Sababu za kushuka surat al bayyinah


image


Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane.


Surat al bayyinah imeshuka Madina kwa maelezo ya Jamhuri ya wanazuoni akiwemo Ibn Abas.   Hata hivyo wapo ambao wamesema imeshuka Makka kwa kauli ya Yahya Ibn Sallaam (Tafsir qurtub). 

 

Sura hii iliposhuka Mtume s. a.w aliamrishwa amsomee Ubayya. 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ لِأُبَيِّ بْنِ كَعْبٍ: "إِنَّ اللَّهَ أَمَرَنِي أَنْ أَقْرَأَ عَلَيْكَ: " لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَرُوا " قَالَ: وَسَمَّانِي لَكَ؟ قَالَ: "نَعَمْ". فَبَكَى.
وَرَوَاهُ الْبُخَارِيُّ، وَمُسْلِمٌ، وَالتِّرْمِذِيُّ، وَالنَّسَائِيُّ، مِنْ حَدِيثِ شُعْبَةَ، بِهِ  .

 

Imepokewa hadithi kutoka kwa Anas Ibn Malik kuwa amesema Mtume s.a. w kumwambia Ubayya Ibn Ka‘ab "Hakika Allah ameniamuru nikusomee (sura hii)  lam yakun ladhiina kafaruu" akasema Ubayya "na nimetajwa kwa jina? " akasema Mtume "naam" hapo akalia kwa furaha (Bukhari na Muslim). 

 

Sababu za kushuka sura hii

Hakuna tukio maalumu lilopelekea kushuka sura hii. Hata hivyo sura ipo wazi inaonyesha dhahiri kike ambacho kilikuwa kikiaminiwa na ahalul kitab na washirikina. 

 

Sura inaeleza kuwa hapo awali Ahalul kitab na washirikina walikuwa wakiamini kuwa atakuja mtume wa Mwisho. Mahubiri haya yalikuwa yakitolewa na Mayahudi na Wakristo kuwaambia waumini wao na waarabu. 

 

Lakini Mtume wa mwisho alipokuja wakamkataa na kumpinga. Alikuwa wakipinga ukweli kwa sababu ya chuki zao. 

Allah anasema katika sura hii: - 

(وَمَا تَفَرَّقَ ٱلَّذِینَ أُوتُوا۟ ٱلۡكِتَـٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَاۤءَتۡهُمُ ٱلۡبَیِّنَةُ)
[Surah Al-Bayyinah 4]

Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana.

 

Mwisho kwa uovu huu wa kufarikiana na haki baada ya kuwajia bayana (uwazi na ukweli wa mambo) Allah amewaahidi kukaa maisha ya Motoni milele. 

 

Fadhila za sura hii

kuhusu fadhila za sura hii,  kuna hadithi nyingi lakini zinatikiwa shaka usahihi wake. Miongoni mwazo kuna inayosema kuwa sura hii haisomwi na mtu mnafiki wala mtu ambaye ana shaka juu ya Mwenyezi Mungu na kuwa Malaika wanaosoma sura hii na mwenye kuisoma Allah atampa Malaina wamuhifadhi…. Hadithi hii sio sahihi. Angalia Matini ya hadithi hapo chini. 

 

عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى الله: (لو يعلم الناس ما في [لَمْ يَكُنِ [الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ،، لَعَطَّلُوا الْأَهْلَ وَالْمَالَ، فَتَعَلَّمُوهَا) فَقَالَ رَجُلٌ مِنْ خُزَاعَةَ: وَمَا فِيهَا مِنَ الْأَجْرِ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟ قَالَ: (لَا يَقْرَؤُهَا مُنَافِقٌ أَبَدًا، وَلَا عَبْدٌ فِي قَلْبِهِ شَكٌّ فِي اللَّهِ. وَاللَّهِ إِنَّ الْمَلَائِكَةَ المقربين يقرءونها  Ù…نذ خلق الله السموات وَالْأَرْضَ مَا يَفْتُرُونَ مِنْ قِرَاءَتِهَا. وَمَا مِنْ عَبْدٍ يَقْرَؤُهَا إِلَّا بَعَثَ اللَّهُ إِلَيْهِ مَلَائِكَةً يَحْفَظُونَهُ فِي دِينِهِ وَدُنْيَاهُ، وَيَدْعُونَ لَهُ بِالْمَغْفِرَةِ وَالرَّحْمَةِ (. قَالَ الْحَضْرَمِيُّ: فَجِئْتُ إِلَى أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ نُمَيْرٍ، فَأَلْقَيْتُ هَذَا الْحَدِيثَ عَلَيْهِ، فقال: هذا قَدْ كَفَانَا مَئُونَتَهُ، فَلَا تَعُدْ إِلَيْهِ. قَالَ ابْنُ الْعَرَبِيِّ:" رَوَى إِسْحَاقُ بْنُ بِشْرٍ الْكَاهِلِيُّ عن مالك ابن أَنَسٍ، عَنْ يَحْيَى بْنِ سَعِيدٍ، عَنِ ابْنِ الْمُسَيَّبِ: عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، عَنِ النَّبِيِّ ï·º: (لَوْ يَعْلَمُ النَّاسُ مَا فِي [لَمْ يَكُنْ [الَّذِينَ كَفَرُوا لَعَطَّلُوا الْأَهْلَ وَالْمَالَ وَلَتَعَلَّمُوهَا) . حَدِيثٌ بَاطِلٌ

Angalia Tafsir Qurtub

 

Khabari njema kwa waumini

Mwisho sura inatia habari za furaha kuwa waliamini na kufanya vitendo vizuri yaani amali njema malipo yao ni pepo na wakae humo milele. 

 



Sponsored Posts


  👉    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       👉    2 Jifunze Fiqh       👉    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       👉    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Makundi ya Id-ghamu katika usomaji wa Quran Tajwid
Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu. Soma Zaidi...

image Sababu za kushukasurat an Nasr
Sura hii ni katika sura za mwisho kushuka, huwendakuwa ndio ya mwisho kabisa. Masahaba waliamini kuwa sura hii imetabiri kifo cha Mtume S.A.W Soma Zaidi...

image Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid
Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo. Soma Zaidi...

image Sababu za kushuka surat al alaqa
Asbsb nuzul surat al alaqa, sababu za kushuka surat alaqa. Sura hii imeshuka Makka na ina aya 19. Ni sura ya 96 katika mpangilio wa Quran. Soma Zaidi...

image Aina za usomaji wa Quran
Je kuna aina ngapi zabusomaji wa Quran Soma Zaidi...

image Vifaa saba na herufi saba katika usomaji wa quran
Ni zipi hizo herufi saba, na ni vipi viraa saba katika usomaji wa Quran Soma Zaidi...

image Aina saba za Viraa vya usomaji wa Quran
Post hii inakwenda kukuorodheshea aina saba za viraka vya usomaji wa Quran. Soma Zaidi...

image Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid
Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo. Soma Zaidi...

image Sababu za kushuka kwa surat al qariah
Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume. Soma Zaidi...

image Sababu za kshuka surat al Asr
Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo… Soma Zaidi...