Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun).
Surat at Tin ni sura ya 95 katika mpangilio wa Quran kama ilivyoandikwa kwenye Mashaf. Sura hii ina aya 8 na imeshuka Makkah. Mtume s.a.w alikuwa akiisoma sura hii wakati anaposwali swala ya safari.
Amesimulia Ala Baraa bin Azib kuwa alikuwa Mtume s.a.w akisoma katika swala za safa katika moja ya rakaa mbili alikuwa akisoma surat at Tin (watin wazaytun)……
Sababu za kushuka kwake.
Hakuna nukuu hasa za kuonyesha kama kulikuwa na tukio maalumu lililopelekea kushuka sura hii. Kuna baadhi ya kauli ni kuwa kuna swahaba alimfuata Mtumr s.a.w navkumuuliza kuhusu watu ambao ni wazee, na wana matatizo ya kusahau, ama ya akili, vipi amali zao je wataendelea kulipwa? Hapo ndipo ikashuka sura hii.
Sura hii imrjibu vyema swali hilo. Allah anasema wale waliokuwa na imani na kufanya matendo mema basi wana wao malipo yasiokatika.
Maana ya tin, zaitun na mlima sinai
Wametofautiana wafasiri kuhusu maana ya tin na zaitun. Wapo waliosema kuwa hii ni misikiti, yaani msikiti wa Damaska na wa palestina Bayt al Maqsid.
Ila uhakika wa maneno na kaulicyenye nguvu makusudio hapa ni matunda mawili haya yani tunda Tini na tunda Zaituni. Matunda haya yanafahamika kwa kuwa navladha nzuri na manufaa makubwa kwa afya. Allah anaapia kwa kitu chochote kile akitakacho.
Makusudio ya mlima sinai, huu ni mlima ambao Nabii Musa alikuwa akizungunza na Allah. Na Mji wa amani uliotajwa makusudio ni Makkah ambapo kuna msikito mtukufu zaidi.
Ujumla wa sura hii
Sura hii Allah ameanza kuapa kisha akatupa masingatio kuwa hakika mwanadamu ameumbwa katika umbo zuri. Kisha akatupa mazingatio kuwa mwanadamu huyu aliyekuwa katika umbo zuri endapo atafanyavmatendo mema atabakia katika hadhi yake ya juu. Na endapo atamuasi Allah atushushwa awe na hadhi ya chini kabisa katika wenye hadhi za chini.
Allah akatupa mazingatio menginr kuwa wale wanaomuamini Allah ana kufanya matendo mema wana wao malipo yasiokatika.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah.
Soma Zaidi...Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya.
Soma Zaidi...Mada zipo katika makundi mawili ambayo ni madda far-iy na mdada twab-iy.
Soma Zaidi...Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii
Soma Zaidi...