Hoja juu ya kukubalika hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
7.0. SUNNAH NA HADITH.
7.1. Hoja juu ya Kukubalika Hadith.
- Hadith ni chanzo na chem chem ya pili kuwa muongozo wa maisha ya waumini baada ya Qur’an.
“Anachokupeni Mtume chukuweni na anachokukatazeni nacho kiacheni.” (59:7).
“Anayemtii Mtume ameshamtii Mwenyezi Mungu.” (4:80)
Rejea pia Qur’an (52:3-4).
- Zifuatazo ni baadhi ya hoja za wapinzani wa Hadith.
- Hadith hazikufuata mpango kama ulivyo mpangilio wa Qur’an wakati wa kushuka, kupangwa, kuhifadhiwa na kuandikwa.
Udhaifu wa dai hili;
- Kutoandikwa kwa Hadith kama ilivyoandikwa Qur’an sio hoja na sababu ya kutokubalika Hadith.
- Mtume mwenyewe aliwakataza Maswahaba kuandika Hadith wakati wa uhai wake.
- Baada ya kufa Mtume (s.a.w), waislamu waligawanyika makundi tofauti yanayopingana, na hata kuweza kubuni maneno na kudai kuwa ni Hadith za Mtume (s.a.w). Je utajuaje Hadith zilizosahihi?
Udhaifu wa Hoja hii;
- Kuna Wanachuoni wenye msimamo madhubuti waliobobea katika elimu ya Hadith na hawakujihusisha na migogoro yeyote iliyozuka.
- Vigezo vya kisayansi kama Isnad, Riwaya na Matin vilitumika katika kuchambua usahihi na udhaifu wa Hadith.
- Hadith zilikusanywa na kuandikwa muda mrefu baada ya kufa Mtume (s.a.w) na Maswahaba. Je kuna ushahidi gani unaothibitisha kuwa maneno yaliyosemwa ni ya mtume (s.a.w)?
Udhaifu wa Hoja hii;
- Sunnah ya Mtume (s.a.w) ni maelezo juu ya maisha yake ambayo maswahaba walirithishana baada ya kutawafu (kufa) Mtume.
- Ukusanyaji na uandishi wa Hadith ulifanyika kwa utaalamu wa kisayansi katika kubaini ukweli wa Hadith.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 ai web app 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Sababu za kushuka kwa surat Dhuha
Sura hii imetermka Makkah na ina aya 11. Sura hii ni moja ya sura ambazo zimeshuka mwanzoni wakati ambapo Mtume ameanza kazi ya utume.
Soma Zaidi...Aina za Madda twabiy kwenye usomaji wa Quran
Madda zimegawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo ni madda twabiy na madda fariy
Soma Zaidi...