ أَقْرَأَ عَلَيْكَ: " لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَرُوا " قَالَ: وَسَمَّانِي لَكَ؟ قَالَ: "نَعَمْ". فَبَكَى.
وَرَوَاهُ الْبُخَارِيُّ، وَمُسْلِمٌ، وَالتِّرْمِذِيُّ، وَالنَّسَائِيُّ، مِنْ حَدِيثِ شُعْبَةَ، بِهِ  .

 

Imepokewa hadithi kutoka kwa Anas Ibn Malik kuwa amesema Mtume s.a. w kumwambia Ubayya Ibn Ka‘ab "Hakika Allah ameniamuru nikusomee (sura hii)  lam yakun ladhiina kafaruu" akasema Ubayya "na nimetajwa kwa jina? " akasema Mtume "naam" hapo akalia kwa furaha (Bukhari na Muslim). 

 

Sababu za kushuka sura hii

Hakuna tukio maalumu lilopelekea kushuka sura hii. Hata hivyo sura ipo wazi inaonyesha dhahiri kike ambacho kilikuwa kikiaminiwa na ahalul kitab na washirikina. 

 

Sura inaeleza kuwa hapo awali Ahalul kitab na washirikina walikuwa wakiamini kuwa atakuja mtume wa Mwisho. Mahubiri haya yalikuwa yakitolewa na Mayahudi na Wakristo kuwaambia waumini wao na waarabu. 

 

Lakini Mtume wa mwisho alipokuja wakamkataa na kumpinga. Alikuwa wakipinga ukweli kwa sababu ya chuki zao. 

Allah anasema katika sura hii: - 

(وَمَا تَفَرَّقَ ٱلَّذِینَ أُوتُوا۟ ٱلۡكِتَـٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَاۤءَتۡهُمُ ٱلۡبَیِّنَةُ)
[Surah Al-Bayyinah 4]

Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana.

 

Mwisho kwa uovu huu wa kufarikiana na haki baada ya kuwajia bayana (uwazi na ukweli wa mambo) Allah amewaahidi kukaa maisha ya Motoni milele. 

 

Fadhila za sura hii

kuhusu fadhila za sura hii,  kuna hadithi nyingi lakini zinatikiwa shaka usahihi wake. Miongoni mwazo kuna inayosema kuwa sura hii haisomwi na mtu mnafiki wala mtu ambaye ana shaka juu ya Mwenyezi Mungu na kuwa Malaika wanaosoma sura hii na mwenye kuisoma Allah atampa Malaina wamuhifadhi…. Hadithi hii sio sahihi. Angalia Matini ya hadithi hapo chini. 

 

عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى الله: (لو يعلم الناس ما في [لَمْ يَكُنِ [الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ،، لَعَطَّلُوا الْأَهْلَ وَالْمَالَ، فَتَعَلَّمُوهَا) فَقَالَ رَجُلٌ مِنْ خُزَاعَةَ: وَمَا فِيهَا مِنَ الْأَجْرِ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟ قَالَ: (لَا يَقْرَؤُهَا مُنَافِقٌ أَبَدًا، وَلَا عَبْدٌ فِي قَلْبِهِ شَكٌّ فِي اللَّهِ. وَاللَّهِ إِنَّ الْمَلَائِكَةَ المقربين يقرءونها  Ù…نذ خلق الله السموات وَالْأَرْضَ مَا يَفْتُرُونَ مِنْ قِرَاءَتِهَا. وَمَا مِنْ عَبْدٍ يَقْرَؤُهَا إِلَّا بَعَثَ اللَّهُ إِلَيْهِ مَلَائِكَةً يَحْفَظُونَهُ فِي دِينِهِ وَدُنْيَاهُ، وَيَدْعُونَ لَهُ بِالْمَغْفِرَةِ وَالرَّحْمَةِ (. قَالَ الْحَضْرَمِيُّ: فَجِئْتُ إِلَى أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ نُمَيْرٍ، فَأَلْقَيْتُ هَذَا الْحَدِيثَ عَلَيْهِ، فقال: هذا قَدْ كَفَانَا مَئُونَتَهُ، فَلَا تَعُدْ إِلَيْهِ. قَالَ ابْنُ الْعَرَبِيِّ:" رَوَى إِسْحَاقُ بْنُ بِشْرٍ الْكَاهِلِيُّ عن مالك ابن أَنَسٍ، عَنْ يَحْيَى بْنِ سَعِيدٍ، عَنِ ابْنِ الْمُسَيَّبِ: عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، عَنِ النَّبِيِّ ï·º: (لَوْ يَعْلَمُ النَّاسُ مَا فِي [لَمْ يَكُنْ [الَّذِينَ كَفَرُوا لَعَطَّلُوا الْأَهْلَ وَالْمَالَ وَلَتَعَلَّمُوهَا) . حَدِيثٌ بَاطِلٌ

Angalia Tafsir Qurtub

 

Khabari njema kwa waumini

Mwisho sura inatia habari za furaha kuwa waliamini na kufanya vitendo vizuri yaani amali njema malipo yao ni pepo na wakae humo milele. 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2912

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Sababu za kushuka kwa Surat At-Takaathur

Wanazuoni wengi zaidi wanakubaliana ya kuwa sura hii surat At-Takaathur ilishuka Makka, na hizi ndio sababu za kushuka kwa sura hii

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka Surat al fatiha (Alhamdu)

Kwa kuwa hakuna sababu mwalumu ikiyonukuliwa kuwa ndio chanzo cha kushushwa suravhii. Basi post hii itakujuza mambo ambayo huwenda hukuyajuwa kuhusu fadhika za surabhii na mengineyo.

Soma Zaidi...
Utofauti wa Quran na hadithi Al Quds

Has utakwenda kujifunza utofauti was Hadithi Al Quds na Quran

Soma Zaidi...
HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Saratul-asr 103

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Mauun

Sura hii ni katika sura ambazo zinahitaji kusomwa kwa mazingatio sana. Wanaoswali bila ya kuzingatia swala zao, wameonywa vikali sana. Wanaowatesa na kuwanyanyasa mayatima wameonywa vikali. Wanaowanyima wenye haja na masikini huku wakiwakaripia nakuwasem

Soma Zaidi...
Fadhila za kusoma surat al Fatiha (Alhamdu)

Post hii inakwenda kufundisha fadhila na faida za kusoma Alhamdu.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat Dhuha

Sura hii imetermka Makkah na ina aya 11. Sura hii ni moja ya sura ambazo zimeshuka mwanzoni wakati ambapo Mtume ameanza kazi ya utume.

Soma Zaidi...