Hoja juu ya kukubalika hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
7.0. SUNNAH NA HADITH.
7.1. Hoja juu ya Kukubalika Hadith.
- Hadith ni chanzo na chem chem ya pili kuwa muongozo wa maisha ya waumini baada ya Qur’an.
“Anachokupeni Mtume chukuweni na anachokukatazeni nacho kiacheni.” (59:7).
“Anayemtii Mtume ameshamtii Mwenyezi Mungu.” (4:80)
Rejea pia Qur’an (52:3-4).
- Zifuatazo ni baadhi ya hoja za wapinzani wa Hadith.
- Hadith hazikufuata mpango kama ulivyo mpangilio wa Qur’an wakati wa kushuka, kupangwa, kuhifadhiwa na kuandikwa.
Udhaifu wa dai hili;
- Kutoandikwa kwa Hadith kama ilivyoandikwa Qur’an sio hoja na sababu ya kutokubalika Hadith.
- Mtume mwenyewe aliwakataza Maswahaba kuandika Hadith wakati wa uhai wake.
- Baada ya kufa Mtume (s.a.w), waislamu waligawanyika makundi tofauti yanayopingana, na hata kuweza kubuni maneno na kudai kuwa ni Hadith za Mtume (s.a.w). Je utajuaje Hadith zilizosahihi?
Udhaifu wa Hoja hii;
- Kuna Wanachuoni wenye msimamo madhubuti waliobobea katika elimu ya Hadith na hawakujihusisha na migogoro yeyote iliyozuka.
- Vigezo vya kisayansi kama Isnad, Riwaya na Matin vilitumika katika kuchambua usahihi na udhaifu wa Hadith.
- Hadith zilikusanywa na kuandikwa muda mrefu baada ya kufa Mtume (s.a.w) na Maswahaba. Je kuna ushahidi gani unaothibitisha kuwa maneno yaliyosemwa ni ya mtume (s.a.w)?
Udhaifu wa Hoja hii;
- Sunnah ya Mtume (s.a.w) ni maelezo juu ya maisha yake ambayo maswahaba walirithishana baada ya kutawafu (kufa) Mtume.
- Ukusanyaji na uandishi wa Hadith ulifanyika kwa utaalamu wa kisayansi katika kubaini ukweli wa Hadith.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 web hosting π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Kitabu cha Afya π4 Bongolite - Game zone - Play free game π5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π6 ai web app
Post zinazofanana:
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa
Soma Zaidi...ASBAB-NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN
ASBAB NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN Quran imeteremka kwa muda wa miaka 23 kidogokido.
Soma Zaidi...HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA
SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina iβrab ( Ω Ω).
Soma Zaidi...Quran si njozi za mvurugano alizoota Mtume Muhammad
(ii)Dai kuwa Qur-an ni zao la njozi za Mtume (s.
Soma Zaidi...Aasbab Nuzul surat Ash sharh: sababu za kushuka alam nashrah (surat Ash sharh)
Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh.
Soma Zaidi...